Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 15.5
Bible en Swahili de l’est


Prophétie sur Moab

1 Ufunuo juu ya Moabu. Maana katika usiku mmoja Ari wa Moabu umeharibiwa kabisa na kuangamizwa; maana katika usiku mmoja Kiri wa Moabu umeharibiwa kabisa na kuangamizwa.
Ezéchiel 25.8-25.11 Esaïe 11.14 Amos 2.1-2.3 Nombres 21.28 Esaïe 14.28
2 Wanapanda juu hata Bayithi na Diboni, mpaka mahali palipo juu ili walie; juu ya Nebo na juu ya Medeba Wamoabi wanalia; Wana upaa juu ya vichwa vyao vyote; kila ndevu zimenyolewa.
Lévitique 21.5 Jérémie 48.1 Jérémie 48.18 Esaïe 3.24 Deutéronome 34.1
3 Wanajivika nguo za magunia katika njia kuu zao; juu ya dari zao, na katika mitaa yao, kila mtu analia, anamwaga machozi.
Jonas 3.6-3.8 Esaïe 22.1 2 Rois 6.30 Esaïe 22.4 2 Samuel 3.31
4 Heshboni analia na Eleale; mpaka Yahasa sauti ya kulia kwao inasikiwa; hata watu wa Moabu waliovaa silaha wanapiga kelele sana kwa sababu hiyo; nafsi yake inatetemeka ndani yake.
Jérémie 48.34 Job 7.15-7.16 Nombres 21.23 Jérémie 20.18 Apocalypse 9.6
5 Moyo wangu unamlilia Moabu; wakuu wake wanakimbilia Soari kama ndama wa miaka mitatu; kwa maana wanapanda mbavu za Luhithi wakilia; maana katika njia iendayo hata Horonaimu wanapaliza sauti ya kukata tamaa.
Jérémie 48.5 Jérémie 4.20 2 Samuel 15.23 Luc 19.41-19.44 Jérémie 13.17
6 Kwa maana maji ya Nimrimu yamekuwa mahali palipoharibika, kwa kuwa majani yamekauka, miche imenyauka, majani mabichi yamekoma.
Nombres 32.36 Joël 1.10-1.12 Nombres 32.3 Habakuk 3.17-3.18 Jérémie 48.34
7 Kwa hiyo vitu walivyojipatia tele, na akiba yao, wanavichukua hata kijito cha mierebi.
Jérémie 48.36 Esaïe 10.6 Esaïe 30.6 Esaïe 10.14 Esaïe 5.29
8 Maana kilio hicho kimezunguka mipaka ya Moabu, malalamiko yao yamefika hata Eglaimu, na malalamiko yao hata Beer-Elimu.
Jérémie 48.31-48.34 Esaïe 15.2-15.5 Jérémie 48.20-48.24 Ezéchiel 47.10
9 Maana maji ya Dimoni yamejaa damu; maana ninaweka tayari msiba mpya juu ya Dimoni, simba juu ya watu wa Moabu waliokimbia, na juu ya mabaki yao.
2 Rois 17.25 Jérémie 50.17 Jérémie 15.3 Lévitique 26.18 Amos 5.19

Cette Bible est dans le domaine public.