Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 88.16
Bible en Swahili de l’est


Lamentation dans le malheur

1 Ee Bwana, Mungu wa wokovu wangu Mchana na usiku nimelia mbele zako.
Luc 18.7 Psaumes 22.2 Psaumes 27.9 Psaumes 51.14 1 Chroniques 2.6
2 Maombi yangu yafike mbele zako, Uutegee ukelele wangu sikio lako.
Lamentations 3.8 Psaumes 31.2 Psaumes 141.1-141.2 Psaumes 79.11 1 Rois 8.31
3 Maana nafsi yangu imeshiba taabu, Na uhai wangu umekaribia kuzimu.
Psaumes 107.18 Psaumes 22.11-22.21 Psaumes 88.14-88.15 Psaumes 143.3-143.4 Matthieu 26.37-26.39
4 Nimehesabiwa pamoja nao washukao shimoni; Nimekuwa kama mtu asiye na msaada.
Psaumes 28.1 Psaumes 143.7 Esaïe 38.17-38.18 2 Corinthiens 13.4 Jonas 2.6
5 Miongoni mwao waliokufa nimetupwa, Kama waliouawa walalao makaburini. Hao ambao Wewe huwakumbuki tena, Wametengwa mbali na mkono wako.
Esaïe 53.8 Psaumes 31.22 Psaumes 136.23 Esaïe 14.9-14.12 Esaïe 38.10-38.12
6 Mimi umenilaza katika shimo la chini, Katika mahali penye giza vilindini.
Psaumes 69.15 Psaumes 143.3 Psaumes 86.13 Jean 12.46 Psaumes 40.2
7 Ghadhabu yako imenilemea, Umenitesa kwa mawimbi yako yote.
Psaumes 42.7 Psaumes 102.10 Jean 3.36 Psaumes 32.4 Jonas 2.3
8 Wanijuao umewatenga nami; Umenifanya kuwa chukizo kwao; Nimefungwa wala siwezi kutoka.
Psaumes 31.11 Esaïe 49.7 Zacharie 11.8 Jérémie 32.2 Psaumes 88.18
9 Jicho langu limefifia kwa ajili ya mateso Bwana, nimekuita kila siku; Nimekunyoshea Wewe mikono yangu.
Job 11.13 Psaumes 143.6 Psaumes 86.3 Psaumes 38.10 Psaumes 6.7
10 Wafu je! Utawafanyia miujiza? Au waliofariki watasimama na kukuhimidi?
Psaumes 6.5 Psaumes 30.9 Job 14.7-14.12 Psaumes 118.17 Esaïe 38.18-38.19
11 Fadhili zako zitasimuliwa kaburini? Au uaminifu wako katika uharibifu?
2 Pierre 2.1 Job 26.6 Romains 9.22 Job 21.30 Psaumes 55.23
12 Miujiza yako itajulikana gizani? Au haki yako katika nchi ya usahaulifu?
Ecclésiaste 9.5 Matthieu 8.12 Psaumes 31.12 Ecclésiaste 8.10 Esaïe 8.22
13 Lakini mimi nimekulilia Wewe, Bwana, Na asubuhi maombi yangu yatakuwasilia.
Psaumes 5.3 Psaumes 30.2 Psaumes 119.147-119.148 Marc 1.35
14 Bwana, kwa nini kuitupa nafsi yangu, Na kunificha uso wako?
Job 13.24 Psaumes 13.1 Psaumes 43.2 Psaumes 44.24 Psaumes 44.9
15 Nateswa mimi hali ya kufa tangu ujana, Nimevumilia vitisho vyako na kufadhaika.
Job 6.4 Psaumes 22.14-22.15 Psaumes 73.14 Job 7.11-7.16 Job 17.1
16 Hasira zako kali zimepita juu yangu, Maogofyo yako yameniangamiza.
Psaumes 102.10 Psaumes 90.7 Romains 8.32 Psaumes 38.1-38.2 Galates 3.13
17 Yamenizunguka kama maji mchana kutwa, Yamenisonga yote pamoja.
Psaumes 22.16 Job 16.12-16.13 Psaumes 124.4 Matthieu 27.39-27.44 Lamentations 3.5-3.7
18 Mpenzi na rafiki umewatenga nami, Nao wanijuao wamo gizani.
Psaumes 38.11 Psaumes 88.8 Psaumes 31.11 Job 19.12-19.15

Cette Bible est dans le domaine public.