Expédition contre les Syriens
 1 Basi, Yehoshafati alikuwa na mali na heshima tele, tena akafanya ujamaa na Ahabu.
2 Chroniques 17.5  2 Chroniques 21.6  2 Rois 8.18  2 Chroniques 19.2  Matthieu 6.33  
 2 Hata baada ya miaka kadha wa kadha akamshukia Ahabu huko Samaria. Ahabu akamchinjia kondoo na ng’ombe tele, yeye na watu waliokuwa pamoja naye, akamshawishi ili apande pamoja naye waende Ramoth-gileadi.1 Rois 4.13  1 Rois 1.9  Josué 20.8  1 Rois 22.2-22.35  Esaïe 22.12-22.13  
 3 Ahabu, mfalme wa Israeli, akamwambia Yehoshafati, mfalme wa Yuda, Je! Utakwenda nami mpaka Ramoth-gileadi? Akamjibu, Mimi ni kama wewe, na watu wangu kama watu wako; nasi tutakuwa pamoja nawe vitani.
Ephésiens 5.11  1 Rois 22.4  2 Rois 3.7  2 Jean 1.10-1.11  Psaumes 139.21  
 4 Yehoshafati akamwambia mfalme wa Israeli, Uulize leo, nakusihi, kwa neno la Bwana.
Ezéchiel 20.3  Jérémie 21.2  2 Samuel 5.23  1 Samuel 23.4  1 Rois 22.5-22.6  
 5 Ndipo mfalme wa Israeli akawakusanya manabii, watu mia nne; akawaambia, Je! Tuende Ramoth-gileadi vitani, au niache? Wakasema, Kwea; kwa kuwa Mungu atautia mkononi mwa mfalme.
Jérémie 42.2-42.3  2 Timothée 4.3  Ezéchiel 13.22  Jérémie 8.10-8.11  Jérémie 38.14-38.28  
 6 Lakini Yehoshafati akasema, Je! Hayupo hapa nabii wa Bwana tena, ili tumwulize yeye?
2 Rois 3.11-3.13  1 Rois 22.7-22.9  
 7 Mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati, Yupo mtu mmoja, ambaye tungeweza kumwuliza Bwana kwa yeye; lakini namchukia; kwa sababu hanibashirii mema kamwe, ila siku zote mabaya; naye ndiye Mikaya mwana wa Imla. Yehoshafati akasema, La! Mfalme asiseme hivi.
Luc 6.22  Marc 6.27  Proverbes 9.8  Jérémie 38.4  2 Chroniques 18.13  
 8 Ndipo mfalme wa Israeli akamwita akida mmoja, akasema, Mlete hima Mikaya mwana wa Imla.
Daniel 1.3  Esaïe 39.7  1 Rois 22.9  Daniel 1.7-1.8  1 Chroniques 28.1  
 9 Basi, mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda walikuwa wamekaa kila mtu katika kiti chake cha enzi, wamevaa mavazi yao, wakikaa penye sakafu pa kuingilia lango la Samaria; nao manabii wote wakafanya unabii mbele yao.
1 Rois 22.10-22.12  Ruth 4.1  2 Chroniques 18.29  Ezéchiel 26.16  Jérémie 27.14-27.16  
 10 Na Zedekia mwana wa Kenaana akajifanyia pembe za chuma, akasema, Bwana asema hivi, Kwa hizi utawasukuma Washami, hata watakapoangamia.
2 Timothée 3.8  Jérémie 23.17  Jérémie 23.31  Jérémie 23.21  Jérémie 28.10-28.14  
 11 Na manabii wote wakatoa unabii huo, wakisema, Kwea Ramoth-gileadi, ukafanikiwe, kwa kuwa Bwana atautia mkononi mwa mfalme.
Proverbes 24.24-24.25  Michée 3.5  2 Chroniques 18.33-18.34  Jude 1.16  2 Chroniques 18.5  
 12 Na yule mjumbe, aliyekwenda kumwita Mikaya, akamwambia, akasema, Angalia, maneno ya manabii kwa kinywa kimoja yasema mema kwa mfalme; neno lako basi na liwe kama mojawapo lao, ukaseme mema.
Osée 7.3  Michée 2.11  1 Corinthiens 2.14-2.16  Amos 7.13  Job 22.13  
 13 Mikaya akasema, Kama aishivyo Bwana, neno lile atakalolinena Mungu wangu, ndilo nitakalolinena.
Nombres 22.35  Nombres 24.13  Nombres 22.18-22.20  Michée 2.6-2.7  Nombres 23.12  
 14 Na alipokuja kwa mfalme, mfalme akamwambia, Je! Mikaya, tuende Ramoth-gileadi vitani, au niache? Akasema, Kweeni, mkafanikiwe; nao watatiwa mikononi mwenu.
Amos 4.4-4.5  1 Rois 18.27  Matthieu 26.45  Lamentations 4.21  1 Rois 22.15  
 15 Mfalme akamwambia, Mara ngapi nikuapishe, usiniambie neno ila yaliyo kweli, kwa jina la Bwana?
1 Rois 22.16  1 Samuel 14.24  Actes 19.13  Matthieu 26.63  Marc 5.7  
 16 Akasema, Naliwaona Waisraeli wote wametawanyika milimani, kama kondoo wasio na mchungaji; Bwana akasema, Hawa hawana bwana; na warudi kila mtu nyumbani kwake kwa amani.
Matthieu 9.36  Nombres 27.17  Marc 6.34  Ezéchiel 34.8  1 Rois 22.17  
 17 Mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati, Je! Sikukuambia, hatanibashiria mema, ila mabaya?
2 Chroniques 18.7  1 Rois 22.18  Proverbes 29.1  Jérémie 43.2-43.3  
 18 Mikaya akasema, Sikieni basi neno la Bwana; Nalimwona Bwana ameketi katika kiti chake cha enzi na jeshi lote la mbinguni wamesimama mkono wake wa kuume na wa kushoto.
Daniel 7.9  Esaïe 6.1-6.5  Jérémie 34.4  Psaumes 103.20-103.21  Jérémie 19.3  
 19 Bwana akasema, Ni nani atakayemdanganya Ahabu mfalme wa Israeli, ili akwee Ramoth-gileadi akaanguke? Basi huyu akasema hivi; na huyu hivi.
Job 12.16  Proverbes 11.5  Jacques 1.13-1.14  2 Chroniques 25.19  1 Rois 22.20  
 20 Akatoka pepo, akasimama mbele za Bwana, akasema, Mimi nitamdanganya. Bwana akamwambia, Jinsi gani?
Job 1.6  2 Corinthiens 11.13-11.15  Job 2.1  2 Corinthiens 11.3  
 21 Akasema, Nitaondoka, na kuwa pepo wa uongo vinywani mwa manabii wake wote. Akasema, Utamdanganya, na kudiriki pia; ondoka, ukafanye hivyo.
Jean 8.44  Genèse 3.4-3.5  Psaumes 109.17  Job 1.12  Apocalypse 20.8  
 22 Basi sasa, angalia, Bwana ametia pepo wa uongo vinywani mwa manabii wako hawa; naye Bwana amenena mabaya juu yako.
Ezéchiel 14.9  Esaïe 19.14  Job 12.16  Matthieu 24.24-24.25  Jérémie 18.11  
 23 Ndipo akakaribia Zedekia mwana wa Kenaana, akampiga Mikaya kofi la shavu, akasema, Alitokaje kwangu roho ya Bwana ili aseme na wewe?
Marc 14.65  Jérémie 20.2  Jean 9.40-9.41  Jean 18.22-18.23  Jérémie 29.26-29.27  
 24 Mikaya akasema, Angalia utaona siku ile, utakapoingia katika chumba cha ndani ili ujifiche.
Esaïe 26.20  Jérémie 28.16-28.17  Esaïe 26.11  1 Rois 20.30  Jérémie 29.32  
 25 Mfalme wa Israeli akasema, Mchukueni Mikaya mkamrudishe kwa Amoni mkuu wa mji, na kwa Yoashi mwana wa mfalme;
2 Chroniques 18.8  Actes 24.25-24.27  Jérémie 37.15-37.21  Jérémie 38.6-38.7  2 Chroniques 34.8  
 26 mkaseme, Mfalme asema hivi, Mtieni huyu gerezani, mkamlishe chakula cha shida, na maji ya shida, hata nitakaporudi kwa amani.
2 Chroniques 16.10  Jérémie 20.2-20.3  Actes 22.22  Luc 23.2  1 Rois 22.26-22.28  
 27 Mikaya akasema, Ukirudi kabisa kwa amani, Bwana hakusema kwa mimi. Akasema, Sikieni, enyi watu wote.
Nombres 16.29  Matthieu 13.9  Actes 13.10-13.11  Michée 1.2  Marc 7.14  
 28 Basi mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda wakakwea mpaka Ramoth-gileadi.
1 Rois 22.29-22.33  
 29 Mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati, Nitajibadilisha, na kuingia vitani; lakini wewe uvae mavazi yako. Mfalme wa Israeli akajibadilisha; nao wakaingia vitani.
1 Samuel 28.8  Psaumes 12.2  Jérémie 23.24  2 Chroniques 35.22-35.23  1 Rois 20.38  
 30 Basi mfalme wa Shamu alikuwa amewaamuru maakida wa magari yake, akisema, Msipigane na mdogo wala mkuu, ila na mfalme wa Israeli peke yake.
2 Chroniques 15.13  Deutéronome 1.17  1 Rois 20.33-20.34  Genèse 19.11  1 Rois 20.42  
 31 Ikawa maakida wa magari walipomwona Yehoshafati, wakasema, Mfalme wa Israeli ni huyu. Basi wakamgeukia ili wapigane naye; lakini Yehoshafati akalia, na Bwana akamsaidia; Mungu akawafarakisha kwake.
2 Chroniques 13.14  Néhémie 1.11  Psaumes 34.7  Psaumes 116.1-116.2  Proverbes 21.1  
 32 Ikawa, maakida wa magari walipoona ya kuwa siye mfalme wa Israeli, wakageuka nyuma wasimfuate.
1 Rois 22.33  
 33 Na mtu mmoja akavuta upinde kwa kubahatisha, akampiga mfalme wa Israeli mahali pa kuungana mavazi yake ya chuma; kwa hiyo akamwambia mwendesha gari, Geuza mkono wako, unichukue kutoka katika majeshi; kwa kuwa nimejeruhiwa sana.
2 Chroniques 35.23  1 Rois 22.34-22.35  2 Samuel 15.11  
 34 Pigano likazidi siku ile; lakini mfalme wa Israeli akajitegemeza garini juu ya Washami hata jioni; akafa kama wakati wa kuchwa kwa jua.
2 Chroniques 18.27  2 Chroniques 18.19  2 Chroniques 18.16  Proverbes 13.21  Nombres 32.23