Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Chroniques 18.26
Bible en Swahili de l’est


Expédition contre les Syriens

1 Basi, Yehoshafati alikuwa na mali na heshima tele, tena akafanya ujamaa na Ahabu.
2 Chroniques 17.5 2 Chroniques 21.6 2 Rois 8.18 2 Chroniques 19.2 1 Rois 21.25
2 Hata baada ya miaka kadha wa kadha akamshukia Ahabu huko Samaria. Ahabu akamchinjia kondoo na ng’ombe tele, yeye na watu waliokuwa pamoja naye, akamshawishi ili apande pamoja naye waende Ramoth-gileadi.
Josué 20.8 1 Rois 22.2-22.35 Esaïe 22.12-22.13 1 Rois 17.7 2 Chroniques 19.2
3 Ahabu, mfalme wa Israeli, akamwambia Yehoshafati, mfalme wa Yuda, Je! Utakwenda nami mpaka Ramoth-gileadi? Akamjibu, Mimi ni kama wewe, na watu wangu kama watu wako; nasi tutakuwa pamoja nawe vitani.
2 Rois 3.7 2 Jean 1.10-1.11 Psaumes 139.21 Ephésiens 5.11 1 Rois 22.4
4 Yehoshafati akamwambia mfalme wa Israeli, Uulize leo, nakusihi, kwa neno la Bwana.
2 Samuel 5.23 1 Samuel 23.4 1 Rois 22.5-22.6 2 Samuel 5.19 1 Samuel 23.2
5 Ndipo mfalme wa Israeli akawakusanya manabii, watu mia nne; akawaambia, Je! Tuende Ramoth-gileadi vitani, au niache? Wakasema, Kwea; kwa kuwa Mungu atautia mkononi mwa mfalme.
Jérémie 23.14 Jérémie 23.17 Michée 3.11 Michée 2.11 Jérémie 42.20
6 Lakini Yehoshafati akasema, Je! Hayupo hapa nabii wa Bwana tena, ili tumwulize yeye?
2 Rois 3.11-3.13 1 Rois 22.7-22.9
7 Mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati, Yupo mtu mmoja, ambaye tungeweza kumwuliza Bwana kwa yeye; lakini namchukia; kwa sababu hanibashirii mema kamwe, ila siku zote mabaya; naye ndiye Mikaya mwana wa Imla. Yehoshafati akasema, La! Mfalme asiseme hivi.
Luc 6.22 Jérémie 18.18 Psaumes 55.3 Jean 15.24 Actes 20.26-20.27
8 Ndipo mfalme wa Israeli akamwita akida mmoja, akasema, Mlete hima Mikaya mwana wa Imla.
1 Rois 22.9 Daniel 1.7-1.8 1 Chroniques 28.1 2 Chroniques 18.25-18.26 1 Samuel 8.15
9 Basi, mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda walikuwa wamekaa kila mtu katika kiti chake cha enzi, wamevaa mavazi yao, wakikaa penye sakafu pa kuingilia lango la Samaria; nao manabii wote wakafanya unabii mbele yao.
2 Chroniques 18.29 Ezéchiel 26.16 Jérémie 27.14-27.16 Daniel 7.9 Matthieu 11.8
10 Na Zedekia mwana wa Kenaana akajifanyia pembe za chuma, akasema, Bwana asema hivi, Kwa hizi utawasukuma Washami, hata watakapoangamia.
Jérémie 23.31 Jérémie 23.21 Jérémie 28.10-28.14 Ezéchiel 13.7 Zacharie 1.18-1.21
11 Na manabii wote wakatoa unabii huo, wakisema, Kwea Ramoth-gileadi, ukafanikiwe, kwa kuwa Bwana atautia mkononi mwa mfalme.
2 Chroniques 18.33-18.34 Jude 1.16 2 Chroniques 18.5 2 Pierre 2.1-2.3 Apocalypse 16.13-16.14
12 Na yule mjumbe, aliyekwenda kumwita Mikaya, akamwambia, akasema, Angalia, maneno ya manabii kwa kinywa kimoja yasema mema kwa mfalme; neno lako basi na liwe kama mojawapo lao, ukaseme mema.
1 Corinthiens 2.14-2.16 Amos 7.13 Job 22.13 Esaïe 30.10 Michée 2.6
13 Mikaya akasema, Kama aishivyo Bwana, neno lile atakalolinena Mungu wangu, ndilo nitakalolinena.
Nombres 22.35 Nombres 24.13 Nombres 22.18-22.20 Galates 1.10 1 Corinthiens 11.23
14 Na alipokuja kwa mfalme, mfalme akamwambia, Je! Mikaya, tuende Ramoth-gileadi vitani, au niache? Akasema, Kweeni, mkafanikiwe; nao watatiwa mikononi mwenu.
Matthieu 26.45 Lamentations 4.21 1 Rois 22.15 Ecclésiaste 11.1 Amos 4.4-4.5
15 Mfalme akamwambia, Mara ngapi nikuapishe, usiniambie neno ila yaliyo kweli, kwa jina la Bwana?
Actes 19.13 Matthieu 26.63 Marc 5.7 1 Rois 22.16 1 Samuel 14.24
16 Akasema, Naliwaona Waisraeli wote wametawanyika milimani, kama kondoo wasio na mchungaji; Bwana akasema, Hawa hawana bwana; na warudi kila mtu nyumbani kwake kwa amani.
Matthieu 9.36 Marc 6.34 Ezéchiel 34.8 1 Rois 22.17 Ezéchiel 34.5-34.6
17 Mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati, Je! Sikukuambia, hatanibashiria mema, ila mabaya?
Proverbes 29.1 Jérémie 43.2-43.3 2 Chroniques 18.7 1 Rois 22.18
18 Mikaya akasema, Sikieni basi neno la Bwana; Nalimwona Bwana ameketi katika kiti chake cha enzi na jeshi lote la mbinguni wamesimama mkono wake wa kuume na wa kushoto.
Daniel 7.9 Esaïe 6.1-6.5 Jérémie 19.3 1 Rois 22.19-22.23 Esaïe 1.10
19 Bwana akasema, Ni nani atakayemdanganya Ahabu mfalme wa Israeli, ili akwee Ramoth-gileadi akaanguke? Basi huyu akasema hivi; na huyu hivi.
Jacques 1.13-1.14 2 Chroniques 25.19 1 Rois 22.20 2 Chroniques 25.8 Esaïe 54.16
20 Akatoka pepo, akasimama mbele za Bwana, akasema, Mimi nitamdanganya. Bwana akamwambia, Jinsi gani?
Job 1.6 Job 2.1 2 Corinthiens 11.3 2 Corinthiens 11.13-11.15
21 Akasema, Nitaondoka, na kuwa pepo wa uongo vinywani mwa manabii wake wote. Akasema, Utamdanganya, na kudiriki pia; ondoka, ukafanye hivyo.
Jean 8.44 Job 1.12 Apocalypse 20.8 1 Jean 4.6 2 Chroniques 18.22
22 Basi sasa, angalia, Bwana ametia pepo wa uongo vinywani mwa manabii wako hawa; naye Bwana amenena mabaya juu yako.
Esaïe 19.14 Ezéchiel 14.9 Job 12.16 Esaïe 3.11 2 Thessaloniciens 2.9-2.11
23 Ndipo akakaribia Zedekia mwana wa Kenaana, akampiga Mikaya kofi la shavu, akasema, Alitokaje kwangu roho ya Bwana ili aseme na wewe?
Jérémie 20.2 Marc 14.65 Jean 18.22-18.23 Jérémie 29.26-29.27 1 Rois 22.23-22.25
24 Mikaya akasema, Angalia utaona siku ile, utakapoingia katika chumba cha ndani ili ujifiche.
Esaïe 26.11 1 Rois 20.30 Jérémie 29.32 Jérémie 29.21-29.22 Esaïe 26.20
25 Mfalme wa Israeli akasema, Mchukueni Mikaya mkamrudishe kwa Amoni mkuu wa mji, na kwa Yoashi mwana wa mfalme;
2 Chroniques 18.8 Jérémie 37.15-37.21 Jérémie 38.6-38.7 2 Chroniques 34.8 Actes 24.25-24.27
26 mkaseme, Mfalme asema hivi, Mtieni huyu gerezani, mkamlishe chakula cha shida, na maji ya shida, hata nitakaporudi kwa amani.
2 Chroniques 16.10 Proverbes 14.16 Deutéronome 29.19 2 Corinthiens 11.23 1 Samuel 25.21
27 Mikaya akasema, Ukirudi kabisa kwa amani, Bwana hakusema kwa mimi. Akasema, Sikieni, enyi watu wote.
Actes 13.10-13.11 Michée 1.2 Marc 7.14 Amos 9.10 Matthieu 15.10
28 Basi mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda wakakwea mpaka Ramoth-gileadi.
1 Rois 22.29-22.33
29 Mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati, Nitajibadilisha, na kuingia vitani; lakini wewe uvae mavazi yako. Mfalme wa Israeli akajibadilisha; nao wakaingia vitani.
1 Samuel 28.8 2 Chroniques 35.22-35.23 1 Rois 20.38 1 Rois 14.2-14.6 Job 24.15
30 Basi mfalme wa Shamu alikuwa amewaamuru maakida wa magari yake, akisema, Msipigane na mdogo wala mkuu, ila na mfalme wa Israeli peke yake.
1 Rois 20.33-20.34 Genèse 19.11 1 Rois 20.42 2 Chroniques 15.13 Deutéronome 1.17
31 Ikawa maakida wa magari walipomwona Yehoshafati, wakasema, Mfalme wa Israeli ni huyu. Basi wakamgeukia ili wapigane naye; lakini Yehoshafati akalia, na Bwana akamsaidia; Mungu akawafarakisha kwake.
2 Chroniques 13.14 Proverbes 21.1 2 Chroniques 14.11 2 Chroniques 26.7 Esdras 7.27
32 Ikawa, maakida wa magari walipoona ya kuwa siye mfalme wa Israeli, wakageuka nyuma wasimfuate.
1 Rois 22.33
33 Na mtu mmoja akavuta upinde kwa kubahatisha, akampiga mfalme wa Israeli mahali pa kuungana mavazi yake ya chuma; kwa hiyo akamwambia mwendesha gari, Geuza mkono wako, unichukue kutoka katika majeshi; kwa kuwa nimejeruhiwa sana.
2 Samuel 15.11 2 Chroniques 35.23 1 Rois 22.34-22.35
34 Pigano likazidi siku ile; lakini mfalme wa Israeli akajitegemeza garini juu ya Washami hata jioni; akafa kama wakati wa kuchwa kwa jua.
2 Chroniques 18.16 Proverbes 13.21 Nombres 32.23 Proverbes 28.17 2 Chroniques 18.27

Cette Bible est dans le domaine public.