Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Hébreux 1.1
Bible en Swahili de l’est


Supériorité de Christ le Fils

Christ supérieur aux anges

1 Mungu, ambaye alisema zamani na baba zetu katika manabii kwa sehemu nyingi na kwa njia nyingi,
2 Pierre 1.20-1.21 Joël 2.28 1 Pierre 1.10-1.12 Nombres 12.6-12.8 Luc 24.27
2 mwisho wa siku hizi amesema na sisi katika Mwana, aliyemweka kuwa mrithi wa yote, tena kwa yeye aliufanya ulimwengu.
1 Corinthiens 8.6 Jean 1.3 Matthieu 28.18 Jean 1.14 Jean 3.16
3 Yeye kwa kuwa ni mng’ao wa utukufu wake na chapa ya nafsi yake, akivichukua vyote kwa amri ya uweza wake, akiisha kufanya utakaso wa dhambi, aliketi mkono wa kuume wa Ukuu huko juu;
2 Corinthiens 4.4 Colossiens 1.15-1.17 Jean 14.9-14.10 Jean 1.14 Hébreux 7.27
4 amefanyika bora kupita malaika, kwa kadiri jina alilolirithi lilivyo tukufu kuliko lao.
Ephésiens 1.21 Philippiens 2.9-2.11 1 Pierre 3.22 2 Thessaloniciens 1.7 Hébreux 2.9
5 Kwa maana alimwambia malaika yupi wakati wo wote, Ndiwe mwanangu, Mimi leo nimekuzaa? Na tena, Mimi nitakuwa kwake baba, Na yeye atakuwa kwangu mwana?
Psaumes 2.7 Actes 13.33 Hébreux 5.5 1 Chroniques 22.10 2 Samuel 7.14
6 Hata tena, amletapo mzaliwa wa kwanza ulimwenguni, asema, Na wamsujudu malaika wote wa Mungu.
Deutéronome 32.43 Psaumes 97.7 Romains 8.29 Colossiens 1.18 1 Jean 4.9
7 Na kwa habari za malaika asema, Afanyaye malaika zake kuwa pepo, Na watumishi wake kuwa miali ya moto.
Psaumes 104.4 Hébreux 1.14 Zacharie 6.5 2 Rois 2.11 Daniel 7.10
8 Lakini kwa habari za Mwana asema, Kiti chako cha enzi,Mungu,ni cha milele na milele; Na fimbo ya ufalme wako ni fimbo ya adili.
Psaumes 45.6-45.7 Jérémie 23.5-23.6 Jean 10.30 Esaïe 9.6-9.7 Tite 2.13-2.14
9 Umependa haki, umechukia maasi; Kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekutia mafuta, Mafuta ya shangwe kupita wenzio.
Esaïe 61.3 Psaumes 45.7 Esaïe 61.1 Amos 5.15 Luc 4.18
10 Na tena, Wewe,Bwana,hapo mwanzo uliitia misingi ya nchi, Na mbingu ni kazi za mikono yako;
Psaumes 102.25-102.27 Genèse 1.1 Psaumes 19.1 Esaïe 42.5 Jean 1.1-1.3
11 Hizo zitaharibika, bali wewe unadumu; Nazo zote zitachakaa kama nguo,
Esaïe 51.6 Esaïe 34.4 Luc 21.33 Apocalypse 2.8 Psaumes 29.10
12 Na kama mavazi utazizinga, nazo zitabadilika; Lakini wewe u yeye yule, Na miaka yako haitakoma.
Psaumes 102.26-102.27 Hébreux 13.8 Exode 3.14 Jacques 1.17 Psaumes 90.4
13 Je! Yuko malaika aliyemwambia wakati wo wote, Uketi mkono wangu wa kuume Hata nitakapoweka adui zako chini ya nyayo zako?
Psaumes 110.1 Matthieu 22.44 Hébreux 1.3 1 Corinthiens 15.25-15.26 Apocalypse 20.15
14 Je! Hao wote si roho watumikao, wakitumwa kuwahudumu wale watakaourithi wokovu?
Psaumes 34.7 Psaumes 103.20-103.21 Luc 16.22 Daniel 3.28 Daniel 6.22

Cette Bible est dans le domaine public.