Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 88.13
Bible en Swahili de l’est


Lamentation dans le malheur

1 Ee Bwana, Mungu wa wokovu wangu Mchana na usiku nimelia mbele zako.
Psaumes 22.2 Luc 18.7 Psaumes 27.9 Psaumes 51.14 Esaïe 12.2
2 Maombi yangu yafike mbele zako, Uutegee ukelele wangu sikio lako.
Psaumes 31.2 Psaumes 141.1-141.2 Psaumes 79.11 1 Rois 8.31 Lamentations 3.8
3 Maana nafsi yangu imeshiba taabu, Na uhai wangu umekaribia kuzimu.
Psaumes 107.18 Esaïe 53.3 Psaumes 69.17-69.21 Esaïe 53.10-53.11 Lamentations 3.15-3.19
4 Nimehesabiwa pamoja nao washukao shimoni; Nimekuwa kama mtu asiye na msaada.
Psaumes 28.1 Psaumes 143.7 Job 17.1 Romains 5.6 Psaumes 31.12
5 Miongoni mwao waliokufa nimetupwa, Kama waliouawa walalao makaburini. Hao ambao Wewe huwakumbuki tena, Wametengwa mbali na mkono wako.
Esaïe 53.8 Psaumes 31.22 Genèse 19.29 Job 6.9 Ezéchiel 32.18-32.32
6 Mimi umenilaza katika shimo la chini, Katika mahali penye giza vilindini.
Psaumes 69.15 Psaumes 143.3 Psaumes 86.13 Proverbes 4.19 Psaumes 130.1
7 Ghadhabu yako imenilemea, Umenitesa kwa mawimbi yako yote.
Psaumes 42.7 Apocalypse 6.16-6.17 1 Pierre 2.24 Job 6.4 Psaumes 38.1
8 Wanijuao umewatenga nami; Umenifanya kuwa chukizo kwao; Nimefungwa wala siwezi kutoka.
Psaumes 31.11 Zacharie 11.8 Jérémie 32.2 Esaïe 49.7 Jean 15.23-15.24
9 Jicho langu limefifia kwa ajili ya mateso Bwana, nimekuita kila siku; Nimekunyoshea Wewe mikono yangu.
Job 11.13 Psaumes 143.6 Psaumes 86.3 Psaumes 38.10 Job 17.7
10 Wafu je! Utawafanyia miujiza? Au waliofariki watasimama na kukuhimidi?
Psaumes 6.5 Psaumes 30.9 Luc 7.12-7.16 Psaumes 115.17 1 Corinthiens 15.52-15.57
11 Fadhili zako zitasimuliwa kaburini? Au uaminifu wako katika uharibifu?
Psaumes 55.23 Psaumes 73.18 Matthieu 7.13 Proverbes 15.11 2 Pierre 2.1
12 Miujiza yako itajulikana gizani? Au haki yako katika nchi ya usahaulifu?
Ecclésiaste 9.5 Psaumes 143.3 Ecclésiaste 2.16 Jude 1.13 Job 10.21-10.22
13 Lakini mimi nimekulilia Wewe, Bwana, Na asubuhi maombi yangu yatakuwasilia.
Psaumes 5.3 Psaumes 30.2 Psaumes 119.147-119.148 Marc 1.35
14 Bwana, kwa nini kuitupa nafsi yangu, Na kunificha uso wako?
Job 13.24 Psaumes 13.1 Psaumes 43.2 Psaumes 44.24 Psaumes 69.17
15 Nateswa mimi hali ya kufa tangu ujana, Nimevumilia vitisho vyako na kufadhaika.
Job 6.4 Luc 22.44 Esaïe 53.10 Job 17.11-17.16 Esaïe 53.3
16 Hasira zako kali zimepita juu yangu, Maogofyo yako yameniangamiza.
Apocalypse 6.17 Esaïe 53.4-53.6 Daniel 9.26 Psaumes 90.11 Esaïe 53.8
17 Yamenizunguka kama maji mchana kutwa, Yamenisonga yote pamoja.
Psaumes 22.16 Psaumes 69.1-69.2 Psaumes 118.10-118.12 Psaumes 42.7 Job 30.14-30.15
18 Mpenzi na rafiki umewatenga nami, Nao wanijuao wamo gizani.
Psaumes 38.11 Psaumes 88.8 Psaumes 31.11 Job 19.12-19.15

Cette Bible est dans le domaine public.