Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Apocalypse 10.9
Bible en Swahili de l’est


Le petit livre

1 Kisha nikaona malaika mwingine mwenye nguvu akishuka kutoka mbinguni, amevikwa wingu; na upinde wa mvua juu ya kichwa chake; na uso wake ulikuwa kama jua, na miguu yake kama nguzo za moto.
Matthieu 17.2 Apocalypse 1.15-1.16 Apocalypse 4.3 Ezéchiel 1.28 Apocalypse 5.2
2 Na katika mkono wake alikuwa na kitabu kidogo kimefunguliwa. Akaweka mguu wake wa kuume juu ya bahari, nao wa kushoto juu ya nchi.
Apocalypse 10.5 Ezéchiel 2.9-2.10 Matthieu 28.18 Proverbes 8.15-8.16 Esaïe 59.19
3 Naye akalia kwa sauti kuu, kama simba angurumavyo. Na alipolia, zile ngurumo saba zikatoa sauti zao.
Amos 1.2 Esaïe 31.4 Joël 3.16 Esaïe 5.29 Jérémie 25.30
4 Hata ngurumo saba zilipotoa sauti zao, nalikuwa tayari kuandika. Nami nalisikia sauti kutoka mbinguni ikisema, Yatie muhuri maneno hayo yaliyonenwa na hizo ngurumo saba, usiyaandike.
Daniel 12.9 Daniel 12.4 Daniel 8.26 Apocalypse 1.11 Apocalypse 22.10
5 Na yule malaika niliyemwona, akisimama juu ya bahari na juu ya nchi, akainua mkono wake wa kuume kuelekea mbinguni,
Daniel 12.7 Deutéronome 32.40 Genèse 22.15-22.16 Actes 14.15 Apocalypse 1.18
6 akaapa kwa yeye aliye hai hata milele na milele, yeye aliyeziumba mbingu na vitu vilivyomo, na nchi na vitu vilivyomo, na bahari na vitu vilivyomo, ya kwamba hapatakuwa na wakati baada ya haya;
Apocalypse 4.11 Apocalypse 4.9 Apocalypse 16.17
7 isipokuwa katika siku za sauti ya malaika wa saba atakapokuwa tayari kupiga baragumu; hapo ndipo siri ya Mungu itakapotimizwa, kama alivyowahubiri watumishi wake hao manabii.
Ephésiens 3.3-3.9 Romains 16.25 Amos 3.7 Actes 3.21 Apocalypse 11.15-11.18
8 Na sauti ile niliyoisikia kutoka mbinguni ilinena nami tena, ikisema, Enenda, ukakitwae kile kitabu kilichofunguliwa katika mkono wa yule malaika, aliyesimama juu ya bahari na juu ya nchi.
Apocalypse 10.4-10.5 Apocalypse 10.2 Esaïe 30.21
9 Nikamwendea malaika yule nikamwambia kwamba anipe kile kitabu kidogo. Akaniambia, Kitwae, ukile, nacho kitakutia uchungu tumboni mwako, bali katika kinywa chako kitakuwa kitamu kama asali.
Ezéchiel 3.1-3.3 Ezéchiel 2.8 Jérémie 15.16 Ezéchiel 3.14 Job 23.12
10 Nikakitwaa kile kitabu kidogo katika mkono wa malaika yule, nikakila; nacho kikawa kitamu kama asali kinywani mwangu, na nilipokwisha kukila tumbo langu likatiwa uchungu.
Ezéchiel 3.3 Psaumes 19.10 Proverbes 16.24 Ezéchiel 2.10 Psaumes 104.34
11 Wakaniambia, Imekupasa kutoa unabii tena juu ya watu na taifa na lugha na wafalme wengi.
Ezéchiel 37.4 Jérémie 25.15-25.30 Jérémie 1.9-1.10 Apocalypse 11.9 Apocalypse 14.6

Cette Bible est dans le domaine public.