Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Samuel 21.3
Bible en Swahili de l’est


1 Kulikuwa na njaa siku za Daudi muda wa miaka mitatu, mwaka kwa mwaka; naye Daudi akautafuta uso wa Bwana. Bwana akasema, Ni kwa ajili ya Sauli, na kwa nyumba yake yenye damu, kwa kuwa aliwaua hao Wagibeoni.Genèse 12.10 Nombres 27.21 Genèse 26.1 1 Rois 18.2 1 Samuel 22.17-22.19
2 Ndipo mfalme akawaita Wagibeoni akawaambia; (basi Wagibeoni si wa wana wa Israeli, ila ni wa masalio ya Waamori; na wana wa Israeli walikuwa wamewaapia; lakini Sauli akatafuta kuwaua katika juhudi yake kwa ajili ya wana wa Israeli na Yuda;)Galates 4.17 1 Samuel 14.44 Deutéronome 7.16 Genèse 15.16 Josué 9.3-9.21
3 basi Daudi akawaambia hao Wagibeoni, Niwatendee nini? Na kwa tendo gani nifanye upatanisho, mpate kuubariki urithi wa Bwana?2 Samuel 20.19 1 Samuel 26.19 Hébreux 10.4-10.12 Michée 6.6-6.7 1 Samuel 2.25
4 Na hao Wagibeoni wakamwambia, Si jambo la fedha wala dhahabu lililo kati ya sisi na Sauli, au nyumba yake; wala si juu yetu kumwua mtu ye yote katika Israeli. Akasema Mtakayoyanena, ndiyo nitakayowatendea ninyi.Psaumes 49.6-49.8 1 Pierre 1.18-1.19
5 Wakamwambia mfalme, Yule mtu aliyetupoteza, na kutufanyia shauri la kutuharibu, tusikae katika mipaka yo yote ya Israeli,2 Samuel 21.1 Matthieu 7.2 Esther 9.24-9.25 Daniel 9.26
6 basi, na tutolewe watu saba katika wanawe, nasi tutawatundika mbele za Bwana katika Gibeoni, katika mlima wa Bwana. Mfalme akasema, Nitawatoa.1 Samuel 10.24 1 Samuel 11.4 Nombres 25.4-25.5 1 Samuel 10.26 2 Samuel 17.23
7 Lakini mfalme akamwachilia Mefiboshethi, mwana wa Yonathani, mwana wa Sauli, kwa ajili ya kiapo cha Bwana kilichokuwa kati yao, yaani, kati ya Daudi na Yonathani, mwana wa Sauli.1 Samuel 18.3 1 Samuel 20.8 2 Samuel 4.4 1 Samuel 23.18 1 Samuel 20.15
8 Ila mfalme akawatwaa hao wana wawili wa Rispa, binti Aya, aliomzalia Sauli, Armoni na Mefiboshethi; na wana watano wa Merabu binti Sauli, aliomzalia Adrieli, mwana wa Barzilai, Mmeholathi;2 Samuel 3.7 1 Samuel 18.19
9 akawatia mikononi mwa Wagibeoni, nao wakawatundika mlimani mbele za Bwana, nao wakaangamia wote saba pamoja; wakauawa siku za mavuno, za kwanza, mwanzo wa mavuno ya shayiri.Ruth 1.22 Exode 20.5 Nombres 35.31-35.34 2 Samuel 6.21 Deutéronome 21.1-21.9
10 Naye Rispa, binti Aya, akatwaa nguo ya magunia akajitandikia mwambani, tangu mwanzo wa mavuno hata waliponyeshewa mvua toka mbinguni; wala hakuacha ndege wa angani kukaa juu yao mchana, wala wanyama wa mwitu usiku.Deutéronome 21.23 2 Samuel 3.7 1 Rois 21.27 Ezéchiel 39.4 Joël 1.18
11 Kisha akaambiwa Daudi hayo aliyoyafanya huyo Rispa binti Aya, suria wa Sauli.2 Samuel 2.4 Ruth 2.11-2.12
12 Akaenda Daudi, akaitwaa mifupa ya Sauli na mifupa ya Yonathani mwanawe mikononi mwa watu wa Yabesh-gileadi; waliyoiiba katika njia ya Bethshani, hapo Wafilisti walipowatungika, katika siku hiyo waliyomwua Sauli huko Gilboa;1 Samuel 31.10-31.13 Josué 17.11 1 Samuel 31.1 1 Chroniques 10.1 1 Samuel 28.4
13 naye akaileta toka huko hiyo mifupa ya Sauli, na mifupa ya Yonathani mwanawe; nao wakaizoa mifupa yao waliotundikwa. 14 Kisha wakaizika mifupa ya Sauli na ya Yonathani mwanawe katika nchi ya Benyamini, huko Zela, kaburini mwa Kishi babaye; wakafanya yote aliyoyaamuru mfalme. Na baadaye Mungu aliiridhia hiyo nchi.Josué 18.28 2 Samuel 24.25 Josué 7.26 Amos 7.1-7.6 2 Samuel 3.32
15 Basi kulikuwa na vita tena kati ya Wafilisti na Israeli; Daudi akashuka mpaka Gobu, na watumishi wake pamoja naye, akapigana na Wafilisti; naye Daudi akaishiwa na nguvu.2 Samuel 5.22 2 Samuel 5.17 2 Samuel 5.25 Psaumes 71.9 Ecclésiaste 12.3
16 Naye Ishi-benobu, aliyekuwa mmojawapo wa Warefai, ambaye uzito wa mkuki wake ulikuwa shekeli mia tatu za shaba kwa uzani ,naye amejifungia upanga mpya,alijaribu kumwua Daudi.2 Samuel 21.18 2 Samuel 21.20 Deutéronome 2.21 2 Samuel 21.22 Nombres 13.32-13.33
17 Lakini Abishai, mwana wa Seruya, akamsaidia, akampiga Mfilisti, akamwua. Ndipo watu wa Daudi wakamwapia, wakasema, Wewe hutatoka tena pamoja nasi kwenda vitani, usije ukaizima taa ya Israeli.1 Rois 11.36 2 Samuel 18.3 1 Rois 15.4 2 Samuel 20.6-20.10 Psaumes 132.17
18 Ikawa baada ya hayo, kulikuwa na vita tena na Wafilisti huko Gobu; ndipo Sibekai, Mhushathi, alipomwua Safu, aliyekuwa mmojawapo wa Warefai.1 Chroniques 11.29 2 Samuel 21.20 1 Chroniques 27.11 2 Samuel 21.16 1 Chroniques 20.4-20.8
19 Kulikuwa na vita tena na Wafilisti huko Gobu; na Elhanani, mwana wa Yairi, Mbethlehemi, alimwua Goliathi, Mgiti, ambaye mti wa mkuki wake ulikuwa kama mti wa mfumaji.1 Chroniques 20.5 1 Samuel 17.4-17.11 1 Chroniques 11.26
20 Kulikuwa na vita tena huko Gathi; ambako kulikuwa na mtu mrefu sana, mwenye vidole sita katika kila mkono, na vidole sita katika kila mguu, jumla yake ishirini na vinne; yeye naye alizaliwa kwa Mrefai.2 Samuel 21.16 2 Samuel 21.18 1 Chroniques 20.6
21 Naye huyo alipowatukana Israeli, ndipo Yonathani, mwana wa Shama, nduguye Daudi, akamwua.1 Samuel 17.10 1 Samuel 17.36 1 Samuel 17.25-17.26 1 Samuel 16.9 1 Chroniques 27.32
22 Hao wanne walizaliwa kwake huyo Mrefai wa Gathi; wakaanguka kwa mkono wa Daudi, na kwa mikono ya watumishi wake.1 Chroniques 20.8 Ecclésiaste 9.11 Josué 14.12 Psaumes 60.12 Romains 8.31

Cette Bible est dans le domaine public.