Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Chroniques 5.7
Bible en Swahili de l’est


Transport de l’arche

1 Hivyo ikaisha kazi yote Sulemani aliyoifanyia nyumba ya Bwana. Sulemani akaviingiza vitu alivyovitakasa baba yake Daudi; fedha, na dhahabu, na vyombo vyote, akavitia ndani ya hazina za nyumba ya Mungu.
1 Rois 7.51 1 Chroniques 26.26-26.28 2 Samuel 8.11 1 Chroniques 22.14
2 Ndipo Sulemani alipowakusanya wazee wa Israeli, na wakuu wote wa kabila, wakuu wa mbari za mababa wa wana wa Israeli, huko Yerusalemu, ili walipandishe sanduku la agano la Bwana kutoka mji wa Daudi, yaani, Sayuni.
2 Samuel 6.12 2 Chroniques 1.4 2 Chroniques 5.12 2 Samuel 5.7 Nombres 10.33
3 Wakakutana watu wote wa Israeli mbele ya mfalme wakati wa sikukuu, katika mwezi wa saba.
1 Rois 8.2 2 Chroniques 7.8-7.10 Lévitique 23.34-23.36
4 Wakaja wazee wote wa Israeli, nao Walawi wakajitwika sanduku.
Josué 3.6 1 Rois 8.3 1 Chroniques 15.12-15.14 2 Chroniques 5.7 1 Chroniques 15.2
5 Wakalipandisha sanduku, na ile hema ya kukutania, na vyombo vitakatifu vyote vilivyokuwamo Hemani, vitu hivyo makuhani Walawi wakavipandisha.
2 Chroniques 1.3 1 Rois 8.4 1 Rois 8.6
6 Mfalme Sulemani, na mkutano wote wa Israeli, waliokutanika kwake, walikuwako mbele ya sanduku, wakichinja dhabihu za kondoo na ng’ombe, wasiohesabika wala kujumlishwa kwa kuwa wengi.
1 Chroniques 29.21 1 Chroniques 16.1-16.2 2 Samuel 6.13 1 Rois 8.5
7 Makuhani wakaliingiza sanduku la agano la Bwana mahali pake katika chumba cha ndani cha nyumba, patakatifu pa patakatifu, yaani, chini ya mabawa ya makerubi.
1 Rois 8.6-8.7 Hébreux 9.4-9.5 Exode 37.6-37.9 1 Rois 6.23-6.28 Psaumes 132.8
8 Kwa maana makerubi yalinyosha mabawa yao juu ya mahali pa sanduku, makerubi yakalifunika lile sanduku na miti yake kwa juu.
Exode 25.12-25.15 Nombres 4.6 Exode 37.3-37.5
9 Na ile miti ilikuwa mirefu, hata ncha za miti zilionekana sandukuni mbele ya chumba cha ndani, lakini hazikuonekana nje; nayo iko kuko huko hata leo.
1 Rois 8.8-8.9
10 Hamkuwa na kitu ndani ya sanduku, ila zile mbao mbili alizozitia Musa huko Horebu, Bwana alipofanya agano na wana wa Israeli, hapo walipotoka Misri.
Hébreux 9.4 Deutéronome 10.2-10.5 2 Chroniques 6.11 Deutéronome 29.1 Deutéronome 29.10-29.14
11 Ikawa makuhani walipokwisha kutoka katika patakatifu; (kwani makuhani wote waliokuwapo, walikuwa wamejitakasa, wala hawakuzishika zamu zao;
Exode 19.14-19.15 2 Chroniques 35.4 2 Chroniques 29.5 2 Chroniques 29.34 1 Chroniques 24.1-24.31
12 tena Walawi waimbaji, wote pia, yaani Asafu, na Hemani, na Yeduthuni, na wana wao, na ndugu zao, hali wamevaa kitani safi, wenye matoazi na vinanda na vinubi, wamesimama upande wa mashariki wa madhabahu, na pamoja nao makuhani mia na ishirini wakipiga panda;)
1 Chroniques 15.24 1 Chroniques 6.33 Psaumes 68.25 2 Chroniques 29.25 1 Chroniques 23.5
13 hata ikawa, wenye panda na waimbaji walipokuwa kama mmoja, wakisikizisha sauti moja ya kumsifu na kumshukuru Bwana nao wakipaza sauti pamoja na panda na matoazi na vinanda, wakimsifu Bwana, wakisema, Kwa kuwa ni mwema; kwa maana fadhili zake ni za milele; ndipo nyumba ikajawa na wingu, naam, nyumba ya Bwana,
2 Chroniques 7.3 Jérémie 33.11 Esdras 3.11 2 Chroniques 20.21 Jérémie 32.39
14 hata makuhani hawakuweza kusimama ili kufanya huduma yao, kwa sababu ya lile wingu; kwa kuwa nyumba ya Mungu imejaa utukufu wa Bwana.
Exode 40.35 2 Chroniques 7.2 Apocalypse 15.8 Ezéchiel 10.4 1 Rois 8.11

Cette Bible est dans le domaine public.