Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Chroniques 22
Bible en Swahili de l’est


Règne d’Achazia

1 Nao wenyeji wa Yerusalemu walimfanya Ahazia mwanawe mdogo awe mfalme mahali pake; maana wakubwa wote wamekwisha kuuawa na kikosi cha watu waliokuja matuoni pamoja na Waarabu. Hivyo akatawala Ahazia mwana wa Yehoramu mfalme wa Yuda.
2 Chroniques 21.16-21.17 2 Rois 8.24-8.29 2 Chroniques 36.1 2 Chroniques 26.1 2 Chroniques 33.25
2 Ahazia alikuwa na umri wa miaka arobaini na miwili alipoanza kutawala; akatawala mwaka mmoja huko Yerusalemu; na jina la mamaye aliitwa Athalia binti Omri.
2 Rois 8.26 2 Chroniques 21.6 1 Rois 16.28
3 Yeye naye akaziendea njia za nyumba ya Ahabu; kwa kuwa mamaye alikuwa mshauri wake katika kufanya maovu.
Deutéronome 13.6-13.10 Genèse 27.12-27.13 Malachie 2.15 Genèse 6.4-6.5 Juges 17.4-17.5
4 Akafanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana kama nyumba ya Ahabu; kwa kuwa hao walikuwa washauri wake, alipokwisha kufa babaye, hata aangamie.
Proverbes 13.20 Proverbes 1.10 2 Chroniques 24.17-24.18 Proverbes 19.27 Proverbes 12.5
5 Naye akaenda kwa mashauri yao, akafuatana na Yoramu mwana wa Ahabu mfalme wa Israeli ili kupigana na Hazaeli mfalme wa Shamu huko Ramoth-Gileadi;nao Washami wakamjeruhi Yoramu.
Psaumes 1.1 2 Rois 8.9 Daniel 5.22 Michée 6.16 2 Chroniques 19.2
6 Akarudi Yezreeli ili aponye jeraha walizomjeruhi huko Rama, alipopigana na Hazaeli mfalme wa Shamu. Naye Ahazia mwana wa Yehoramu mfalme wa Yuda ,akashuka amtazame Yoramu mwana wa Ahabu,katika Yezreeli,kwa sababu alikuwa hawezi.
2 Rois 9.15 2 Chroniques 22.1 2 Rois 8.29 2 Chroniques 21.17 2 Rois 10.13-10.14
7 Basi kuangamia kwake Ahazia kulitokana na Mungu, kwa vile alivyomwendea Yoramu; kwa kuwa alipofika, akatoka pamoja na Yoramu juu ya Yehu mwana wa Nimshi, ambaye Bwana alimtia mafuta ili awakatilie mbali nyumba ya Ahabu.
2 Rois 9.21 2 Chroniques 10.15 Osée 14.9 1 Rois 19.16 Malachie 4.3
8 Ikawa, Yehu alipokuwa akiwafanyia hukumu nyumba ya Ahabu, aliwakuta wakuu wa Yuda, na wana wa nduguze Ahazia, wakimtumikia Ahazia, akawaua.
2 Rois 10.10-10.14
9 Akamtafuta Ahazia, wakamkamata, (naye alikuwa amejificha Samaria,) wakamleta kwa Yehu, wakamwua; wakamzika, kwa maana wakasema, Huyu ni mwana wa Yehoshafati, huyo aliyemtafuta Bwana kwa moyo wake wote. Wala nyumba ya Ahazia hawakuwa na uwezo wa kuushika ufalme.
2 Chroniques 21.20-22.1 1 Rois 14.13 1 Rois 13.21 2 Chroniques 21.17 2 Chroniques 21.4

Règne d’Athalie

10 Basi Athalia, mama wa Ahazia, alipoona ya kuwa mwanawe amekufa, akainuka, akawaangamiza wazao wote wa kifalme wa nyumba ya Yuda.
2 Rois 11.1-11.3 2 Chroniques 22.2-22.4
11 Ila Yehosheba, binti mfalme, akamtwaa Yoashi, mwana wa Ahazia, akamwiba miongoni mwa wana wa mfalme waliouawa, akamweka yeye na yaya wake katika chumba cha kulala. Basi Yehosheba, binti mfalme Yehoramu, mkewe Yehoyada kuhani, (naye alikuwa umbu lake Ahazia,) akaficha usoni pa Athalia, asimwue.
2 Rois 11.2 1 Rois 15.4 Esaïe 65.8 Psaumes 76.10 2 Chroniques 21.7
12 Akawako pamoja nao, amefichwa nyumbani mwa Mungu, miaka sita. Na Athalia akaitawala nchi.
Psaumes 12.8 Jérémie 12.1 Habakuk 1.12 Psaumes 27.5 Psaumes 73.18-73.19

Cette Bible est dans le domaine public.