Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Exode 3.12
Bible en Swahili de l’est


1 Basi huyo Musa alikuwa akilichunga kundi la Yethro mkwewe, kuhani wa Midiani; akaliongoza kundi nyuma ya jangwa, akafika mpaka mlima wa Mungu, hata Horebu.
1 Rois 19.8 Nombres 10.29 Juges 4.11 Exode 17.6 Exode 19.3
2 Malaika wa Bwana akamtokea, katika mwali wa moto uliotoka katikati ya kijiti; akatazama, na kumbe! Kile kijiti kiliwaka moto, nacho kijiti hakikuteketea.
Actes 7.30-7.35 Deutéronome 33.16 Jean 1.14 Marc 12.26 Esaïe 63.9
3 Musa akasema, Nitageuka sasa, niyaone maono haya makubwa, na sababu kijiti hiki hakiteketei.
Actes 7.31 Psaumes 111.2-111.4 Job 37.14 Psaumes 107.8
4 Bwana alipoona ya kuwa amegeuka ili atazame, Mungu akamwita kutoka katikati ya kile kijiti, akasema, Musa! Musa! Akasema, Mimi hapa.
Deutéronome 33.16 1 Samuel 3.6 Actes 10.3 Actes 9.4 1 Samuel 3.8
5 Naye akasema, Usikaribie hapa; vua viatu vyako miguuni mwako; maana mahali hapo unaposimama ni nchi takatifu.
Josué 5.15 Actes 7.33 Exode 19.12 Ecclésiaste 5.1 Genèse 28.16-28.17
6 Tena akasema, Mimi ni Mungu wa baba yako, Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo. Musa akaficha uso wake; kwa maana aliogopa kumwangalia Mungu.
Luc 20.37 Exode 4.5 Matthieu 22.32 Marc 12.26 Actes 7.32
7 Bwana akasema, Hakika nimeyaona mateso ya watu wangu walioko Misri, nami nimekisikia kilio chao kwa sababu ya wasimamizi wao; maana nayajua maumivu yao;
Psaumes 106.44 Psaumes 145.19 Exode 2.23-2.25 Néhémie 9.9 Esaïe 63.9
8 nami nimeshuka ili niwaokoe na mikono ya Wamisri, niwapandishe kutoka nchi ile, hata nchi njema, kisha pana; nchi ijaayo maziwa na asali; hata mahali pa Mkanaani, na Mhiti, na Mwamori, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi.
Genèse 50.24 Exode 3.17 Genèse 15.18-15.21 Deutéronome 1.25 Ezéchiel 20.6
9 Basi, tazama, kilio cha wana wa Israeli kimenifikilia; tena nimeyaona hayo mateso ambayo Wamisri wanawatesa.
Exode 2.23 Exode 3.7 Exode 1.11 Exode 1.22 Exode 1.13-1.14
10 Haya, basi, nitakutuma sasa kwa Farao, ili upate kuwatoa watu wangu, hao wana wa Israeli, katika Misri.
Michée 6.4 Esaïe 63.11-63.12 Psaumes 105.26 Psaumes 77.20 Psaumes 103.6-103.7

Objections de Moïse

11 Musa akamwambia Mungu, Mimi ni nani, hata niende kwa Farao, nikawatoe wana wa Israeli watoke Misri?
1 Samuel 18.18 Exode 6.12 2 Corinthiens 3.5 Jérémie 1.6 Esaïe 6.5-6.8
12 Akasema, Bila shaka mimi nitakuwa pamoja nawe; na dalili ya kuwa nimekutuma ndiyo hii; utakapokuwa umekwisha kuwatoa hao watu katika Misri, mtamwabudu Mungu katika mlima huu.
Josué 1.5 Exode 4.15 Romains 8.31 Genèse 31.3 Exode 4.12
13 Musa akamwambia Mungu, Tazama, nitakapofika kwa wana wa Israeli, na kuwaambia, Mungu wa baba zenu amenituma kwenu; nao wakaniuliza, Jina lake n’nani? Niwaambie nini?
Esaïe 9.6 Exode 3.14 Esaïe 7.14 Proverbes 30.4 Jérémie 23.6
14 Mungu akamwambia Musa, MIMI NIKO AMBAYE NIKO;akasema,Ndivyo utakavyowaambia wana wa Israeli;MIMI NIKO amenituma kwenu.
Jean 8.58 Exode 6.3 Hébreux 13.8 Apocalypse 1.8 Apocalypse 4.8
15 Tena Mungu akamwambia Musa, Waambie wana wa Israeli maneno haya, Bwana, Mungu wa baba zenu, Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka, Mungu wa Yakobo, amenituma kwenu; hili ndilo jina langu hata milele, nalo ni kumbukumbu langu hata vizazi vyote.
Osée 12.5 Psaumes 135.13 Exode 3.6 Psaumes 102.12 Psaumes 72.17
16 Enenda, ukawakusanye wazee wa Israeli pamoja, ukawaambie, Bwana, Mungu wa baba zenu, Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka, Mungu wa Yakobo, amenitokea, akaniambia, Hakika nimewajilieni, tena nimeyaona mnayotendewa huko Misri;
Exode 4.29 Exode 4.31 Genèse 50.24 1 Pierre 5.1 1 Pierre 2.12
17 Nami nimesema, Nitawapandisha kutoka katika mateso ya Misri na kuwaingiza katika nchi ya Mkanaani, na Mhiti, na Mwamori, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi, nchi ijaayo maziwa na asali.
Genèse 15.13-15.21 Genèse 50.24 Genèse 46.4 Josué 24.11 Exode 2.23-2.25
18 Nao watakusikia sauti yako; nawe utakwenda, wewe na wazee wa Israeli kwa mfalme wa Misri, na kumwambia, Bwana Mungu wa Waebrania, amekutana nasi; basi sasa twakuomba, tupe ruhusa twende mwendo siku tatu jangwani, ili tumtolee dhabihu Bwana Mungu wetu.
Exode 9.1 Exode 7.16 Nombres 23.3-23.4 Nombres 23.15-23.16 Exode 29.42-29.43
19 Nami najua ya kuwa huyo mfalme wa Misri hatawapa ruhusa mwende zenu, la, hata kwa mkono wa nguvu.
Exode 5.2 Exode 6.1 Exode 7.1-7.14 Esaïe 63.12-63.13 Psaumes 136.11-136.12
20 Nami nitaunyosha mkono wangu, na kuipiga Misri kwa ajabu zangu zote, nitakazofanya kati yake, kisha baadaye atawapa ruhusa kwenda.
Néhémie 9.10 Exode 9.15 Actes 7.36 Deutéronome 6.22 Exode 11.8-11.9
21 Nami nitawapa watu hao kufadhiliwa mbele ya Wamisri; hata itakuwa, hapo mtakapokwenda zenu hamtakwenda kitupu;
Exode 12.36 Exode 11.3 Proverbes 16.7 Psaumes 106.46 Psaumes 105.37
22 Lakini kila mwanamke ataomba kwa jirani, na kwa huyo akaaye naye nyumbani, vyombo vya fedha, na vyombo vya dhahabu, na mavazi; nanyi mtawavika wana wenu na binti zenu; nanyi mtawateka nyara Wamisri.
Ezéchiel 39.10 Exode 11.2 Psaumes 105.37 Genèse 15.14 Proverbes 13.22

Cette Bible est dans le domaine public.