Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Exode 40.12
Bible en Swahili de l’est


Mise en place du tabernacle

1 Bwana akanena na Musa, na kumwambia,
2 Siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza utaisimamisha hiyo maskani ya hema ya kukutania.
Exode 13.4 Exode 26.30 Exode 12.1-12.2 Exode 40.17-40.19 Exode 27.21
3 Nawe utatia ndani yake sanduku la ushuhuda, nawe utalisitiri hilo sanduku kwa pazia.
Nombres 4.5 Exode 35.12 Apocalypse 11.19 Exode 40.20-40.21 Exode 36.35-36.36
4 Nawe utaleta meza na kuitia ndani, na kuviweka sawasawa vile vitu juu yake; kisha utakileta ndani kile kinara cha taa, na kuziwasha taa zake.
Lévitique 24.5-24.6 Exode 25.23-25.39 Lévitique 24.8 Exode 37.10-37.24 Exode 26.35-26.36
5 Kisha utaisimamisha madhabahu ya dhahabu kwa kufukizia uvumba mbele ya sanduku la ushuhuda, na kulitia pazia mlangoni mwa hiyo maskani.
Hébreux 10.19-10.22 Exode 30.1-30.5 Exode 26.36-26.37 1 Jean 2.1-2.2 Exode 35.25-35.28
6 Kisha utaweka madhabahu ya kuteketeza sadaka mbele ya mlango wa maskani ya hema ya kukutania.
Exode 40.29 Ephésiens 1.6-1.7 Exode 38.1-38.7 Exode 27.1-27.8 1 Jean 2.2
7 Kisha utaliweka birika kati ya hema ya kukutania na hiyo madhabahu, nawe utatia maji ndani yake.
1 Jean 1.7 Hébreux 10.22 Tite 3.5 Zacharie 13.1 Apocalypse 1.5-1.6
8 Kisha utausimamisha ukuta wa ua kuuzunguka pande zote, na kuitundika sitara ya lango la ua.
Exode 38.9-38.20 Exode 40.33 Exode 27.9-27.19 Ephésiens 4.11-4.12 Matthieu 16.18
9 Kisha utayatwaa mafuta ya kutiwa, na kuitia mafuta hiyo maskani, na kila kitu kilicho ndani yake, na kuiweka iwe takatifu, na vyombo vyake vyote; nayo itakuwa takatifu.
Lévitique 8.10 Psaumes 45.7 2 Corinthiens 1.4 Jean 3.34 Esaïe 61.1
10 Kisha utaitia mafuta madhabahu ya kuteketeza sadaka, na vyombo vyake vyote; na kuiweka takatifu madhabahu; na hiyo madhabahu itakuwa takatifu sana.
Exode 29.36-29.37 Hébreux 7.26 1 Corinthiens 1.30 Luc 1.35 Lévitique 8.11
11 Kisha utalitia mafuta birika na tako lake, na kuliweka liwe takatifu.
12 Kisha utamleta Haruni na wanawe hapo mlangoni pa hema ya kukutania, nawe utawaosha kwa maji.
Lévitique 8.1-8.13 Luc 1.35 Romains 8.3 Jean 3.34 Matthieu 3.16
13 Kisha utamvika Haruni mavazi matakatifu; nawe utamtia mafuta, na kumweka awe mtakatifu, ili apate kunitumikia katika kazi ya ukuhani.
Exode 28.41 Jean 3.34 Esaïe 61.1 1 Jean 2.27 Jean 17.19
14 Kisha utawaleta wanawe, na kuwavika kanzu zao;
Romains 8.30 Romains 13.14 Esaïe 61.10 1 Corinthiens 1.30 1 Corinthiens 1.9
15 nawe utawatia mafuta kama ulivyomtia mafuta baba yao, ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani; na huko kutiwa mafuta kwao kutakuwa ni kwa ukuhani wa milele katika vizazi vyao vyote.
Nombres 25.13 Psaumes 110.4 Hébreux 7.17-7.24 Hébreux 5.1-5.14 Hébreux 8.1-8.10
16 Musa akafanya hayo yote; kama yote Bwana aliyoagiza ndivyo alivyofanya.
Deutéronome 4.1 Exode 40.17-40.32 Matthieu 28.20 Esaïe 8.20 Deutéronome 12.32
17 Hata mwezi wa kwanza wa mwaka wa pili, siku ya kwanza ya mwezi ile maskani ilisimamishwa.
Nombres 7.1 Exode 40.1-40.2 Nombres 9.1
18 Musa akaisimamisha maskani, akayaweka matako yake, akazisimamisha mbao zake akayatia mataruma yake, akazisimamisha nguzo zake.
Esaïe 33.24 Exode 26.15-26.30 Matthieu 16.18 Jean 1.14 1 Pierre 1.5
19 Akaitanda hema juu ya maskani, akakitia kifuniko cha hema juu yake; kama Bwana alivyomwamuru Musa.
Exode 26.1-26.14 Exode 36.8-36.19
20 Akautwaa ule ushuhuda, akautia ndani ya sanduku, akaiweka miti ya kuchukulia juu ya sanduku, akakiweka kiti cha rehema juu ya sanduku;
Exode 16.34 Exode 40.3 Exode 37.6-37.9 Hébreux 10.19-10.21 Psaumes 40.8
21 kisha akalileta sanduku akalitia ndani ya maskani, naye akalitundika pazia la sitara, akalisitiri sanduku la ushuhuda; kama Bwana alivyomwamuru Musa.
Exode 40.3 Exode 26.33 Exode 35.12 Hébreux 10.19-10.20
22 Akaitia meza ndani ya hema ya kukutania, upande wa maskani ulioelekea kaskazini, nje ya pazia.
Exode 26.35 Ephésiens 3.8 Exode 40.24 Jean 6.53-6.57
23 Akaipanga ile mikate juu yake mbele za Bwana; kama Bwana alivyomwamuru Musa.
Exode 40.4 Exode 25.30 Hébreux 9.2 Matthieu 12.4
24 Kisha akakitia kinara cha taa ndani ya hema ya kukutania, kuikabili ile meza, upande wa maskani ulioelekea kusini.
Apocalypse 1.20 Jean 1.1 Apocalypse 2.5 Jean 8.12 Exode 26.35
25 Kisha akaziwasha taa zake mbele za Bwana, kama Bwana alivyomwamuru Musa.
Exode 25.37 Exode 40.4 Apocalypse 4.5
26 Akaitia madhabahu ya dhahabu ndani ya hema ya kukutania mbele ya pazia.
Exode 40.5 Jean 11.42 Matthieu 23.19 Exode 30.1-30.10 Jean 17.1-17.26
27 Akafukiza juu yake uvumba wa manukato kama Bwana alivyomwamuru Musa.
Exode 30.7
28 Akalitia pazia la mlango wa maskani.
Exode 40.5 Hébreux 10.19-10.20 Exode 38.9-38.19 Exode 26.36-26.37 Jean 10.9
29 Akaiweka madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa mlangoni pa maskani ya kukutania, akatoa sadaka ya kuteketezwa juu yake, na sadaka ya unga; kama Bwana alivyomwamuru Musa.
Exode 40.6 Exode 27.1-27.8 Romains 3.24-3.26 Hébreux 9.12 Exode 38.1-38.7
30 Akaliweka birika kati ya hema ya kukutania na madhabahu, akatia maji ndani yake ya kuoshea.
Exode 40.7 Exode 38.8 Hébreux 10.22 Exode 30.18-30.21 Ezéchiel 36.25
31 Musa na Haruni, na wanawe wakanawa mikono yao na miguu yao ndani yake;
Jean 13.10 1 Jean 1.7 Psaumes 26.6 Exode 30.19-30.20 1 Jean 1.9
32 hapo walipoingia hema ya kukutania, na hapo walipoikaribia madhabahu walinawa kama Bwana alivyomwamuru Musa.
Exode 40.19 Exode 30.19-30.20 Psaumes 73.19
33 Akausimamisha ukuta wa ua kuizunguka maskani na madhabahu, akalitundika pazia la mlango wa ule ua. Basi Musa akaimaliza hiyo kazi.
Exode 40.8 Exode 27.9-27.16 Jean 4.34 Hébreux 4.14-4.16 1 Rois 6.9

Présence de la gloire de l’Éternel sur le tabernacle

34 Ndipo lile wingu likaifunikiza hema ya kukutania, na huo utukufu wa Bwana ukaijaza maskani.
Nombres 9.15-9.23 Apocalypse 15.8 Aggée 2.7 1 Rois 8.10-8.11 Exode 33.9
35 Wala Musa hakuweza kuliingia hema la kukutania, kwa sababu lile wingu lilikaa juu yake, na huo utukufu wa Bwana ukaijaza maskani.
1 Rois 8.11 Apocalypse 15.8 2 Chroniques 5.13-5.14 2 Chroniques 7.2 Esaïe 6.4
36 Na hapo lile wingu lilipoinuliwa kutoka juu ya maskani, wana wa Israeli wakaenda mbele katika safari zao zote,
Néhémie 9.19 Nombres 9.17 2 Corinthiens 5.19-5.20 Exode 13.21-13.22 Psaumes 78.14
37 bali kama lile wingu halikuinuliwa, wakati ule hawakusafiri hata siku ile lilipoinuliwa tena.
Nombres 9.19-9.22 Psaumes 31.15
38 Kwa maana lile wingu la Bwana lilikuwa juu ya maskani wakati wa mchana, na mlikuwa na moto ndani yake wakati wa usiku, mbele ya macho ya nyumba ya Israeli katika safari zao zote.
Exode 13.21 Nombres 9.15 Psaumes 78.14 Psaumes 105.39 Esaïe 4.5-4.6

Cette Bible est dans le domaine public.