Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Samuel 21.7
Bible en Swahili de l’est


Vengeance des Gabaonites

1 Kulikuwa na njaa siku za Daudi muda wa miaka mitatu, mwaka kwa mwaka; naye Daudi akautafuta uso wa Bwana. Bwana akasema, Ni kwa ajili ya Sauli, na kwa nyumba yake yenye damu, kwa kuwa aliwaua hao Wagibeoni.
Genèse 12.10 Nombres 27.21 Genèse 26.1 Job 5.8-5.10 1 Samuel 23.2
2 Ndipo mfalme akawaita Wagibeoni akawaambia; (basi Wagibeoni si wa wana wa Israeli, ila ni wa masalio ya Waamori; na wana wa Israeli walikuwa wamewaapia; lakini Sauli akatafuta kuwaua katika juhudi yake kwa ajili ya wana wa Israeli na Yuda;)
Luc 9.54-9.55 Jean 16.2 2 Rois 10.16 Galates 4.17 1 Samuel 14.44
3 basi Daudi akawaambia hao Wagibeoni, Niwatendee nini? Na kwa tendo gani nifanye upatanisho, mpate kuubariki urithi wa Bwana?
2 Samuel 20.19 1 Samuel 26.19 Hébreux 9.22 Hébreux 10.4-10.12 Michée 6.6-6.7
4 Na hao Wagibeoni wakamwambia, Si jambo la fedha wala dhahabu lililo kati ya sisi na Sauli, au nyumba yake; wala si juu yetu kumwua mtu ye yote katika Israeli. Akasema Mtakayoyanena, ndiyo nitakayowatendea ninyi.
Psaumes 49.6-49.8 1 Pierre 1.18-1.19
5 Wakamwambia mfalme, Yule mtu aliyetupoteza, na kutufanyia shauri la kutuharibu, tusikae katika mipaka yo yote ya Israeli,
2 Samuel 21.1 Esther 9.24-9.25 Daniel 9.26 Matthieu 7.2
6 basi, na tutolewe watu saba katika wanawe, nasi tutawatundika mbele za Bwana katika Gibeoni, katika mlima wa Bwana. Mfalme akasema, Nitawatoa.
1 Samuel 10.24 Nombres 25.4-25.5 1 Samuel 10.26 1 Samuel 11.4 Josué 10.26
7 Lakini mfalme akamwachilia Mefiboshethi, mwana wa Yonathani, mwana wa Sauli, kwa ajili ya kiapo cha Bwana kilichokuwa kati yao, yaani, kati ya Daudi na Yonathani, mwana wa Sauli.
1 Samuel 20.15 1 Samuel 18.3 1 Samuel 20.8 2 Samuel 4.4 1 Samuel 23.18
8 Ila mfalme akawatwaa hao wana wawili wa Rispa, binti Aya, aliomzalia Sauli, Armoni na Mefiboshethi; na wana watano wa Merabu binti Sauli, aliomzalia Adrieli, mwana wa Barzilai, Mmeholathi;
2 Samuel 3.7 1 Samuel 18.19
9 akawatia mikononi mwa Wagibeoni, nao wakawatundika mlimani mbele za Bwana, nao wakaangamia wote saba pamoja; wakauawa siku za mavuno, za kwanza, mwanzo wa mavuno ya shayiri.
Ruth 1.22 2 Rois 24.3-24.4 1 Samuel 15.33 2 Samuel 21.6 Exode 20.5
10 Naye Rispa, binti Aya, akatwaa nguo ya magunia akajitandikia mwambani, tangu mwanzo wa mavuno hata waliponyeshewa mvua toka mbinguni; wala hakuacha ndege wa angani kukaa juu yao mchana, wala wanyama wa mwitu usiku.
Deutéronome 21.23 2 Samuel 3.7 1 Rois 18.41-18.45 Jérémie 14.22 Genèse 40.19
11 Kisha akaambiwa Daudi hayo aliyoyafanya huyo Rispa binti Aya, suria wa Sauli.
2 Samuel 2.4 Ruth 2.11-2.12
12 Akaenda Daudi, akaitwaa mifupa ya Sauli na mifupa ya Yonathani mwanawe mikononi mwa watu wa Yabesh-gileadi; waliyoiiba katika njia ya Bethshani, hapo Wafilisti walipowatungika, katika siku hiyo waliyomwua Sauli huko Gilboa;
Josué 17.11 1 Samuel 31.10-31.13 2 Samuel 1.21 1 Samuel 31.1 1 Chroniques 10.1
13 naye akaileta toka huko hiyo mifupa ya Sauli, na mifupa ya Yonathani mwanawe; nao wakaizoa mifupa yao waliotundikwa.
14 Kisha wakaizika mifupa ya Sauli na ya Yonathani mwanawe katika nchi ya Benyamini, huko Zela, kaburini mwa Kishi babaye; wakafanya yote aliyoyaamuru mfalme. Na baadaye Mungu aliiridhia hiyo nchi.
2 Samuel 24.25 Josué 18.28 Josué 7.26 Nombres 25.13 Jonas 1.15

Derniers exploits contre les Philistins

15 Basi kulikuwa na vita tena kati ya Wafilisti na Israeli; Daudi akashuka mpaka Gobu, na watumishi wake pamoja naye, akapigana na Wafilisti; naye Daudi akaishiwa na nguvu.
2 Samuel 5.22 2 Samuel 5.17 1 Chroniques 20.4 Jérémie 9.23-9.24 Esaïe 40.28-40.30
16 Naye Ishi-benobu, aliyekuwa mmojawapo wa Warefai, ambaye uzito wa mkuki wake ulikuwa shekeli mia tatu za shaba kwa uzani ,naye amejifungia upanga mpya,alijaribu kumwua Daudi.
2 Samuel 21.18 2 Samuel 21.20 Deutéronome 1.28 2 Samuel 5.18 Deutéronome 9.2
17 Lakini Abishai, mwana wa Seruya, akamsaidia, akampiga Mfilisti, akamwua. Ndipo watu wa Daudi wakamwapia, wakasema, Wewe hutatoka tena pamoja nasi kwenda vitani, usije ukaizima taa ya Israeli.
1 Rois 11.36 2 Samuel 18.3 Psaumes 132.17 1 Rois 15.4 2 Samuel 20.6-20.10
18 Ikawa baada ya hayo, kulikuwa na vita tena na Wafilisti huko Gobu; ndipo Sibekai, Mhushathi, alipomwua Safu, aliyekuwa mmojawapo wa Warefai.
1 Chroniques 11.29 2 Samuel 21.20 1 Chroniques 27.11 2 Samuel 21.16 2 Samuel 21.22
19 Kulikuwa na vita tena na Wafilisti huko Gobu; na Elhanani, mwana wa Yairi, Mbethlehemi, alimwua Goliathi, Mgiti, ambaye mti wa mkuki wake ulikuwa kama mti wa mfumaji.
1 Chroniques 20.5 1 Samuel 17.4-17.11 1 Chroniques 11.26
20 Kulikuwa na vita tena huko Gathi; ambako kulikuwa na mtu mrefu sana, mwenye vidole sita katika kila mkono, na vidole sita katika kila mguu, jumla yake ishirini na vinne; yeye naye alizaliwa kwa Mrefai.
2 Samuel 21.16 2 Samuel 21.18 1 Chroniques 20.6
21 Naye huyo alipowatukana Israeli, ndipo Yonathani, mwana wa Shama, nduguye Daudi, akamwua.
1 Samuel 17.25-17.26 1 Samuel 16.9 1 Samuel 17.10 1 Samuel 17.36 1 Samuel 17.3
22 Hao wanne walizaliwa kwake huyo Mrefai wa Gathi; wakaanguka kwa mkono wa Daudi, na kwa mikono ya watumishi wake.
1 Chroniques 20.8 Psaumes 108.13 Jérémie 9.23 Psaumes 118.15 Ecclésiaste 9.11

Cette Bible est dans le domaine public.