Accueil  /  Bible  /  Bible en Swahili de l’est  /  Psaumes 112

La Bible Bible en Swahili de l’est

Psaumes 112

Un clic sur un verset envoie vers le comparateur de versions.

Chapitre 111 Chapitre 113

Le bonheur du juste

1 Haleluya. Heri mtu yule amchaye Bwana, Apendezwaye sana na maagizo yake.
2 Wazao wake watakuwa hodari duniani; Kizazi cha wenye adili kitabarikiwa.
3 Nyumbani mwake mna utajiri na mali, Na haki yake yakaa milele.
4 Nuru huwazukia wenye adili gizani; Ana fadhili na huruma na haki.
5 Heri atendaye fadhili na kukopesha; Atengenezaye mambo yake kwa haki.
6 Kwa maana hataondoshwa kamwe; Mwenye haki atakumbukwa milele.
7 Hataogopa habari mbaya; Moyo wake u imara ukimtumaini Bwana.
8 Moyo wake umethibitika hataogopa, Hata awaone watesi wake wameshindwa.
9 Amekirimu, na kuwapa maskini, Haki yake yakaa milele, Pembe yake itatukuzwa kwa utukufu.
10 Asiye haki ataona na kusikitika, Atasaga meno yake na kuyeyuka, Tamaa ya wasio haki itapotea.


Vous êtes actuellement sur une version optimisée pour mobile, si vous souhaitez basculer sur la version complète suivez le lien suivant : Psaumes 112.1 (Lemaîtstre de Sacy)

Cette Bible est dans le domaine public.