1 Paulo, mtumwa wa Mungu, na mtume wa Yesu Kristo; kwa ajili ya imani ya wateule wa Mungu, na ujuzi wa kweli ile iletayo utauwa;
Romains 1.1  1 Timothée 6.3  2 Timothée 2.25  Tite 2.11-2.12  2 Timothée 2.23  
 2 katika tumaini la uzima wa milele, ambao Mungu asiyeweza kusema uongo aliuahidi tangu milele;
2 Timothée 1.1  Tite 3.7  2 Timothée 1.9  Tite 2.13  Jude 1.21  
 3 akalifunua neno lake kwa majira yake katika ule ujumbe niliowekewa amana mimi kwa amri ya Mwokozi wetu Mungu;
1 Timothée 1.11  1 Timothée 1.1  Tite 3.4-3.6  Tite 2.10  Ephésiens 1.10  
 4 kwa Tito, mwanangu hasa katika imani tuishirikiyo. Neema na iwe kwako na amani zitokazo kwa Mungu Baba na kwa Kristo Yesu Mwokozi wetu.
Jude 1.3  2 Timothée 1.2  2 Pierre 1.1  2 Corinthiens 2.13  2 Corinthiens 8.23  
 5 Kwa sababu hii nalikuacha Krete, ili uyatengeneze yaliyopunguka, na kuweka wazee katika kila mji kama vile nilivyokuamuru;
Actes 14.23  1 Timothée 1.3  Actes 27.7  2 Timothée 2.2  1 Chroniques 6.32  
 6 ikiwa mtu hakushitakiwa neno, naye ni mume wa mke mmoja, ana watoto waaminio, wasioshitakiwa kuwa ni wafisadi wala wasiotii.
1 Timothée 3.12  1 Timothée 3.2-3.7  Tite 1.6-1.8  Ezéchiel 44.22  Tite 1.10  
 7 Maana imempasa askofu awe mtu asiyeshitakiwa neno ,kwa kuwa ni wakili wa MUNGU;asiwe mtu wa kujipendeza nafsi yake,asiwe mwepesi wa hasira,asiwe mlevi wala mgomvi,asiwe mpenda mapato ya aibu.
Luc 12.42  2 Pierre 2.10  1 Pierre 5.2  Esaïe 28.7  1 Pierre 4.10  
 8 bali awe mkaribishaji, mpenda wema, mwenye kiasi, mwenye haki, mtakatifu, mwenye kudhibiti nafsi yake;
1 Timothée 3.2  1 Rois 5.1  1 Timothée 4.12  Psaumes 16.3  1 Thessaloniciens 2.10  
 9 akilishika lile neno la imani vile vile kama alivyofundishwa, apate kuweza kuwaonya watu kwa mafundisho yenye uzima, na kuwashinda wenye kupinga.1 Timothée 1.10  2 Thessaloniciens 2.15  1 Timothée 6.3  2 Timothée 1.13  1 Timothée 1.15  
 10 Kwa maana kuna wengi wasiotii, wenye maneno yasiyo na maana, wadanganyaji, na hasa wale wa tohara, ambao yapasa wazibwe vinywa vyao.
1 Timothée 1.6  Actes 11.2  Galates 1.6-1.8  Apocalypse 2.14  Galates 4.17-4.21  
 11 Hao wanapindua watu wa nyumba nzima, wakifundisha yasiyowapasa kwa ajili ya mapato ya aibu.
2 Timothée 3.6  1 Timothée 6.5  Tite 3.10  Ezéchiel 16.63  Esaïe 56.10-56.11  
 12 Mtu wa kwao, nabii wao wenyewe, amesema, Wakrete ni waongo siku zote, hayawani wabaya, walafi wavivu.
Actes 17.28  Jude 1.8-1.13  2 Pierre 2.12  1 Timothée 4.2  Actes 2.11  
 13 Ushuhuda huo ni kweli. Kwa sababu hiyo uwakemee kwa ukali, ili wapate kuwa wazima katika imani;
Tite 2.2  2 Corinthiens 13.10  1 Timothée 5.20  Tite 2.15  2 Timothée 4.2  
 14 wasisikilize hadithi za Kiyahudi, wala maagizo ya watu wajiepushao na yaliyo kweli.
Colossiens 2.22  2 Timothée 4.4  Marc 7.7  Esaïe 29.13  Hébreux 12.25  
 15 Vitu vyote ni safi kwa hao walio safi; lakini hakuna kilicho safi kwao walio wanajisi, wasioamini; bali akili zao zimekuwa najisi, na nia zao pia.
Romains 14.20  Romains 14.14  Romains 14.23  1 Corinthiens 10.23  1 Timothée 4.3-4.4  
 16 Wanakiri ya kwamba wanamjua Mungu, bali kwa matendo yao wanamkana; ni wenye machukizo, waasi, wala kwa kila tendo jema hawafai.
1 Jean 2.4  Esaïe 29.13  Ezéchiel 33.31  2 Timothée 3.5-3.8  Jude 1.4