Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Rois 11
Bible en Swahili de l’est


Règne d’Athalie sur Juda

1 Na Athalia, mama yake Ahazia, alipoona ya kuwa mwanawe amekufa, akainuka, akawaharibu wazao wote wa kifalme.
2 Rois 8.26 2 Chroniques 22.10-22.12 2 Chroniques 24.7 Matthieu 21.38-21.39 Jérémie 41.1
2 Ila Yehosheba, binti wa mfalme Yehoramu, umbu lake Ahazia ,akamtwaa Yoashi mwana wa Ahazia ,akamwiba miongoni mwa hao wana wa mfalme waliouawa ,yeye na mlezi wake ,na kuwatia katika chumba cha kulala;wakamficha usoni pa Athalia,basi kwa hiyo hakuuawa.
2 Rois 8.16 Proverbes 21.30 Jérémie 33.21 Esaïe 65.8-65.9 Jérémie 35.2
3 Alikuwako pamoja naye, amefichwa nyumbani mwa Bwana, miaka sita. Naye Athalia akaitawala nchi.
2 Chroniques 22.12 Malachie 3.15 Psaumes 12.8
4 Hata mwaka wa saba Yehoyada akatuma, na kuwaleta wakuu wa mamia, wa Wakari, na wa walinzi, akawaleta kwake ndani ya nyumba ya Bwana; akapatana nao, akawaapisha nyumbani mwa Bwana, akawaonyesha huyo mwana wa mfalme.
2 Rois 11.19 2 Rois 11.9 2 Rois 11.17 2 Chroniques 15.12 2 Chroniques 34.31-34.32
5 Akawaamuru, akasema, Hili ndilo neno mtakalolifanya; theluthi yenu, mtakaoingia siku ya sabato, mtayalinda malinzi ya nyumba ya mfalme;
1 Chroniques 9.25 1 Chroniques 24.3-24.6 2 Rois 16.18 1 Rois 10.5 Ezéchiel 46.2-46.3
6 na theluthi mtakuwapo mlangoni pa Suri; na theluthi langoni nyuma ya walinzi; hivyo mtayalinda malinzi ya nyumba, kuzuia watu wasiingie.
2 Chroniques 23.4-23.5 1 Chroniques 26.13-26.19
7 Na sehemu mbili zenu, yaani, wote watokao siku ya sabato, mtayalinda malinzi ya nyumba ya Bwana kumzunguka mfalme.
2 Chroniques 23.6 2 Rois 11.5
8 Mtamzunguka mfalme pande zote, kila mtu mwenye silaha zake mkononi; naye awaye yote aingiaye ndani ya safu auawe; mkafuatane na mfalme, akitoka na akiingia.
1 Rois 2.28-2.31 2 Rois 11.15 2 Chroniques 23.7 Exode 21.14 Nombres 27.17
9 Nao wakuu wa mamia wakafanya sawasawa na yote aliyowaamuru Yehoyada kuhani; wakawatwaa kila mtu watu wake, hao watakaoingia sabato, nao watakaotoka sabato, wakaja kwa Yehoyada kuhani.
2 Chroniques 23.8 2 Rois 11.4 1 Chroniques 26.26
10 Naye yule kuhani akawapa wakuu wa mamia mikuki na ngao zilizokuwa za mfalme Daudi, zilizokuwamo nyumbani mwa Bwana.
2 Samuel 8.7 1 Chroniques 18.7 1 Samuel 21.9 2 Chroniques 23.9-23.10 2 Chroniques 5.1
11 Walinzi wakasimama, kila mtu na silaha zake mkononi, kutoka pembe ya kuume ya nyumba mpaka pembe ya kushoto ya nyumba, kando ya madhabahu na nyumba, wakimzunguka mfalme pande zote.
2 Rois 11.10 Luc 11.51 Joël 2.17 Exode 40.6 Matthieu 23.35
12 Ndipo akamleta nje mwana wa mfalme, akamvika taji, na kumpa ushuhuda; wakamfanya mfalme, wakamtia mafuta; wakapiga makofi, wakasema, mfalme na aishi.
Exode 25.16 1 Samuel 10.24 Exode 31.18 1 Rois 1.39 2 Samuel 1.10
13 Na Athalia alipoisikia sauti ya walinzi na ya watu, aliingia kwa watu nyumbani kwa Bwana;
2 Chroniques 23.12-23.15
14 akatazama, na tazama, mfalme amesimama karibu na nguzo kama ilivyokuwa desturi, nao wakuu na wapiga baragumu karibu na mfalme; na watu wote wa nchi wakafurahi, wakapiga baragumu. Ndipo Athalia akararua mavazi yake, akalia, Fitina! Fitina!
2 Rois 23.3 2 Chroniques 34.31 2 Rois 9.23 1 Rois 1.39-1.40 Apocalypse 19.1-19.7
15 Naye Yehoyada kuhani akawaamuru wakuu wa mamia, majemadari wa jeshi, akawaambia, Mtoeni kati ya safu; naye ye yote amfuataye mwueni kwa upanga. Kwani kuhani akasema, Asiuawe nyumbani mwa Bwana.
2 Rois 11.4 2 Chroniques 23.14 2 Chroniques 23.9 Ezéchiel 9.7 2 Rois 11.9-11.10
16 Basi wakampisha njia; akaenda kwa njia ya kuingia kwa farasi nyumbani mwa mfalme; akauawa huko.
Genèse 9.6 Jacques 2.13 Matthieu 7.2 Juges 1.7 Apocalypse 16.5-16.7
17 Kisha, Yehoyada akafanya mapatano kati ya Bwana na mfalme na watu, ili wawe watu wa Bwana; tena kati ya mfalme na watu.
2 Samuel 5.3 2 Chroniques 34.31 Josué 24.25 2 Chroniques 15.12-15.14 2 Chroniques 29.10
18 Watu wote wa nchi wakaiendea nyumba ya Baali, wakaiangusha; madhabahu zake na sanamu zake wakazivunja-vunja kabisa, na Matani kuhani wa Baali wakamwua mbele ya madhabahu. Na Yehoyada kuhani akaweka maakida juu ya nyumba ya Bwana.
Deutéronome 12.3 2 Rois 18.4 1 Rois 18.40 2 Rois 10.26 Deutéronome 13.5
19 Akawatwaa wakuu wa mamia, na Wakari, na walinzi, na watu wote wa nchi; wakamleta mfalme kushuka nyumbani mwa Bwana, wakaja kwa njia ya mlango wa walinzi mpaka nyumba ya mfalme. Naye akakaa katika kiti cha enzi cha wafalme.
Matthieu 25.31 Jérémie 22.30 2 Chroniques 23.5 1 Rois 1.13 Matthieu 19.28
20 Basi watu wote wa nchi wakafurahi, na mji ukatulia. Naye Athalia wakamwua kwa upanga karibu na nyumba ya mfalme.
Proverbes 11.10 Proverbes 29.2 2 Rois 11.14 2 Chroniques 23.21
21 Yoashi alikuwa na umri wa miaka saba alipoanza kutawala.
2 Chroniques 24.1-24.14 2 Rois 22.1 2 Rois 11.4

Cette Bible est dans le domaine public.