Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 88.17
Bible en Swahili de l’est


Lamentation dans le malheur

1 Ee Bwana, Mungu wa wokovu wangu Mchana na usiku nimelia mbele zako.
Luc 18.7 Psaumes 22.2 Psaumes 51.14 Psaumes 27.9 1 Chroniques 2.6
2 Maombi yangu yafike mbele zako, Uutegee ukelele wangu sikio lako.
Psaumes 79.11 1 Rois 8.31 Lamentations 3.8 Psaumes 31.2 Psaumes 141.1-141.2
3 Maana nafsi yangu imeshiba taabu, Na uhai wangu umekaribia kuzimu.
Psaumes 107.18 Psaumes 107.26 Job 33.22 Psaumes 22.11-22.21 Psaumes 88.14-88.15
4 Nimehesabiwa pamoja nao washukao shimoni; Nimekuwa kama mtu asiye na msaada.
Psaumes 28.1 Psaumes 143.7 Psaumes 109.22-109.24 Ezéchiel 26.20 Esaïe 38.17-38.18
5 Miongoni mwao waliokufa nimetupwa, Kama waliouawa walalao makaburini. Hao ambao Wewe huwakumbuki tena, Wametengwa mbali na mkono wako.
Esaïe 53.8 Psaumes 31.22 Job 11.10 Psaumes 31.12 Psaumes 136.23
6 Mimi umenilaza katika shimo la chini, Katika mahali penye giza vilindini.
Psaumes 69.15 Psaumes 143.3 Psaumes 86.13 Jude 1.13 Lamentations 3.55
7 Ghadhabu yako imenilemea, Umenitesa kwa mawimbi yako yote.
Psaumes 42.7 Romains 2.5-2.9 Psaumes 102.10 Jean 3.36 Psaumes 32.4
8 Wanijuao umewatenga nami; Umenifanya kuwa chukizo kwao; Nimefungwa wala siwezi kutoka.
Psaumes 31.11 Esaïe 49.7 Zacharie 11.8 Jérémie 32.2 Jean 11.57
9 Jicho langu limefifia kwa ajili ya mateso Bwana, nimekuita kila siku; Nimekunyoshea Wewe mikono yangu.
Job 11.13 Psaumes 143.6 Psaumes 86.3 Psaumes 38.10 Psaumes 88.1
10 Wafu je! Utawafanyia miujiza? Au waliofariki watasimama na kukuhimidi?
Psaumes 6.5 Psaumes 30.9 Esaïe 26.19 Marc 5.35-5.36 Job 14.7-14.12
11 Fadhili zako zitasimuliwa kaburini? Au uaminifu wako katika uharibifu?
Matthieu 7.13 Proverbes 15.11 2 Pierre 2.1 Job 26.6 Romains 9.22
12 Miujiza yako itajulikana gizani? Au haki yako katika nchi ya usahaulifu?
Ecclésiaste 9.5 Jude 1.13 Job 10.21-10.22 Matthieu 8.12 Psaumes 31.12
13 Lakini mimi nimekulilia Wewe, Bwana, Na asubuhi maombi yangu yatakuwasilia.
Psaumes 5.3 Psaumes 30.2 Marc 1.35 Psaumes 119.147-119.148
14 Bwana, kwa nini kuitupa nafsi yangu, Na kunificha uso wako?
Job 13.24 Psaumes 13.1 Psaumes 43.2 Psaumes 44.24 Matthieu 27.46
15 Nateswa mimi hali ya kufa tangu ujana, Nimevumilia vitisho vyako na kufadhaika.
Job 6.4 Esaïe 53.3 Zacharie 13.7 Psaumes 22.14-22.15 Psaumes 73.14
16 Hasira zako kali zimepita juu yangu, Maogofyo yako yameniangamiza.
Esaïe 53.8 Psaumes 89.46 Psaumes 102.10 Psaumes 90.7 Romains 8.32
17 Yamenizunguka kama maji mchana kutwa, Yamenisonga yote pamoja.
Psaumes 22.16 Psaumes 42.7 Job 30.14-30.15 Job 16.12-16.13 Psaumes 124.4
18 Mpenzi na rafiki umewatenga nami, Nao wanijuao wamo gizani.
Psaumes 38.11 Psaumes 88.8 Psaumes 31.11 Job 19.12-19.15

Cette Bible est dans le domaine public.