Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Juges 10.11
Bible en Swahili de l’est


Thola et Jaïr juges en Israël

1 Baada yake Abimeleki, akainuka Tola mwana wa Pua, mwana wa Dodo, mtu wa Isakari, kuwaokoa Israeli; naye alikuwa akikaa Shamiri, katika nchi ya vilima vilima ya Efraimu.
Juges 2.16 Juges 3.9 Josué 15.48
2 Huyo akawa mwamuzi wa Israeli muda wa miaka ishirini na mitatu, akafa, akazikwa katika Shamiri.
3 Baada yake huyo akainuka Yairi, Mgileadi; naye akawa mwamuzi wa Israeli muda wa miaka ishirini na miwili.
Genèse 31.48 Nombres 32.29
4 Huyo alikuwa na wana thelathini waliokuwa wakipanda wana-punda thelathini, nao walikuwa na miji thelathini, ambayo inaitwa Hawoth-yairi hata hivi leo, nayo iko katika nchi ya Gileadi.
Nombres 32.41 Deutéronome 3.14 Juges 12.14 Juges 5.10
5 Yairi akafa, akazikwa huko Kamoni.

Intervention de Jephthé

6 Kisha wana wa Israeli walifanya tena yaliyo maovu mbele za macho ya Bwana, wakawatumikia Mabaali, na Maashtorethi, na miungu ya Shamu, na miungu ya Sidoni, na miungu ya Moabu, na miungu ya wana wa Amoni, na miungu ya Wafilisti; nao wakamwacha Bwana, wala hawakumtumikia yeye.
2 Rois 23.13 1 Rois 11.33 1 Rois 11.5 1 Rois 11.7 Jérémie 2.13
7 Hasira za Bwana ziliwaka juu ya Israeli, akawauza na kuwaua mikononi mwa Wafilisti, na mikononi mwa wana wa Amoni.
Juges 2.14 Psaumes 44.12 Psaumes 74.1 Deutéronome 29.20-29.28 Nahum 1.2
8 Nao wakawasumbua na kuwaonea wana wa Israeli mwaka huo; waliwaonea wana wa Israeli wote waliokuwa ng’ambo ya pili ya Yordani katika nchi ya Waamori, iliyoko huko Gileadi, muda wa miaka kumi na minane.
1 Thessaloniciens 5.3 Esaïe 30.13 Juges 10.5
9 Wana wa Amoni nao wakavuka Yordani ili wapigane na Yuda, na kupigana na Benyamini, na nyumba ya Efraimu; basi hivyo Israeli walikuwa wanasumbuliwa sana.
2 Chroniques 15.5 Juges 3.12-3.13 2 Chroniques 20.1-20.2 Juges 6.3-6.5 Deutéronome 28.65
10 Ndipo wana wa Israeli wakamlilia Bwana, wakisema, Sisi tumekufanyia dhambi, kwa sababu tumemwacha Mungu wetu, na kuyatumikia Mabaali.
1 Samuel 12.10 Juges 3.9 Psaumes 107.19 Psaumes 107.28 Psaumes 106.43-106.44
11 Naye Bwana akawaambia wana wa Israeli, Je! Sikuwaokoa ninyi na hao Wamisri, na Waamori, na wana wa Amoni, na Wafilisti?
Exode 14.30 Nombres 21.21-21.25 Juges 3.31 Psaumes 106.8-106.11 Psaumes 78.51-78.53
12 Hao Wasidoni nao, na Waamaleki, na Wamaoni, waliwaonea, nanyi mlinililia, nami niliwaokoa na mikono yao.
Juges 6.3 Psaumes 106.42-106.43 2 Chroniques 26.6-26.7 Juges 5.19-5.31
13 Lakini mmeniacha mimi, na kuitumikia miungu mingine; basi kwa ajili ya hayo mimi sitawaokoa tena.
Jérémie 2.13 Juges 2.12 Deutéronome 32.15 1 Chroniques 28.9 Jonas 2.8
14 Haya, endeni mkaililie hiyo miungu mliyoichagua; na hiyo iwaokoe wakati wa kusumbuka kwenu.
Deutéronome 32.37-32.38 Jérémie 2.28 Deutéronome 32.26-32.28 1 Rois 18.27-18.28 Proverbes 1.25-1.27
15 Wana wa Israeli wakamwambia Bwana Tumefanya dhambi; utufanyie yote uyaonayo kuwa ni mema; lakini tuokoe, twakusihi, siku hii ya leo, haya tu.
1 Samuel 3.18 2 Samuel 15.26 2 Samuel 24.14 Josué 9.25 Job 33.27
16 Nao wakaiondoa hiyo miungu ya kigeni iliyokuwa kati yao, nao wakamtumikia Bwana; na roho yake ilihuzunika kwa sababu ya msiba wa Israeli.
Esaïe 63.9 Psaumes 106.44-106.45 Ezéchiel 18.30-18.32 Hébreux 4.15 Hébreux 3.10
17 Wakati huo wana wa Amoni walikutana pamoja, wakapanga marago huko Gileadi. Wana wa Israeli nao wakajikusanya wakapanga marago Mispa.
Juges 11.29 Genèse 31.49 Juges 11.11
18 Na hao watu, wakuu wa Gileadi, wakaambiana wao kwa wao, Je! Ni mtu yupi atakayeanza kupigana na wana wa Amoni? Yeye atakuwa ni kichwa juu ya wenyeji wote wa Gileadi.
Juges 11.11 Juges 12.7 Juges 11.5-11.8 1 Samuel 17.25 Esaïe 34.12

Cette Bible est dans le domaine public.