Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Cantique 5.10
Bible en Swahili de l’est


1 Naingia bustanini mwangu, umbu langu, bibi arusi, Nachuma manemane yangu na rihani, Nala sega la asali na asali yangu, Nanywa divai yangu na maziwa. Kaleni, rafiki zangu, kanyweni, Naam, nyweni sana, wapendwa wangu.Cantique 6.2 Cantique 4.16 Esaïe 61.11 Jean 3.29 Jean 15.14-15.15
2 Nalikuwa nimelala, lakini moyo wangu u macho, Sikiliza! Mpendwa wangu anabisha! Nifungulie, umbu langu, mpenzi wangu, Hua wangu, mkamilifu wangu, Kwa maana kichwa changu kimelowa umande, Nywele zangu zina manyunyu ya usiku.Cantique 2.14 Cantique 6.9 Apocalypse 3.20 Cantique 8.7 Matthieu 26.40-26.41
3 Nimeivua kanzu yangu; niivaeje? Nimeitawadha miguu; niichafueje?Luc 11.7 Proverbes 22.13 Romains 7.22-7.23 Proverbes 3.28 Proverbes 13.4
4 Mpendwa wangu aliutia mkono wake tunduni, Na moyo wangu ukachomeka kwa ajili yake.Philippiens 2.13 2 Corinthiens 8.1-8.2 Psaumes 110.3 1 Rois 3.26 Esaïe 26.8-26.9
5 Nikaondoka nimfungulie mpendwa wangu; Mikono yangu ilidondoza manemane, Na vidole vyangu matone ya manemane, Penye vipini vya komeo.Cantique 5.13 Apocalypse 3.20 2 Corinthiens 7.7 Ephésiens 3.17 Luc 12.36
6 Nalimfungulia mpendwa wangu, Lakini mpendwa wangu amegeuka amepita; (Nimezimia nafsi yangu aliponena), Nikamtafuta, nisimpate, Nikamwita, asiniitikie.Cantique 5.2 Psaumes 30.7 Psaumes 69.3 Psaumes 28.1 Psaumes 88.9-88.14
7 Walinzi wazungukao mjini waliniona, Wakanipiga na kunitia jeraha, Walinzi walindao kuta zake Wakaninyang’anya shela yangu.Cantique 3.3 Psaumes 141.5 Hébreux 12.2 1 Corinthiens 4.10-4.13 Philippiens 3.6
8 Nawasihi, enyi binti za Yerusalemu, Ninyi mkimwona mpendwa wangu, Ni nini mtakayomwambia? Ya kwamba nazimia kwa mapenzi.Cantique 2.7 Cantique 2.5 Psaumes 42.1-42.3 Psaumes 119.81-119.83 Psaumes 77.1-77.3
9 Mpendwa wa namna gani ni mpendwa wako, Wewe uliye mzuri katika wanawake, Mpendwa wa namna gani ni mpendwa wako, Hata wewe utusihi hivyo?Cantique 6.1 Cantique 1.8 Cantique 6.9-6.10 Psaumes 87.3 Matthieu 16.13-16.17
10 Mpendwa wangu ni mweupe, tena mwekundu, Mashuhuri miongoni mwa elfu kumi;Psaumes 45.2 Esaïe 66.19 Esaïe 59.19 1 Samuel 16.12 Cantique 2.1
11 Kichwa chake ni kama dhahabu safi sana, Nywele zake ni za ukoka, nyeusi kama kunguru;Cantique 5.2 Daniel 7.9 Daniel 2.37-2.38 Cantique 7.5 Ephésiens 1.21-1.22
12 Macho yake ni kama hua penye vijito, Wakioga kwa maziwa, wakiikalia mito iliyojaa;Cantique 4.1 Cantique 1.15 Hébreux 4.13
13 Mashavu yake ni kama matuta ya rihani, Ambayo hufanyizwa manukato; Midomo yake ni kama nyinyoro, Inadondoza matone ya manemane;Cantique 1.10 Cantique 6.2 Cantique 2.1 Psaumes 89.15 Cantique 3.6
14 Mikono yake ni kama mianzi ya dhahabu, lliyopambwa kwa zabarajadi; Kiwiliwili chake kama kazi ya pembe, Iliyonakishiwa kwa yakuti samawi;Exode 24.10 Esaïe 54.11 Ezéchiel 1.26-1.28 Psaumes 44.4-44.7 Esaïe 52.13
15 Miguu yake ni kama nguzo za marimari, Zilizowekwa juu ya misingi ya dhahabu; Sura yake ni kama Lebanoni, Ni bora mfano wa mierezi;1 Rois 4.33 Matthieu 17.2 Zacharie 9.17 Cantique 2.14 Exode 26.19
16 Kinywa chake kimejaa maneno matamu, Ndiye mzuri sana pia pia. Ni huyu mpendwa wangu, ni huyu rafiki yangu, Enyi binti za Yerusalemu.Cantique 7.9 Psaumes 45.2 Esaïe 9.6-9.7 Cantique 2.3 Psaumes 89.6

Cette Bible est dans le domaine public.