Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Cantique 5.9
Bible en Swahili de l’est


Le jeune homme

1 Naingia bustanini mwangu, umbu langu, bibi arusi, Nachuma manemane yangu na rihani, Nala sega la asali na asali yangu, Nanywa divai yangu na maziwa. Kaleni, rafiki zangu, kanyweni, Naam, nyweni sana, wapendwa wangu.
Cantique 6.2 Cantique 4.16 Esaïe 61.11 Jean 3.29 Jean 15.14-15.15

La jeune femme

2 Nalikuwa nimelala, lakini moyo wangu u macho, Sikiliza! Mpendwa wangu anabisha! Nifungulie, umbu langu, mpenzi wangu, Hua wangu, mkamilifu wangu, Kwa maana kichwa changu kimelowa umande, Nywele zangu zina manyunyu ya usiku.
Cantique 2.14 Cantique 6.9 Cantique 8.7 Apocalypse 3.20 Esaïe 52.14
3 Nimeivua kanzu yangu; niivaeje? Nimeitawadha miguu; niichafueje?
Luc 11.7 Matthieu 25.5 Matthieu 26.38-26.43 Proverbes 22.13 Romains 7.22-7.23
4 Mpendwa wangu aliutia mkono wake tunduni, Na moyo wangu ukachomeka kwa ajili yake.
Cantique 1.4 Actes 16.14 Philippiens 2.13 2 Corinthiens 8.1-8.2 Psaumes 110.3
5 Nikaondoka nimfungulie mpendwa wangu; Mikono yangu ilidondoza manemane, Na vidole vyangu matone ya manemane, Penye vipini vya komeo.
Cantique 5.13 2 Corinthiens 7.9-7.11 Cantique 4.13-4.14 Apocalypse 3.20 2 Corinthiens 7.7
6 Nalimfungulia mpendwa wangu, Lakini mpendwa wangu amegeuka amepita; (Nimezimia nafsi yangu aliponena), Nikamtafuta, nisimpate, Nikamwita, asiniitikie.
Cantique 5.2 Esaïe 8.17 Cantique 6.1 Psaumes 80.4 Esaïe 58.2
7 Walinzi wazungukao mjini waliniona, Wakanipiga na kunitia jeraha, Walinzi walindao kuta zake Wakaninyang’anya shela yangu.
Cantique 3.3 Esaïe 62.6 Cantique 8.11 Osée 6.5 Apocalypse 17.5-17.6
8 Nawasihi, enyi binti za Yerusalemu, Ninyi mkimwona mpendwa wangu, Ni nini mtakayomwambia? Ya kwamba nazimia kwa mapenzi.
Cantique 2.7 Cantique 2.5 Psaumes 42.1-42.3 Jacques 5.16 Cantique 3.5

Les filles de Jérusalem

9 Mpendwa wa namna gani ni mpendwa wako, Wewe uliye mzuri katika wanawake, Mpendwa wa namna gani ni mpendwa wako, Hata wewe utusihi hivyo?
Cantique 1.8 Cantique 6.1 Psaumes 45.13 Cantique 6.9-6.10 Psaumes 87.3

La jeune femme

10 Mpendwa wangu ni mweupe, tena mwekundu, Mashuhuri miongoni mwa elfu kumi;
Psaumes 45.2 Psaumes 45.17 Esaïe 66.19 Esaïe 59.19 1 Samuel 16.12
11 Kichwa chake ni kama dhahabu safi sana, Nywele zake ni za ukoka, nyeusi kama kunguru;
Ephésiens 1.21-1.22 Apocalypse 1.14 Cantique 5.2 Daniel 7.9 Daniel 2.37-2.38
12 Macho yake ni kama hua penye vijito, Wakioga kwa maziwa, wakiikalia mito iliyojaa;
Cantique 1.15 Cantique 4.1 Hébreux 4.13
13 Mashavu yake ni kama matuta ya rihani, Ambayo hufanyizwa manukato; Midomo yake ni kama nyinyoro, Inadondoza matone ya manemane;
Cantique 1.10 Cantique 6.2 Cantique 2.1 Apocalypse 21.23 Luc 4.22
14 Mikono yake ni kama mianzi ya dhahabu, lliyopambwa kwa zabarajadi; Kiwiliwili chake kama kazi ya pembe, Iliyonakishiwa kwa yakuti samawi;
Exode 24.10 Esaïe 54.11 Ezéchiel 1.26-1.28 Psaumes 44.4-44.7 Esaïe 52.13
15 Miguu yake ni kama nguzo za marimari, Zilizowekwa juu ya misingi ya dhahabu; Sura yake ni kama Lebanoni, Ni bora mfano wa mierezi;
1 Rois 4.33 Actes 2.28 Apocalypse 1.15-1.16 Matthieu 17.2 Zacharie 9.17
16 Kinywa chake kimejaa maneno matamu, Ndiye mzuri sana pia pia. Ni huyu mpendwa wangu, ni huyu rafiki yangu, Enyi binti za Yerusalemu.
Cantique 7.9 Psaumes 45.2 Esaïe 9.6-9.7 Jacques 2.23 Psaumes 119.103

Cette Bible est dans le domaine public.