1 Kila mtu na aitii mamlaka iliyo kuu; kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu; na ile iliyopo umeamriwa na Mungu.
Tite 3.1  1 Pierre 2.13-2.17  Jean 19.11  Proverbes 8.15-8.16  Jude 1.8  
 2 Hivyo amwasiye mwenye mamlaka hushindana na agizo la Mungu; nao washindanao watajipatia hukumu.
1 Pierre 2.13  Tite 3.1  Romains 13.5  Marc 12.40  Jacques 3.1  
 3 Kwa maana watawalao hawatishi watu kwa sababu ya matendo mema, bali kwa sababu ya matendo mabaya. Basi, wataka usimwogope mwenye mamlaka? Fanya mema, nawe utapata sifa kwake;
Romains 13.4  Proverbes 14.35  Jérémie 22.15-22.18  Proverbes 20.2  Deutéronome 25.1  
 4 kwa kuwa yeye ni mtumishi wa Mungu kwako kwa ajili ya mema. Lakini ufanyapo mabaya, ogopa; kwa maana hauchukui upanga bure; kwa kuwa ni mtumishi wa Mungu, amlipizaye kisasi mtenda mabaya kwa ajili ya ghadhabu.
Romains 12.19  2 Chroniques 19.6  1 Thessaloniciens 4.6  Proverbes 24.23-24.24  Jérémie 5.28  
 5 Kwa hiyo ni lazima kutii, si kwa sababu ya ile ghadhabu tu, ila na kwa sababu ya dhamiri.
Ecclésiaste 8.2  1 Pierre 2.19  Actes 24.16  Hébreux 13.18  Tite 3.1-3.2  
 6 Kwa sababu hiyo tena mwalipa kodi; kwa kuwa wao ni wahudumu wa Mungu, wakidumu katika kazi iyo hiyo.
Matthieu 22.17-22.21  Matthieu 17.24-17.27  Marc 12.14-12.17  Luc 20.21-20.26  Deutéronome 1.9-1.17  
 7 Wapeni wote haki zao; mtu wa kodi, kodi; mtu wa ushuru, ushuru; astahiliye hofu, hofu; astahiliye heshima, heshima.
Matthieu 17.25  Luc 20.25  Matthieu 22.21  1 Timothée 5.17  Lévitique 19.32  
 8 Msiwiwe na mtu cho chote, isipokuwa kupendana; kwa maana ampendaye mwenzake ameitimiza sheria.
Romains 13.10  Matthieu 7.12  Galates 5.14  Jacques 2.8  Matthieu 22.39-22.40  
 9 Maana kule kusema, Usizini, Usiue, Usiibe, Usitamani; na ikiwapo amri nyingine yo yote, inajumlishwa katika neno hili, ya kwamba, Mpende jirani yako kama nafsi yako.Lévitique 19.18  Matthieu 19.18-19.19  Exode 20.12-20.17  Luc 10.27  Marc 12.31  
 10 Pendo halimfanyii jirani neno baya; basi pendo ndilo utimilifu wa sheria.
Romains 13.8  Matthieu 22.39-22.40  1 Corinthiens 13.4-13.7  
 11 Naam, tukiujua wakati, kwamba saa ya kuamka katika usingizi imekwisha kuwadia; kwa maana sasa wokovu wetu u karibu nasi kuliko tulipoanza kuamini
Ephésiens 5.14  1 Corinthiens 15.34  1 Pierre 4.7  Luc 21.28  Ecclésiaste 9.10  
 12 Usiku umeendelea sana, mchana umekaribia, basi na tuyavue matendo ya giza, na kuzivaa silaha za nuru.
Ephésiens 5.11  2 Corinthiens 6.7  Ezéchiel 18.31-18.32  1 Thessaloniciens 5.5-5.8  Esaïe 30.22  
 13 Kama ilivyohusika na mchana na tuenende kwa adabu; si kwa ulafi na ulevi, si kwa ufisadi na uasherati, si kwa ugomvi na wivu.
Galates 5.21  1 Thessaloniciens 4.12  Luc 21.34  1 Thessaloniciens 4.3-4.5  Ephésiens 5.18  
 14 Bali mvaeni Bwana Yesu Kristo, wala msiuangalie mwili, hata kuwasha tamaa zake.
Galates 3.27  Ephésiens 4.24  Galates 5.24  1 Pierre 2.11  Romains 8.12-8.13