Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Exode 4.2
Bible en Swahili de l’est


1 Musa akajibu akasema, Lakini, tazama, hawataniamini, wala hawataisikia sauti yangu; maana watasema, Bwana hakukutokea.
Exode 3.18 Actes 7.25 Exode 4.31 Ezéchiel 3.14 Jérémie 1.6
2 Bwana akamwambia, Ni nini hiyo uliyo nayo mkononi mwako? Akasema, Ni fimbo.
Exode 4.17 Exode 4.20 Lévitique 27.32 Psaumes 110.2 Michée 7.14
3 Akamwambia, Itupe chini; akaitupa chini, nayo ikawa nyoka; Musa akakimbia mbele yake.
Exode 4.17 Exode 7.10-7.15 Amos 5.19
4 Bwana akamwambia Musa, Nyosha mkono wako, kamshike mkia; (akaunyosha mkono wake akamshika, naye akageuka kuwa fimbo mkononi mwake;)
Actes 28.3-28.6 Jean 2.5 Psaumes 91.13 Luc 10.19 Genèse 22.1-22.2
5 ili kwamba wapate kusadiki ya kwamba Bwana, Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka, Mungu wa Yakobo, amekutokea.
Exode 19.9 Genèse 48.3 Exode 3.15 Exode 4.31 Genèse 12.7
6 Bwana akamwambia tena, Sasa tia mkono wako kifuani mwako. Akautia mkono wake kifuani mwake; naye alipoutoa, kumbe! Mkono wake ulikuwa una ukoma, umekuwa mweupe kama theluji.
Nombres 12.10 2 Rois 5.27
7 Akasema, Tia mkono wako kifuani mwako tena. Akautia mkono wake kifuani mwake tena, na alipoutoa kifuani mwake, kumbe! Umerudia hali ya mwili wake.
2 Rois 5.14 Deutéronome 32.39 Matthieu 8.3 Nombres 12.13-12.15
8 Basi itakuwa, wasipokusadiki, wala kuisikiliza sauti ya ishara ya kwanza, wataisikiliza sauti ya ishara ya pili.
2 Rois 5.7 Jean 12.37 Job 5.18 Exode 4.30-4.31 Esaïe 28.10
9 Kisha itakuwa wasipoamini hata ishara hizo mbili, wala kuisikiliza sauti yako, basi, yatwae maji ya mtoni uyamwage juu ya nchi kavu, na yale maji uyatwaayo mtoni yatakuwa damu juu ya nchi kavu.
Exode 7.19-7.25 Exode 1.22 Matthieu 7.2
10 Musa akamwambia Bwana Ee Bwana, mimi si msemaji, tokea zamani, wala tokea hapo uliposema na mtumishi wako; maana mimi si mwepesi wa kusema, na ulimi wangu ni mzito.
Exode 6.12 Jérémie 1.6 Actes 7.22 Exode 4.1 2 Corinthiens 11.6
11 Bwana akamwambia, Ni nani aliyekifanya kinywa cha mwanadamu? Au ni nani afanyaye mtu kuwa bubu au kiziwi, au mwenye kuona, au kuwa kipofu? Si mimi, Bwana?
Amos 3.6 Psaumes 94.9 Psaumes 146.8 Jérémie 1.6 Ezéchiel 3.26-3.27
12 Basi sasa, enenda, nami nitakuwa pamoja na kinywa chako, na kukufundisha utakalolinena.
Jérémie 1.9 Marc 13.11 Matthieu 10.19-10.20 Luc 21.14-21.15 Luc 12.11-12.12
13 Akasema, Ee Bwana, nakuomba, tuma kwa mkono wake huyo utakayemtuma.
Jonas 1.3 Exode 4.1 1 Rois 19.4 Jérémie 1.6 Genèse 24.7
14 Hasira ya Bwana ikawaka juu ya Musa, akasema, Je! Hayuko Haruni, ndugu yako, Mlawi? Najua ya kuwa yeye aweza kusema vizuri. Pamoja na hayo, tazama, anakuja kukulaki; naye atakapokuona, atafurahi moyoni mwake.
Exode 4.27 1 Samuel 10.1-10.7 2 Corinthiens 7.6-7.7 2 Corinthiens 2.13 1 Rois 11.9
15 Nawe utasema naye, na kuyatia maneno kinywani mwake; nami nitakuwa pamoja na kinywa chako, na pamoja na kinywa chake, na kuwafundisheni mtakayofanya.
Esaïe 51.16 Nombres 23.16 Nombres 23.5 Nombres 23.12 Deutéronome 18.18
16 Naye atakuwa msemaji wako kwa watu, hata yeye atakuwa mfano wa kinywa kwako, nawe utakuwa mfano wa Mungu kwake.
Exode 7.1-7.2 Exode 18.19 Psaumes 82.6 Jean 10.34-10.35
17 Nawe utatwaa fimbo hii mkononi mwako, na kwa hiyo utazifanya zile ishara.
Exode 4.2 Exode 7.9-7.20 1 Corinthiens 1.27
18 Basi Musa akaenda na kurejea kwa Yethro mkwewe, na kumwambia, Nipe ruhusa niende, nakusihi, niwarudie hao ndugu zangu walioko Misri, nipate kuwaona kwamba wako hai hata sasa. Yethro akamwambia Musa, Haya, nenda kwa amani.
Exode 3.1 1 Samuel 1.17 Genèse 45.3 Actes 15.36 Actes 16.36

Retour de Moïse en Égypte

19 Bwana akamwambia Musa huko Midiani, Haya, nenda, karudi Misri; kwa kuwa wale watu wote waliokutaka uhai wako wamekwisha kufa.
Exode 2.23 Exode 2.15 Matthieu 2.20
20 Basi Musa akamchukua mkewe na wanawe, na kuwapandisha juu ya punda, naye akarudi mpaka nchi ya Misri; na Musa akaichukua ile fimbo ya Mungu mkononi mwake.
Exode 17.9 Nombres 20.8-20.9 Exode 4.17 Nombres 20.11 Exode 18.3-18.4
21 Bwana akamwambia Musa, Hapo utakaporudi Misri, angalia ukazifanye mbele ya Farao zile ajabu zote nilizozitia mkononi mwako; lakini nitaufanya mgumu moyo wake, naye hatawapa ruhusa hao watu waende zao.
Romains 9.18 Exode 14.8 Exode 7.13 Exode 3.20 Exode 9.12
22 Nawe umwambie Farao, Bwana asema hivi, Israeli ni mwanangu mimi, mzaliwa wa kwanza wangu;
Osée 11.1 Jérémie 31.9 Romains 9.4 Esaïe 64.8 Jacques 1.18
23 nami nimekuambia, Mpe mwanangu ruhusa aende, ili apate kunitumikia, nawe umekataa kumpa ruhusa aende; angalia basi, mimi nitamwua mwanao, mzaliwa wa kwanza wako.
Exode 11.5 Exode 12.29 Psaumes 105.36 Psaumes 135.8 Psaumes 78.51
24 Ilikuwa walipokuwa njiani mahali pa kulala, Bwana akakutana naye akataka kumwua.
Genèse 17.14 1 Chroniques 21.16 Lévitique 10.3 Osée 13.8 Nombres 22.22-22.23
25 Ndipo Sipora akashika jiwe gumu na kuikata govi ya zunga la mwanawe, na kuibwaga miguuni pake akasema. Hakika wewe u bwana arusi wa damu kwangu mimi.
Josué 5.2-5.3 Genèse 17.14 2 Samuel 16.7
26 Basi akamwacha. Ndipo huyo mkewe akanena, U bwana arusi wa damu wewe, kwa ajili ya kutahiri.
27 Bwana akamwambia Haruni, Nenda jangwani uonane na Musa. Naye akaenda, akamkuta katika mlima wa Mungu, akambusu.
Exode 3.1 Actes 10.5-10.6 Exode 4.14-4.16 Actes 10.20 Ecclésiaste 4.9
28 Musa akamwambia Haruni hayo maneno yote ya Bwana ambayo alimtuma aende nayo, na ishara hizo zote alizomwagiza.
Exode 4.15-4.16 Exode 4.8-4.9 Matthieu 21.29 Jonas 3.2
29 Musa na Haruni wakaenda, wakawakusanya wazee wote wa watu wa Israeli.
Exode 3.16 Exode 24.1 Exode 24.11
30 Haruni akawaambia maneno yote Bwana aliyonena na Musa akazifanya zile ishara mbele ya watu.
Exode 4.16
31 Watu wakaamini, na waliposikia ya kuwa Bwana amewajilia wana wa Israeli, na ya kuwa ameyaona mateso yao, wakainama vichwa vyao wakasujudu.
Exode 3.18 Luc 8.13 Psaumes 106.12-106.13 1 Chroniques 29.20 Genèse 24.26

Cette Bible est dans le domaine public.