Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Chroniques 10.10
Bible en Swahili de l’est


Juda à partir du schisme

Division du royaume

1 Rehoboamu akaenda Shekemu; maana Israeli wote walikuwa wamekuja Shekemu, ili wamfanye mfalme.
Josué 24.1 1 Chroniques 3.10 Genèse 12.6 1 Rois 12.1-12.20 Genèse 37.12-37.13
2 Ikawa Yeroboamu mwana wa Nebati aliposikia, (maana alikuwako Misri, ambako amekimbilia mbele ya mfalme Sulemani), Yeroboamu akarudi kutoka Misri.
1 Rois 11.40 1 Rois 11.26 1 Rois 12.2 1 Rois 11.28
3 Wakapeleka ujumbe, wakamwita, Yeroboamu akaja na Israeli wote, wakamwambia Rehoboamu, wakasema,
1 Rois 12.3
4 Baba yako alilifanya zito kongwa letu; basi sasa upunguze utumwa mgumu wa baba yako, na kongwa lake zito alilotutwika, nasi tutakutumikia.
1 Rois 4.25 1 Samuel 8.11-8.18 Exode 1.13-1.14 Exode 2.23 1 Jean 5.3
5 Akawaambia, Mnirudie baada ya siku tatu. Watu wakaenda zao.
Proverbes 3.28 1 Rois 12.5
6 Mfalme Rehoboamu akataka shauri kwa wazee, waliosimama mbele ya Sulemani baba yake, alipokuwa hai bado, akasema, Mwanipa shauri gani la kuwajibu watu hawa?
Job 32.7 Jérémie 42.2-42.5 Proverbes 19.20 Jérémie 42.20 Job 12.12-12.13
7 Wakamwambia, wakasema, Ukiwa mwema kwao watu hawa, na kuwapendeza, na kuwaambia maneno mazuri, ndipo watakapokuwa watumishi wako siku zote.
Proverbes 15.1 1 Rois 12.7 2 Samuel 15.2-15.6 Genèse 49.21
8 Lakini akaliacha shauri lile la wazee walilompa, akataka shauri kwa wale vijana waliokua pamoja naye, waliosimama mbele yake.
2 Samuel 17.14 2 Chroniques 25.15-25.16 Proverbes 9.9 Proverbes 13.20 Proverbes 19.20
9 Akawaambia, Je! Mwanipa shauri gani la kuwajibu watu hawa, waliosema nami, wakisema, Utufanyie jepesi kongwa alilotutwika baba yako.
2 Chroniques 10.6 1 Rois 22.6-22.8 2 Samuel 17.5-17.6
10 Na wale vijana waliokua pamoja naye wakamwambia, wakasema, Uwaambie hivi watu wale waliosema nawe, wakinena, Baba yako alilifanya zito kongwa letu, lakini wewe tufanyie jepesi; uwaambie hivi, Kidole changu cha mwisho ni kinene kuliko kiuno cha baba yangu.
Proverbes 21.30 Proverbes 28.25 Esaïe 19.11-19.13 1 Rois 12.10-12.11 Proverbes 14.16
11 Basi kama baba yangu aliwatwika kongwa zito, mimi nitaongeza kongwa lenu; baba yangu akiwapiga kwa mijeledi, lakini mimi nitawapiga kwa nge.
Matthieu 11.29 Apocalypse 9.5 Exode 1.13-1.14 Apocalypse 9.10 Exode 5.18
12 Basi Yeroboamu na watu wote wakamjia Rehoboamu siku ya tatu, kama mfalme alivyoamuru, akisema, Mnirudie siku ya tatu.
1 Rois 12.12-12.15 2 Chroniques 10.5
13 Mfalme akawajibu kwa ukali; mfalme Rehoboamu akaliacha shauri la wazee, akasema nao kwa shauri la vijana,
Exode 10.28 Genèse 42.7 Genèse 42.30 Proverbes 15.1 1 Samuel 25.10-25.11
14 akinena, Baba yangu aliwafanyia kongwa zito, nami nitawaongezea; baba yangu aliwapiga kwa mijeledi, lakini mimi nitawapiga kwa nge.
Ecclésiaste 2.19 2 Chroniques 10.10-10.11 Ecclésiaste 7.8 Daniel 6.7 2 Chroniques 22.4-22.5
15 Basi mfalme hakuwasikia wale watu; maana jambo hili lilitoka kwa Mungu, ili alithibitishe neno lake alilomwambia Yeroboamu mwana wa Nebati kwa mkono wa Ahiya Mshiloni.
1 Rois 11.29-11.39 2 Chroniques 25.16-25.20 1 Samuel 2.25 Actes 2.23 Esaïe 19.14
16 Basi Israeli wote walipoona ya kuwa mfalme hawasikilizi, watu wakamjibu mfalme, wakasema, Tuna sehemu gani katika Daudi? Wala hatuna urithi katika mwana wa Yese; nendeni zenu hemani kwenu, enyi Israeli, kila mtu; sasa itunze nyumba yako mwenyewe, Daudi. Basi wakaenda zao Israeli wote hemani kwao.
2 Samuel 20.1 2 Chroniques 10.19 2 Samuel 16.11 2 Samuel 15.13 Esaïe 9.6-9.7
17 Lakini kwa habari za wana wa Israeli waliokaa katika miji ya Yuda, Rehoboamu alitawala juu yao.
2 Chroniques 11.1 1 Rois 11.36 1 Rois 12.17
18 Ndipo mfalme Rehoboamu akamtuma Adoramu, msimamizi wa shokoa; nao wana wa Israeli wakamtupia mawe, hata akafa. Mfalme Rehoboamu akafanya haraka kupanda garini mwake, ili akimbilie Yerusalemu.
1 Rois 5.14 1 Rois 4.6 2 Chroniques 24.21 Actes 7.57-7.58
19 Hivyo Israeli wakaasi juu ya nyumba ya Daudi, hata leo.
2 Chroniques 13.5-13.7 1 Rois 12.19-12.20 2 Chroniques 5.9 Esdras 9.7 2 Rois 17.21-17.23

Cette Bible est dans le domaine public.