Accueil  /  Bible  /  Bible en Swahili de l’est  /  Psaumes 36.7

La Bible Bible en Swahili de l’est

Psaumes 36

Un clic sur un verset envoie vers le comparateur de versions.

Chapitre 35 Chapitre 37

Le méchant et sa punition

1 Kuasi kwake yule mwovu hunena moyoni mwake, Hakuna hofu ya Mungu mbele ya macho yake.
2 Kwa maana hujipendekeza machoni pake Kuwa upotovu wake hautaonekana na kuchukiwa.
3 Maneno ya kinywa chake ni uovu na hila, Ameacha kuwa na akili na kutenda mema.
4 Huwaza maovu kitandani pake, Hujiweka katika njia mbaya; ubaya hauchukii.
5 Ee Bwana, fadhili zako zafika hata mbinguni, Uaminifu wako hata mawinguni.
6 Haki yako ni kama milima ya Mungu, Hukumu zako ni vilindi vikuu, Ee Bwana, unawaokoa wanadamu na wanyama.
7 Ee Mungu, jinsi zilivyo na thamani fadhili zako! Wanadamu huukimbilia uvuli wa mbawa zako.
8 Watashibishwa kwa unono wa nyumba yako, Nawe utawanywesha mto wa furaha zako.
9 Maana kwako Wewe iko chemchemi ya uzima, Katika nuru yako tutaona nuru.
10 Uwadumishie wakujuao fadhili zako, Na wanyofu wa moyo uaminifu wako.
11 Mguu wa kiburi usinikaribie, Wala mkono wa wasio haki usinifukuze.
12 Huko ndiko walikoanguka wafanyao maovu; Wameangushwa chini wasiweze kusimama.

Vous êtes actuellement sur une version optimisée pour mobile, si vous souhaitez basculer sur la version complète suivez le lien suivant : Psaumes 36.7 (Lemaîtstre de Sacy)

Cette Bible est dans le domaine public.