Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Juges 16.30
Bible en Swahili de l’est


Samson prisonnier des Philistins

1 Samsoni akaenda Gaza, akaona huko mwanamke kahaba, akaingia kwake.
Josué 15.47 Genèse 10.19 Genèse 38.16-38.18 Esdras 9.1-9.2
2 Watu wa Gaza wakaambiwa, ya kwamba, huyo Samsoni amekuja huku. Wakamzingira, wakamvizia usiku kucha, penye lango la mji, wakanyamaza kimya usiku kucha, wakisema, Na tungoje mpaka mapambazuko, ndipo tutamwua.
Psaumes 118.10-118.12 1 Samuel 23.26 Actes 9.24 Juges 15.18 Matthieu 21.38
3 Basi Samsoni akalala hata usiku wa manane, akaondoka katikati ya usiku, akaishika milango ya lango la mji, na miimo yake miwili, akaing’oa pamoja na komeo lake, akajitwika mabegani, akavichukua hata kilele cha mlima ule unaokabili Hebroni.
Esaïe 63.1-63.5 Psaumes 107.16 Michée 2.13 Actes 2.24
4 Ikawa baada ya hayo akampenda mwanamke mmoja katika bonde la Soreki, jina lake akiitwa Delila.
Proverbes 22.14 Proverbes 26.11 1 Rois 11.1 Néhémie 13.26 Proverbes 23.27
5 Nao wakuu wa Wafilisti wakamwendea, wakamwambia, Mbembeleze, upate kujua asili ya nguvu zake nyingi, na jinsi tutakavyoweza kumshinda, tupate kumfunga na kumtesa; nasi tutakupa kila mtu fedha elfu na mia moja.
Juges 14.15 Josué 13.3 Juges 17.2 Proverbes 2.16-2.19 Matthieu 26.15
6 Delila akamwambia Samsoni, Tafadhali uniambie asili ya nguvu zako nyingi, na jinsi uwezavyo kufungwa, ili uteswe.
Proverbes 6.26 Proverbes 22.14 Jérémie 9.2-9.5 Proverbes 26.28 Michée 7.2
7 Samsoni akamwambia, Wakinifunga kwa kamba mbichi saba ambazo hazijakauka bado, hapo ndipo nitakuwa dhaifu, nitakuwa kama wanadamu wenzangu.
Proverbes 12.19 Proverbes 17.7 1 Samuel 27.10 Galates 6.7 1 Samuel 21.2-21.3
8 Ndipo wakuu wa Wafilisti wakamletea kamba mbichi saba zisizokauka, naye akamfunga nazo.
Ecclésiaste 7.26
9 Na yule mwanamke alikuwa na watu katika chumba cha ndani, wakimwotea. Basi akamwambia Samsoni, Wafilisti wanakujia. Ndipo akazikata zile kamba kama vile uzi wa pamba ukatwavyo ukiguswa na moto. Basi hiyo asili ya nguvu zake haikujulikana.
Psaumes 58.9
10 Delila akamwambia Samsoni, Tazama, umenidhihaki, na kuniambia uongo; sasa tafadhali, niambie, waweza kufungwa kwa kitu gani?
Juges 16.13 Proverbes 23.7-23.8 Luc 22.48 Juges 16.15-16.17 Proverbes 24.28
11 Akamwambia Wakinifunga tu kwa kamba mpya ambazo mtu hakufanya kazi nazo, hapo ndipo nitakuwa dhaifu, nitakuwa kama wanadamu wenzangu.
Proverbes 13.5 Juges 15.13 Proverbes 29.25 Proverbes 13.3 Ephésiens 4.25
12 Basi Delila akatwaa kamba mpya akamfunga nazo, akamwambia, Wafilisti wanakujia, Samsoni. Na wale wenye kuotea walikuwa katika chumba cha ndani. Naye akazikata, akazitupa kutoka mikononi mwake kama uzi.
13 Delila akamwambia Samsoni, Hata sasa umenidhihaki, umeniambia maneno ya uongo; niambie sasa, waweza kufungwa kwa kitu gani? Akamwambia, Ukivifuma hivi vishungi saba vya nywele za kichwa changu katika mtande wa nguo.
14 Basi akazifunga kwa msumari, akamwambia Samsoni, Wafilisti wanakujia. Naye akaamka usingizini, akaung’oa ule msumari, na ule mtande.
Psaumes 106.43 Esdras 9.13-9.14
15 Mwanamke akamwambia, Wawezaje kusema, Nakupenda; na moyo wako haupo pamoja nami? Umenidhihaki mara hizi tatu, wala hukuniambia asili ya nguvu zako nyingi.
Juges 14.16 Jean 15.10 2 Samuel 16.17 Proverbes 2.16 1 Jean 2.15-2.16
16 Ikawa, kwa vile alivyomsumbua kwa maneno yake kila siku, na kumwudhi, roho yake ikadhikika hata kufa.
Luc 18.5 Luc 11.8 Job 21.4 Proverbes 7.26-7.27 Jonas 4.9
17 Ndipo alipomwambia yote yaliyokuwa moyoni mwake, akamwambia, Wembe haukupita juu ya kichwa changu kamwe; maana mimi nimekuwa Mnadhiri wa Mungu, tangu tumboni mwa mama yangu; nikinyolewa, ndipo nguvu zangu zitanitoka, nami nitakuwa dhaifu, nitakuwa kama wanadamu wenzangu.
Juges 13.5 Nombres 6.5 Michée 7.5 Nombres 6.2 Actes 18.18
18 Delila alipoona ya kuwa amemwambia yote yaliyokuwa moyoni mwake, akatuma mtu akawaita wakuu wa Wafilisti, akisema, Njoni huku mara hii tu, maana ameniambia yote aliyo nayo moyoni mwake. Ndipo wakuu wa Wafilisti wakamwendea wakachukua ile fedha mikononi mwao.
Juges 16.5 Psaumes 62.9 Ephésiens 5.5 Jérémie 9.4-9.6 Nombres 22.7
19 Naye akamlaza usingizi magotini pake. Kisha akamwita mtu akavinyoa vile vishungi saba vya nywele za kichwa chake; akaanza kumsumbua, nguvu zake zikamtoka.
Proverbes 7.26-7.27 Ecclésiaste 7.26 Proverbes 23.33-23.34 Proverbes 7.21-7.23
20 Kisha akasema, Samsoni, Wafilisti wanakujia. Akaamka katika usingizi wake, akasema, Nitakwenda nje kama siku nyingine, na kujinyosha. Lakini hakujua ya kuwa Bwana amemwacha.
Nombres 14.42-14.43 1 Samuel 16.14 Josué 7.12 1 Samuel 18.12 2 Chroniques 15.2
21 Wafilisti wakamkamata, wakamng’oa macho; wakatelemka naye mpaka Gaza, wakamfunga kwa vifungo vya shaba; naye alikuwa akisaga ngano katika gereza.
Exode 11.5 Matthieu 24.41 Esaïe 47.2 Proverbes 5.22 Psaumes 107.10-107.12

Mort de Samson

22 Lakini zile nywele za kichwa chake zikaanza kukua tena baada ya kunyolewa kwake.
Psaumes 107.13-107.14 Lévitique 26.44 Psaumes 106.44-106.45 Deutéronome 32.36
23 Kisha wakuu wa Wafilisti wakakusanyika ili kumtolea sadaka Dagoni mungu wao, na kufurahi; maana walisema, Mungu wetu amemtia Samsoni adui wetu mikononi mwetu.
1 Samuel 5.2-5.5 Michée 4.5 1 Corinthiens 10.20 Romains 1.23-1.25 Job 30.9-30.10
24 Na hao watu walipomwona wakamhimidi mungu wao, maana walisema, Mungu wetu amemtia mikononi mwetu huyu adui wetu, aliyeiharibu nchi yetu na kuwaua watu wengi miongoni mwetu.
Daniel 5.4 Esaïe 37.20 Habakuk 1.16 Juges 15.16 1 Samuel 31.9
25 Ikawa mioyo yao iliposhangilia, wakasema, Mwiteni Samsoni, ili atufanyie michezo. Basi wakamwita Samsoni atoke gerezani, akacheze mbele yao wakamweka katikati ya nguzo mbili.
2 Samuel 13.28 Juges 9.27 Juges 19.6 Daniel 5.2-5.3 Matthieu 26.67-26.68
26 Samsoni akamwambia yule kijana aliyemshika mkono, Niache nizipapase nguzo ambazo nyumba hii inazikalia, nipate kuzitegemea.
27 Basi nyumba ile ilikuwa imejaa watu waume kwa wake; na wakuu wote wa Wafilisti walikuwamo humo, na juu ya dari palikuwa na watu elfu tatu waume kwa wake waliokuwa wakitazama, wakati Samsoni alipocheza.
Deutéronome 22.8 Josué 2.8 2 Samuel 11.2 Juges 9.51
28 Samsoni akamwita Bwana, akasema, Ee Bwana MUNGU, unikumbuke, nakuomba, ukanitie nguvu, nakuomba, mara hii tu, Ee Mungu, ili nipate kujilipiza kisasi juu ya Wafilisti kwa ajili ya macho yangu mawili.
Jérémie 15.15 Psaumes 74.18-74.23 2 Chroniques 20.12 Juges 15.18 2 Timothée 4.14
29 Kisha Samsoni akazishika nguzo mbili za katikati ambazo nyumba ile ilikaa juu yake, akazitegemea, moja kwa mkono wake wa kuume na moja kwa mkono wake wa kushoto.
30 Samsoni akasema; Na nife pamoja na hawa Wafilisti. Akainama kwa nguvu zake zote; ile nyumba ikawaangukia hao wakuu, na watu wote waliokuwa ndani yake. Basi wale watu aliowaua wakati wa kufa kwake walikuwa wengi kuliko wale aliowaua wakati wa uhai wake.
Matthieu 16.25 1 Thessaloniciens 5.2 Juges 14.19 Juges 15.8 Ecclésiaste 9.12
31 Ndipo ndugu zake, na watu wote wa nyumba ya baba yake wakatelemka, wakamtwaa wakamchukua, wakamzika kati ya Sora na Eshtaoli, katika kiwanja cha kuzikia cha Manoa baba yake. Naye alikuwa mwamuzi wa Israeli muda wa miaka ishirini.
Juges 15.20 Juges 13.2 Juges 13.25 Josué 19.41 Jean 19.39-19.42

Cette Bible est dans le domaine public.