Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ecclésiaste 11.8
Bible en Swahili de l’est


Activité saine et réjouissance

1 Tupa chakula chako usoni pa maji; Maana utakiona baada ya siku nyingi.
Proverbes 19.17 Matthieu 10.42 Hébreux 6.10 Ecclésiaste 11.6 Galates 6.8-6.10
2 Uwagawie sehemu watu saba, hata wanane; Maana hujui baa gani litakalokuwa juu ya nchi.
1 Timothée 6.18-6.19 Psaumes 112.9 Michée 5.5 Job 5.19 Proverbes 6.16
3 Mawingu yakiwa yamejaa mvua, Yataimimina juu ya nchi; Na mti ukianguka kuelekea kusini, au kaskazini, Paangukapo ule mti, papo hapo utalala.
Psaumes 65.9-65.13 1 Rois 18.45 1 Jean 3.17 Luc 13.7 Luc 16.22-16.26
4 Mwenye kuuangalia upepo hatapanda; Naye ayatazamaye mawingu hatavuna.
Proverbes 22.13 Proverbes 3.27 Proverbes 20.4
5 Kama vile wewe usipojua njia ya upepo ni ipi, wala jinsi mifupa ikuavyo tumboni mwake mja mzito; kadhalika huijui kazi ya Mungu, afanyaye mambo yote.
Jean 3.8 Ecclésiaste 8.17 Psaumes 92.5 Job 5.9 Job 36.24-36.33
6 Asubuhi panda mbegu zako, Wala jioni usiuzuie mkono wako. Kwa maana wewe hujui ni zipi zitakazofanikiwa,kama ni hii au hii,au kama zote zitafaa sawasawa.
Ecclésiaste 9.10 2 Timothée 4.2 Marc 4.26-4.29 2 Corinthiens 9.6 Esaïe 55.10
7 Kweli nuru ni tamu, tena ni jambo la kupendeza macho kutazama jua.
Ecclésiaste 7.11 Matthieu 5.45 Psaumes 84.11 Proverbes 29.13 Job 33.30
8 Naam, mtu akiishi miaka mingi, na aifurahie yote; lakini na azikumbuke siku zijazo za giza, kwa maana zitakuwa nyingi. Mambo yote yajayo ni ubatili.
Jude 1.18 Ecclésiaste 4.16 Ecclésiaste 7.14 Ecclésiaste 2.21-2.23 Ecclésiaste 4.8

Le moment favorable pour rechercher Dieu

9 Wewe kijana, uufurahie ujana wako, na moyo wako ukuchangamshe siku za ujana wako, ukaziendee njia za moyo wako, na katika maono ya macho yako, lakini ujue wewe ya kwamba kwa ajili ya hayo yote Mungu atakuleta hukumuni.
Ecclésiaste 12.14 Ecclésiaste 3.17 Ecclésiaste 2.10 Romains 14.10 Job 31.7
10 Kwa hiyo ondoa majonzi moyoni mwako, nawe uuondoe ubaya mwilini mwako; kwa maana ujana ni ubatili, na utu uzima pia.
2 Timothée 2.22 2 Corinthiens 7.1 Ecclésiaste 12.1 Job 20.11 Ecclésiaste 1.2

Cette Bible est dans le domaine public.