Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 84.6
Bible en Swahili de l’est


Bénédiction dans la maison de Dieu

1 Maskani zako zapendeza kama nini, Ee Bwana wa majeshi!
Psaumes 27.4 Psaumes 43.3 Psaumes 132.5 Psaumes 8.1 1 Rois 22.19
2 Nafsi yangu imezionea shauku nyua za Bwana, Naam, na kuzikondea. Moyo wangu na mwili wangu Vinamlilia Mungu aliye hai.
Psaumes 42.1-42.2 Psaumes 73.26 Psaumes 143.6 Esaïe 26.9 Psaumes 63.1-63.2
3 Shomoro naye ameona nyumba, Na mbayuwayu amejipatia kioto, Alipoweka makinda yake, Kwenye madhabahu zako, Ee Bwana wa majeshi, Mfalme wangu na Mungu wangu.
Psaumes 5.2 Psaumes 90.1 Matthieu 23.37 Psaumes 116.7 Psaumes 91.1
4 Heri wakaao nyumbani mwako, Wanakuhimidi daima.
Psaumes 65.4 Psaumes 27.4 Psaumes 145.1-145.2 Psaumes 42.11 Psaumes 23.6
5 Heri ambaye nguvu zake zatoka kwako, Na njia ziendazo Sayuni zimo moyoni mwake.
Zacharie 10.12 Esaïe 26.9 Psaumes 122.1 Jérémie 31.33 Philippiens 4.13
6 Wakipita kati ya bonde la Vilio, Hulifanya kuwa chemchemi, Naam, mvua ya vuli hulivika baraka
Psaumes 68.9 Romains 5.3-5.5 Joël 2.23 2 Corinthiens 4.17 2 Rois 3.9-3.20
7 Huendelea toka nguvu hata nguvu, Huonekana Sayuni kila mmoja mbele za Mungu.
2 Corinthiens 3.18 Proverbes 4.18 Esaïe 40.31 Deutéronome 16.16 2 Pierre 3.18
8 Bwana, Mungu wa majeshi, uyasikie maombi yangu, Ee Mungu wa Yakobo, usikilize,
Psaumes 59.5
9 Ee Mungu, ngao yetu, uangalie, Umtazame uso masihi wako.
Psaumes 2.2 Genèse 15.1 Actes 4.27 Psaumes 2.6 1 Samuel 16.6
10 Hakika siku moja katika nyua zako Ni bora kuliko siku elfu. Ningependa kuwa bawabu nyumbani mwa Mungu wangu, Kuliko kukaa katika hema za uovu.
Psaumes 27.4 Psaumes 63.2 Psaumes 26.8-26.10 Psaumes 141.4-141.5 Philippiens 3.20
11 Kwa kuwa Bwana, Mungu, ni jua na ngao, Bwana atatoa neema na utukufu. Hatawanyima kitu chema Hao waendao kwa ukamilifu.
Proverbes 2.7 Psaumes 34.9-34.10 Matthieu 6.33 Psaumes 85.12 Philippiens 4.19
12 Ee Bwana wa majeshi, Heri mwanadamu anayekutumaini Wewe.
Psaumes 62.8 Psaumes 2.12 Esaïe 30.18 Psaumes 34.8 Jérémie 17.7-17.8

Cette Bible est dans le domaine public.