Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Chroniques 13.4
Bible en Swahili de l’est


Dépôt de l’arche chez Obed-Edom

1 Kisha Daudi akafanya shauri na maakida wa maelfu, na maakida wa mamia, naam, na kila kiongozi.
1 Chroniques 12.14 2 Rois 23.1 2 Chroniques 34.29-34.30 1 Chroniques 12.32 2 Chroniques 29.20
2 Daudi akawaambia jamii yote ya Israeli, Likiwa jema kwenu, tena likiwa limetoka kwa Bwana, Mungu wetu, na tutume watu huku na huku mahali pote kwa ndugu zetu waliosalia katika nchi yote ya Israeli, ambao pamoja nao makuhani na Walawi wamo ndani ya miji yao yenye viunga, ili wakusanyike kwetu;
1 Samuel 31.1 2 Chroniques 31.4-31.21 Nombres 4.4-4.20 1 Chroniques 6.54-6.81 1 Chroniques 10.7
3 nasi tujirudishie tena sanduku la Mungu wetu; maana hamkuuliza neno kwa hilo katika siku za Sauli.
1 Samuel 7.1-7.2 1 Samuel 14.36 Psaumes 132.6 1 Samuel 14.18 1 Samuel 23.9-23.12
4 Nao jamii nzima wakasema ya kwamba watafanya hivyo; kwa kuwa neno hilo lilikuwa jema machoni pa watu wote.
2 Samuel 3.36 Esther 8.5 1 Samuel 18.20 2 Chroniques 30.4
5 Basi Daudi akawakusanya Israeli wote, toka Shihori, kijito cha Misri, hata pa kuingilia Hamathi, ili kwamba walilete sanduku la Mungu kutoka Kiriath-yearimu.
1 Samuel 6.21-7.1 1 Rois 8.65 2 Samuel 6.1 1 Chroniques 15.3 Josué 13.3-13.6
6 Basi Daudi akapanda, yeye na Israeli wote, mpaka Baala, ndio Kiriath-yearimu, ulio wa Yuda, ili kulileta toka huko sanduku la Mungu, Bwana akaaye juu ya makerubi, lililoitwa kwa Jina lake.
Josué 15.9 Exode 25.22 2 Rois 19.15 1 Samuel 4.4 Josué 15.60
7 Wakalipandisha sanduku la Mungu juu ya gari jipya kutoka nyumba ya Abinadabu; na Uza na Ahio wakaliendesha lile gari.
Nombres 4.15 1 Chroniques 15.13 2 Samuel 6.3 1 Chroniques 15.2 1 Samuel 6.7
8 Wakacheza Daudi na Israeli wote, mbele za Mungu, kwa nguvu zao zote; na kwa nyimbo na kwa vinubi, na kwa vinanda, na kwa matari, na kwa matoazi, na kwa tarumbeta.
Daniel 3.5-3.7 1 Samuel 10.5 Psaumes 150.3-150.5 Amos 5.23 1 Chroniques 16.5
9 Hata walipofika penye uga wa Nakoni, Uza akaunyosha mkono wake alishike sanduku; kwa maana wale ng’ombe walikunguwaa.
2 Samuel 6.6
10 Ndipo hasira ya Bwana ikawaka juu ya Uza, naye akampiga, kwa sababu alilinyoshea sanduku mkono wake, hata akafa pale pale mbele za Mungu.
1 Chroniques 15.15 1 Chroniques 15.13 Nombres 4.15 2 Chroniques 26.16-26.20 1 Corinthiens 11.30-11.32
11 Naye Daudi akaona uchungu, kwa kuwa Bwana amemfurikia Uza; akapaita mahali pale Peres-uza hata leo.
Jonas 4.4 Deutéronome 34.6 Josué 4.9 2 Samuel 6.7 Jonas 4.9
12 Naye Daudi akamwogopa Mungu siku ile, akasema, Nitajileteaje sanduku la Mungu kwangu?
Esaïe 6.5 Job 25.5-25.6 1 Rois 8.27 1 Samuel 5.10-5.11 Luc 5.8-5.9
13 Basi Daudi hakujichukulia sanduku mjini mwa Daudi, ila akalihamisha kando na kulitia nyumbani kwa Obed-edomu Mgiti.
1 Chroniques 26.4 1 Chroniques 15.18 2 Samuel 6.10-6.11 1 Chroniques 16.5 1 Chroniques 26.8
14 Sanduku la Mungu likakaa na jamaa ya Obed-edomu, nyumbani mwake, muda wa miezi mitatu; naye Bwana akaibariki nyumba ya Obed-edomu, na yote aliyokuwa nayo.
1 Chroniques 26.4-26.5 Genèse 30.27 Genèse 39.5 Proverbes 3.9-3.10 Proverbes 10.22

Cette Bible est dans le domaine public.