1 Basi, Yehoshafati alikuwa na mali na heshima tele, tena akafanya ujamaa na Ahabu.
2 Chroniques 17.5  2 Chroniques 21.6  2 Rois 8.18  2 Chroniques 19.2  1 Rois 21.25  
 2 Hata baada ya miaka kadha wa kadha akamshukia Ahabu huko Samaria. Ahabu akamchinjia kondoo na ng’ombe tele, yeye na watu waliokuwa pamoja naye, akamshawishi ili apande pamoja naye waende Ramoth-gileadi.Josué 20.8  1 Rois 22.2-22.35  Esaïe 22.12-22.13  1 Rois 17.7  2 Chroniques 19.2  
 3 Ahabu, mfalme wa Israeli, akamwambia Yehoshafati, mfalme wa Yuda, Je! Utakwenda nami mpaka Ramoth-gileadi? Akamjibu, Mimi ni kama wewe, na watu wangu kama watu wako; nasi tutakuwa pamoja nawe vitani.
2 Rois 3.7  2 Jean 1.10-1.11  Psaumes 139.21  Ephésiens 5.11  1 Rois 22.4  
 4 Yehoshafati akamwambia mfalme wa Israeli, Uulize leo, nakusihi, kwa neno la Bwana.
2 Samuel 5.23  1 Samuel 23.4  1 Rois 22.5-22.6  2 Samuel 5.19  1 Samuel 23.2  
 5 Ndipo mfalme wa Israeli akawakusanya manabii, watu mia nne; akawaambia, Je! Tuende Ramoth-gileadi vitani, au niache? Wakasema, Kwea; kwa kuwa Mungu atautia mkononi mwa mfalme.
Jérémie 23.14  Jérémie 23.17  Michée 3.11  Michée 2.11  Jérémie 42.20  
 6 Lakini Yehoshafati akasema, Je! Hayupo hapa nabii wa Bwana tena, ili tumwulize yeye?
2 Rois 3.11-3.13  1 Rois 22.7-22.9  
 7 Mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati, Yupo mtu mmoja, ambaye tungeweza kumwuliza Bwana kwa yeye; lakini namchukia; kwa sababu hanibashirii mema kamwe, ila siku zote mabaya; naye ndiye Mikaya mwana wa Imla. Yehoshafati akasema, La! Mfalme asiseme hivi.
Luc 6.22  Jérémie 18.18  Psaumes 55.3  Jean 15.24  Actes 20.26-20.27  
 8 Ndipo mfalme wa Israeli akamwita akida mmoja, akasema, Mlete hima Mikaya mwana wa Imla.
1 Rois 22.9  Daniel 1.7-1.8  1 Chroniques 28.1  2 Chroniques 18.25-18.26  1 Samuel 8.15  
 9 Basi, mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda walikuwa wamekaa kila mtu katika kiti chake cha enzi, wamevaa mavazi yao, wakikaa penye sakafu pa kuingilia lango la Samaria; nao manabii wote wakafanya unabii mbele yao.
2 Chroniques 18.29  Ezéchiel 26.16  Jérémie 27.14-27.16  Daniel 7.9  Matthieu 11.8  
 10 Na Zedekia mwana wa Kenaana akajifanyia pembe za chuma, akasema, Bwana asema hivi, Kwa hizi utawasukuma Washami, hata watakapoangamia.
Jérémie 23.31  Jérémie 23.21  Jérémie 28.10-28.14  Ezéchiel 13.7  Zacharie 1.18-1.21  
 11 Na manabii wote wakatoa unabii huo, wakisema, Kwea Ramoth-gileadi, ukafanikiwe, kwa kuwa Bwana atautia mkononi mwa mfalme.
2 Chroniques 18.33-18.34  Jude 1.16  2 Chroniques 18.5  2 Pierre 2.1-2.3  Apocalypse 16.13-16.14  
 12 Na yule mjumbe, aliyekwenda kumwita Mikaya, akamwambia, akasema, Angalia, maneno ya manabii kwa kinywa kimoja yasema mema kwa mfalme; neno lako basi na liwe kama mojawapo lao, ukaseme mema.
1 Corinthiens 2.14-2.16  Amos 7.13  Job 22.13  Esaïe 30.10  Michée 2.6  
 13 Mikaya akasema, Kama aishivyo Bwana, neno lile atakalolinena Mungu wangu, ndilo nitakalolinena.
Nombres 22.35  Nombres 24.13  Nombres 22.18-22.20  Galates 1.10  1 Corinthiens 11.23  
 14 Na alipokuja kwa mfalme, mfalme akamwambia, Je! Mikaya, tuende Ramoth-gileadi vitani, au niache? Akasema, Kweeni, mkafanikiwe; nao watatiwa mikononi mwenu.
Matthieu 26.45  Lamentations 4.21  1 Rois 22.15  Ecclésiaste 11.1  Amos 4.4-4.5  
 15 Mfalme akamwambia, Mara ngapi nikuapishe, usiniambie neno ila yaliyo kweli, kwa jina la Bwana?
Actes 19.13  Matthieu 26.63  Marc 5.7  1 Rois 22.16  1 Samuel 14.24  
 16 Akasema, Naliwaona Waisraeli wote wametawanyika milimani, kama kondoo wasio na mchungaji; Bwana akasema, Hawa hawana bwana; na warudi kila mtu nyumbani kwake kwa amani.
Matthieu 9.36  Marc 6.34  Ezéchiel 34.8  1 Rois 22.17  Ezéchiel 34.5-34.6  
 17 Mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati, Je! Sikukuambia, hatanibashiria mema, ila mabaya?
Proverbes 29.1  Jérémie 43.2-43.3  2 Chroniques 18.7  1 Rois 22.18  
 18 Mikaya akasema, Sikieni basi neno la Bwana; Nalimwona Bwana ameketi katika kiti chake cha enzi na jeshi lote la mbinguni wamesimama mkono wake wa kuume na wa kushoto.
Daniel 7.9  Esaïe 6.1-6.5  Jérémie 19.3  1 Rois 22.19-22.23  Esaïe 1.10  
 19 Bwana akasema, Ni nani atakayemdanganya Ahabu mfalme wa Israeli, ili akwee Ramoth-gileadi akaanguke? Basi huyu akasema hivi; na huyu hivi.
Jacques 1.13-1.14  2 Chroniques 25.19  1 Rois 22.20  2 Chroniques 25.8  Esaïe 54.16  
 20 Akatoka pepo, akasimama mbele za Bwana, akasema, Mimi nitamdanganya. Bwana akamwambia, Jinsi gani?
Job 1.6  Job 2.1  2 Corinthiens 11.3  2 Corinthiens 11.13-11.15  
 21 Akasema, Nitaondoka, na kuwa pepo wa uongo vinywani mwa manabii wake wote. Akasema, Utamdanganya, na kudiriki pia; ondoka, ukafanye hivyo.
Jean 8.44  Job 1.12  Apocalypse 20.8  1 Jean 4.6  2 Chroniques 18.22  
 22 Basi sasa, angalia, Bwana ametia pepo wa uongo vinywani mwa manabii wako hawa; naye Bwana amenena mabaya juu yako.
Esaïe 19.14  Ezéchiel 14.9  Job 12.16  Esaïe 3.11  2 Thessaloniciens 2.9-2.11  
 23 Ndipo akakaribia Zedekia mwana wa Kenaana, akampiga Mikaya kofi la shavu, akasema, Alitokaje kwangu roho ya Bwana ili aseme na wewe?
Jérémie 20.2  Marc 14.65  Jean 18.22-18.23  Jérémie 29.26-29.27  1 Rois 22.23-22.25  
 24 Mikaya akasema, Angalia utaona siku ile, utakapoingia katika chumba cha ndani ili ujifiche.
Esaïe 26.11  1 Rois 20.30  Jérémie 29.32  Jérémie 29.21-29.22  Esaïe 26.20  
 25 Mfalme wa Israeli akasema, Mchukueni Mikaya mkamrudishe kwa Amoni mkuu wa mji, na kwa Yoashi mwana wa mfalme;
2 Chroniques 18.8  Jérémie 37.15-37.21  Jérémie 38.6-38.7  2 Chroniques 34.8  Actes 24.25-24.27  
 26 mkaseme, Mfalme asema hivi, Mtieni huyu gerezani, mkamlishe chakula cha shida, na maji ya shida, hata nitakaporudi kwa amani.
2 Chroniques 16.10  Proverbes 14.16  Deutéronome 29.19  2 Corinthiens 11.23  1 Samuel 25.21  
 27 Mikaya akasema, Ukirudi kabisa kwa amani, Bwana hakusema kwa mimi. Akasema, Sikieni, enyi watu wote.
Actes 13.10-13.11  Michée 1.2  Marc 7.14  Amos 9.10  Matthieu 15.10  
 28 Basi mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda wakakwea mpaka Ramoth-gileadi.
1 Rois 22.29-22.33  
 29 Mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati, Nitajibadilisha, na kuingia vitani; lakini wewe uvae mavazi yako. Mfalme wa Israeli akajibadilisha; nao wakaingia vitani.
1 Samuel 28.8  2 Chroniques 35.22-35.23  1 Rois 20.38  1 Rois 14.2-14.6  Job 24.15  
 30 Basi mfalme wa Shamu alikuwa amewaamuru maakida wa magari yake, akisema, Msipigane na mdogo wala mkuu, ila na mfalme wa Israeli peke yake.
1 Rois 20.33-20.34  Genèse 19.11  1 Rois 20.42  2 Chroniques 15.13  Deutéronome 1.17  
 31 Ikawa maakida wa magari walipomwona Yehoshafati, wakasema, Mfalme wa Israeli ni huyu. Basi wakamgeukia ili wapigane naye; lakini Yehoshafati akalia, na Bwana akamsaidia; Mungu akawafarakisha kwake.
2 Chroniques 13.14  Proverbes 21.1  2 Chroniques 14.11  2 Chroniques 26.7  Esdras 7.27  
 32 Ikawa, maakida wa magari walipoona ya kuwa siye mfalme wa Israeli, wakageuka nyuma wasimfuate.
1 Rois 22.33  
 33 Na mtu mmoja akavuta upinde kwa kubahatisha, akampiga mfalme wa Israeli mahali pa kuungana mavazi yake ya chuma; kwa hiyo akamwambia mwendesha gari, Geuza mkono wako, unichukue kutoka katika majeshi; kwa kuwa nimejeruhiwa sana.
2 Samuel 15.11  2 Chroniques 35.23  1 Rois 22.34-22.35  
 34 Pigano likazidi siku ile; lakini mfalme wa Israeli akajitegemeza garini juu ya Washami hata jioni; akafa kama wakati wa kuchwa kwa jua.
2 Chroniques 18.16  Proverbes 13.21  Nombres 32.23  Proverbes 28.17  2 Chroniques 18.27