Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 5.20
Bible en Swahili de l’est


1 Haya, ita sasa; je! Yuko atakayekujibu? Nawe utamwelekea yupi katika hao watakatifu?
Job 15.15 Esaïe 41.1 Job 4.18 Hébreux 12.1 Psaumes 16.3
2 Kwani hasira humwua mtu mpumbavu, Nao wivu humwua mjinga.
Proverbes 12.16 Jonas 4.9 Job 18.4 Proverbes 8.5 Psaumes 92.6
3 Nimewaona wapumbavu wakishusha mizizi; Lakini mara niliyalaani maskani yake.
Psaumes 73.18-73.20 Psaumes 37.35-37.36 Jérémie 12.1-12.3 Actes 1.20 Deutéronome 27.15-27.26
4 Watoto wake wako mbali na wokovu, Nao wamesongwa langoni, Wala hapana atakayewaponya.
Psaumes 127.5 Psaumes 119.155 Exode 20.5 Job 10.7 Job 1.19
5 Mavuno yake wale wenye njaa huyala, Na kuyatwaa hata kuyatoa miibani, Nao wenye kiu huzitwetea mali zao.
Deutéronome 28.51 2 Chroniques 33.11 Job 12.6 Deutéronome 28.33 Lamentations 2.16
6 Kwani taabu haitoki mchangani, Wala mashaka hayachipuki katika nchi;
Job 34.29 Hébreux 12.15 1 Samuel 6.9 Osée 10.4 Amos 3.6
7 Lakini mwanadamu huzaliwa ili apate mashaka, Kama cheche za moto zirukavyo juu.
Job 14.1 Genèse 3.17-3.19 1 Corinthiens 10.13 Ecclésiaste 1.8 Psaumes 90.8-90.9
8 Lakini mimi ningemtafuta Mungu, Ningemwekea Mungu daawa yangu;
Psaumes 50.15 Psaumes 37.5 1 Pierre 4.19 1 Pierre 2.23 Psaumes 77.1-77.2
9 Yeye afanyaye mambo makuu, yasiyotambulikana; Mambo ya ajabu yasiyo na hesabu;
Job 9.10 Psaumes 40.5 Psaumes 72.18 Romains 11.33 Esaïe 40.28
10 Yeye atoaye mvua inyeshe juu ya nchi, Na kuyapeleka maji mashambani;
Jérémie 5.24 Jérémie 14.22 Actes 14.17 Psaumes 147.8 Jérémie 10.13
11 Awainuaye juu hao walio chini; Na hao waombolezao hukuzwa wawe salama.
Luc 1.52-1.53 1 Samuel 2.7-2.8 1 Pierre 5.10 Psaumes 91.14 Jacques 1.9
12 Yeye huyatangua mashauri ya wadanganyifu, Mikono yao isipate kuyatimiza makusudi yao.
Esaïe 8.10 Néhémie 4.15 Psaumes 33.10-33.11 Psaumes 21.11 Proverbes 21.30
13 Yeye huwanasa wenye hekima katika hila yao wenyewe; Na mashauri ya washupavu yaharibika kwa haraka.
Psaumes 9.15-9.16 1 Corinthiens 1.19-1.20 Luc 1.51 1 Corinthiens 3.19 2 Samuel 15.34
14 Wao hupatwa na giza wakati wa mchana, Hupapasa mchana vilevile kama usiku.
Job 12.25 Deutéronome 28.29 Esaïe 59.10 Proverbes 4.19 Amos 8.9
15 Lakini yeye huokoa na upanga wa kinywa chao, Hata kumwokoa mhitaji na mkono wake aliye hodari.
Psaumes 35.10 Psaumes 10.14 Psaumes 109.31 Psaumes 140.12 Job 4.10
16 Basi hivi huyo maskini ana matumaini, Na uovu hufumba kinywa chake.
Psaumes 107.42 1 Samuel 2.8-2.9 Psaumes 63.11 Exode 11.7 Esaïe 14.32
17 Tazama, yu heri mtu yule Mungu amwadhibuye; Kwa hiyo usidharau kurudiwa na huyo Mwenyezi.
Psaumes 94.12 Hébreux 12.5-12.11 Jacques 1.12 Jérémie 31.18 Apocalypse 3.19
18 Kwani yeye huumiza, lakini tena huuguza; Yeye hutia jeraha, na mikono yake huponya.
Osée 6.1 Deutéronome 32.39 1 Samuel 2.6 Esaïe 30.26 Psaumes 147.3
19 Yeye atakuokoa na mateso sita; Naam, hata katika saba hapana uovu utakaokugusa.
Psaumes 34.19 1 Corinthiens 10.13 Proverbes 24.16 2 Pierre 2.9 Psaumes 91.3-91.10
20 Wakati wa njaa atakukomboa na mauti; Na vitani atakukomboa na nguvu za upanga.
Psaumes 33.19 Psaumes 49.7 Genèse 45.7 1 Rois 17.6 Matthieu 24.6
21 Utafichwa na mapigo ya ulimi; Wala usiogope maangamizo yatakapokuja.
Psaumes 31.20 Jacques 3.5-3.8 Proverbes 12.18 Psaumes 91.5-91.7 Jérémie 18.18
22 Wewe utayacheka maangamizo na njaa; Wala hutawaogopa wanyama wakali wa nchi.
Ezéchiel 34.25 Esaïe 35.9 Esaïe 65.25 Psaumes 91.13 2 Rois 19.21
23 Kwani utakuwa na mapatano na mawe ya bara; Nao wanyama wa bara watakuwa na amani kwako.
Psaumes 91.12-91.13 Lévitique 26.6 Ezéchiel 14.15-14.16 Romains 8.38-8.39 Daniel 6.22
24 Nawe utajua ya kwamba hema yako ina salama; Na zizi lako utaliaua, wala usikose kitu.
Psaumes 91.10 Psaumes 121.7-121.8 Job 18.6 Job 18.21 Job 8.6
25 Tena utajua ya kwamba uzao wako utakuwa mwingi, Na vizazi vyako watakuwa kama nyasi za nchi.
Psaumes 112.2 Psaumes 72.16 Psaumes 127.3-127.5 Genèse 15.5 Psaumes 128.3-128.6
26 Utafika kaburini mwenye umri mtimilifu, Kama mganda wa ngano ulivyo wakati wake.
Genèse 15.15 Proverbes 9.11 Proverbes 10.27 Genèse 25.8 Job 42.16-42.17
27 Tazama, haya tumeyapeleleza, ndivyo yalivyo; Yasikie, uyajue, ili upate mema.
Psaumes 111.2 Job 8.8-8.10 Proverbes 2.3-2.5 Job 15.17 Job 12.2

Cette Bible est dans le domaine public.