Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 22.9
Bible en Swahili de l’est


Intervention n° 3 d’Éliphaz

1 Ndipo huyo Elifazi Mtemani akajibu, na kusema,
2 Je! Yumkini mtu awaye yote kumfaa Mungu? Hakika yeye aliye na hekima hujifaa mwenyewe.
Luc 17.10 Deutéronome 10.13 Galates 6.7-6.8 Proverbes 9.12 Proverbes 4.7-4.9
3 Je! Mwenyezi hupata furaha katika wewe kuwa mwenye haki? Au je, ni faida kwake, kwamba wafanya njia zako kuwa timilifu?
Psaumes 119.59 Psaumes 119.3-119.6 Proverbes 12.22 Job 23.10-23.12 Psaumes 147.10-147.11
4 Je! Ni kwa wewe kumcha yeye anakukemea? Na kuingia hukumuni nawe?
Job 14.3 Psaumes 143.2 Job 9.19 Esaïe 3.14-3.15 Job 23.6-23.7
5 Je! Uovu wako si mkuu? Wala maovu yako hayana mwisho.
Job 21.27 Job 15.5-15.6 Psaumes 40.12 Job 32.3 Psaumes 19.12
6 Kwa kuwa umetwaa dhamana kwa nduguyo bure, Na kuwavua nguo zao walio uchi.
Exode 22.26 Ezéchiel 18.12 Ezéchiel 18.16 Job 24.3 Job 31.19-31.20
7 Hukumpa maji ya kunywa huyo aliyechoka, Nawe umemnyima chakula huyo mwenye njaa.
Job 31.17 Matthieu 25.42 Esaïe 58.7 Ezéchiel 18.7 Ezéchiel 18.16
8 Lakini huyo shujaa, nchi ilikuwa yake; Na huyo mwenye kusifiwa, yeye aliikaa.
Esaïe 9.15 Job 31.34 1 Rois 21.11-21.15 Michée 7.3 Esaïe 3.3
9 Umewafukuza wanawake wajane hali ya utupu, Na mikono ya mayatima imevunjwa.
Job 24.21 Job 24.3 Job 31.21 Ezéchiel 22.7 Esaïe 10.2
10 Kwa hiyo umezungukwa na mitego, Na hofu ya ghafula yakutaabisha,
Job 18.8-18.10 Job 6.4 Job 13.21 Proverbes 1.27 Proverbes 3.25-3.26
11 Au je! Huoni giza, Na maji mengi yanayokufunika?
Lamentations 3.54 Psaumes 69.1-69.2 Jonas 2.3 Job 19.8 Psaumes 124.4-124.5
12 Je! Mungu hayuko mbinguni juu? Tena tazama umbali wa nyota, jinsi zilivyo juu!
Ecclésiaste 5.2 Job 11.8 Esaïe 66.1 Psaumes 8.3-8.4 Esaïe 57.15
13 Nawe wasema, Mungu anajua nini? Je! Aweza kuamua kati ya giza kuu?
Psaumes 10.11 Ezéchiel 8.12 Psaumes 73.11 Psaumes 59.7 Ezéchiel 9.9
14 Mawingu mazito ni kifuniko chake, hata asione; Naye yuatembea juu ya kuba ya mbingu.
Psaumes 139.11-139.12 Luc 12.2-12.3 Psaumes 33.14 Jérémie 23.24 Job 26.9
15 Je! Utaiandama njia ya zamani Waliyoikanyaga watu waovu?
Genèse 6.11-6.13 Luc 17.26-17.27 Genèse 6.5
16 Ambao walinyakuliwa kabla ya wakati wao, Msingi wao ulimwagika kama kijito cha maji;
Job 15.32 Matthieu 24.37-24.39 Genèse 7.17-7.24 1 Pierre 3.19-3.20 2 Pierre 2.5
17 Waliomwambia Mungu, Tuondokee; Tena, Huyo Mwenyezi aweza kutufanyia nini?
Job 21.14-21.15 Psaumes 4.6 Matthieu 8.29 Malachie 3.14 Esaïe 30.11
18 Naye ndiye aliyezijaza nyumba zao vitu vyema; Lakini mashauri ya waovu na yawe mbali nami.
Job 21.16 Job 12.6 1 Samuel 2.7 Psaumes 17.14 Jérémie 12.2
19 Wenye haki huyaona hayo wakafurahi; Nao wasio na hatia huwacheka;
Psaumes 58.10 Psaumes 107.42 Psaumes 52.6 Job 9.23 Proverbes 11.10
20 Wasema, Hakika hao waliotuinukia wamekatiliwa mbali, Na mabaki yao moto umeyateketeza.
2 Pierre 2.6-2.7 Job 1.16 Job 15.5-15.6 Job 21.27-21.28 Job 8.3-8.4
21 Mjue sana Mungu, ili uwe na amani; Ndivyo mema yatakavyokujia.
Philippiens 4.7 1 Chroniques 28.9 Esaïe 27.5 2 Corinthiens 5.20 Psaumes 34.10
22 Uyapokee, tafadhali, mafunzo yatokayo kinywani mwake, Na maneno yake yaweke moyoni mwako.
Job 23.12 Deutéronome 4.1-4.2 Psaumes 119.11 Deutéronome 6.6-6.9 Jérémie 15.16
23 Ukimrudia Mwenyezi, utajengwa; Ukiuondoa udhalimu mbali na hema yako.
Zacharie 1.3 Job 11.13-11.14 Job 8.5-8.6 Esaïe 55.6-55.7 Josué 7.13-7.16
24 Nawe hazina zako ziweke mchangani, Na dhahabu ya Ofiri iweke kati ya mawe ya vijito;
Esaïe 13.12 1 Rois 9.28 1 Rois 22.48 1 Rois 10.21 Psaumes 45.9
25 Naye Mwenyezi atakuwa hazina yako, Atakuwa ni fedha ya thamani kwako.
Jacques 2.5 Esaïe 33.6 Psaumes 18.2 Esaïe 41.10 Genèse 15.1
26 Kwani ndipo utakapojifurahisha katika Mwenyezi, Na kuinua uso wako kumwelekea Mungu.
Esaïe 58.14 Job 27.10 Psaumes 37.4 Job 11.15 Psaumes 86.4
27 Utamwomba yeye naye atakusikia; Nawe utazitimiliza nadhiri zako.
Esaïe 58.9 1 Jean 5.14-5.15 Psaumes 50.14-50.15 Psaumes 66.13-66.14 Psaumes 66.17-66.20
28 Nawe utakusudia neno, nalo litathibitika kwako; Na mwanga utaziangazia njia zako.
Matthieu 21.22 Psaumes 20.4 Jean 8.12 Psaumes 112.4 Psaumes 90.17
29 Hapo watakapokuangusha, utasema, Kuna kuinuka tena; Naye mnyenyekevu Mungu atamwokoa.
1 Pierre 5.5 Jacques 4.6 Matthieu 23.12 Luc 1.52 Proverbes 29.23
30 Atamwokoa na huyo asiye na hatia; Naam, utaokolewa kwa sababu ya usafi wa mikono yako.
Job 42.7-42.8 Genèse 18.26-18.32 Psaumes 18.20 Jacques 5.15-5.16 Actes 19.15-19.16

Cette Bible est dans le domaine public.