Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Rois 20.4
Bible en Swahili de l’est


Maladie et guérison d’Ézéchias

1 Siku hizo Hezekia akaugua, akawa katika hatari ya kufa. Isaya, nabii, mwana wa Amozi, akamjia akamwambia, Bwana asema hivi, Tengeza mambo ya nyumba yako; maana utakufa, wala hutapona.
2 Samuel 17.23 2 Rois 19.20 2 Chroniques 32.24-32.26 2 Rois 19.2 Jonas 3.4-3.10
2 Basi Hezekia akajigeuza, akaelekeza uso wake ukutani, akamwomba Bwana akasema,
Psaumes 50.15 1 Rois 8.30 Matthieu 6.6 Esaïe 38.2-38.3
3 Nakusihi, Bwana, ukumbuke sasa, jinsi nilivyokwenda mbele zako katika kweli na kwa moyo mkamilifu, na kutenda yaliyo mema machoni pako. Hezekia akalia sana sana.
Néhémie 13.22 Néhémie 5.19 2 Rois 18.3-18.6 Néhémie 13.14 Néhémie 13.31
4 Ikawa, kabla Isaya hajatoka katika mji wa kati, neno la Bwana likamjia, kusema,
1 Rois 7.8 2 Rois 22.14
5 Rudi, ukamwambie Hezekia, mkuu wa watu wangu, Bwana, Mungu wa Daudi baba yako asema hivi, Nimeyasikia maombi yako, na kuyaona machozi yako; tazama, nitakuponya; siku ya tatu utapanda nyumbani kwa Bwana.
Psaumes 39.12 2 Rois 19.20 Psaumes 66.19-66.20 1 Samuel 9.16 1 Samuel 10.1
6 Tena, nitazizidisha siku zako, kiasi cha miaka kumi na mitano, nami nitakuokoa wewe, na mji huu, na mkono wa mfalme wa Ashuru, nami nitaulinda mji huu kwa ajili yangu, na kwa ajili ya Daudi, mtumishi wangu.
2 Rois 19.34 Psaumes 116.15 Actes 27.24 Esaïe 10.24 2 Chroniques 32.22
7 Naye Isaya akasema, Twaeni mkate wa tini. Wakautwaa, wakauweka juu ya jipu, naye akapona.
Esaïe 38.21 2 Rois 4.41 2 Rois 2.20-2.22
8 Hezekia akamwambia Isaya, Je! Kutakuwa na ishara gani ya kwamba Bwana ataniponya, nami siku ya tatu nitapanda nyumbani kwa Bwana.
Esaïe 7.11 Osée 6.2 Esaïe 7.14 2 Rois 20.5 Esaïe 38.22
9 Isaya akamwambia, Jambo hili litakuwa ishara kwako, itokayo kwa Bwana, ya kwamba Bwana atalifanya neno hilo alilolinena; je! Kivuli kiendelee madaraja kumi, au kirudi nyuma madaraja kumi?
Esaïe 38.7-38.8 Marc 8.11-8.12 Luc 11.29-11.30 Matthieu 16.1-16.4
10 Hezekia akajibu, Ni jambo jepesi kivuli kuendelea madaraja kumi; la, hicho kivuli na kirudi nyuma madaraja kumi.
2 Rois 2.10 2 Rois 3.18 Esaïe 49.6 Marc 9.28-9.29 Jean 14.12
11 Isaya nabii akamlilia Bwana; akakirudisha nyuma kile kivuli madaraja kumi, ambayo kilikuwa kimeshuka katika madaraja ya Ahazi.
Josué 10.12-10.14 Esaïe 38.8 Exode 14.15 1 Rois 18.36-18.38 2 Chroniques 32.31

Erreur d’Ézéchias

12 Wakati huo Merodak-baladani mwana wa Baladani, Mfalme wa Babeli, alipeleka barua na zawadi kwa Hezekia; kwa maana alipata habari kwamba Hezekia ameugua.
Esaïe 39.1-39.8 2 Chroniques 32.31 Esaïe 14.4 2 Samuel 8.10 Genèse 10.10
13 Hezekia akawasikiliza, akawaonyesha nyumba yote yenye vitu vyake vya thamani, fedha, na dhahabu, na manukato, na marhamu ya thamani, na nyumba yenye silaha zake, na vitu vyote vilivyoonekana katika hazina zake. Wala hapakuwa na kitu asichowaonyesha Hezekia, katika nyumba yake, wala katika ufalme wake wote.
Esaïe 39.2 1 Rois 10.25 Proverbes 23.5 1 Rois 10.15 1 Rois 10.10
14 Ndipo Isaya nabii akamwendea mfalme Hezekia, akamwambia, Wasemaje watu hawa? Nao wametoka wapi kuja kwako? Hezekia akasema, Wametoka katika nchi iliyo mbali, yaani Babeli.
2 Chroniques 16.7-16.10 Esaïe 39.3-39.8 Jérémie 26.18-26.19 Josué 9.9 Esaïe 13.5
15 Ndipo akasema, Wameona nini nyumbani mwako? Hezekia akajibu, Vitu vyote vilivyomo nyumbani mwangu wameviona; hapana kitu nisichowaonyesha katika hazina zangu.
Proverbes 28.13 Josué 7.19 2 Rois 20.13 1 Jean 1.8-1.10 Job 31.33
16 Isaya akamwambia Hezekia, Basi, lisikie neno la Bwana,
Esaïe 1.10 2 Rois 7.1 1 Rois 22.19 Amos 7.16
17 Angalia, siku zinakuja, ambazo vitu vyote vilivyomo nyumbani mwako, na hivyo vilivyowekwa akiba na baba zako hata leo, vitachukuliwa mpaka Babeli; hakitasalia kitu, asema Bwana.
2 Rois 24.13 2 Chroniques 36.10 Jérémie 27.21-27.22 Jérémie 52.17-52.19 2 Rois 25.13-25.15
18 Na baadhi ya wanao watakaotoka kwako, utakaowazaa, watawachukulia mbali; nao watakuwa matowashi jumbani mwake mfalme wa Babeli.
2 Chroniques 33.11 2 Rois 24.12 Daniel 1.3 2 Rois 25.6
19 Ndipo Hezekia akamwambia Isaya, Neno la Bwana ulilolinena ni jema. Tena akasema, Je! Sivyo, ikiwapo amani na kweli katika siku zangu?
1 Samuel 3.18 Zacharie 8.19 Luc 2.14 Esther 9.30 Jérémie 33.6
20 Basi mambo yote ya Hezekia yaliyosalia, na ushujaa wake wote, tena alivyolifanya birika na mfereji, akaleta maji ndani ya mji, je! Hayakuandikwa katika kitabu-cha-tarehe cha wafalme wa Yuda?
Néhémie 3.16 2 Chroniques 32.32 2 Chroniques 32.30 Esaïe 22.9-22.11 2 Rois 8.23
21 Hezekia akalala na baba zake; na Manase mwanawe akatawala mahali pake.
2 Chroniques 32.33 2 Rois 21.18 1 Rois 14.31 1 Rois 11.43 2 Chroniques 26.23

Cette Bible est dans le domaine public.