Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Romains 13.2
Bible en Swahili de l’est


Devoirs envers les autorités

1 Kila mtu na aitii mamlaka iliyo kuu; kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu; na ile iliyopo umeamriwa na Mungu.
Tite 3.1 1 Pierre 2.13-2.17 Jean 19.11 Jude 1.8 Ephésiens 5.21
2 Hivyo amwasiye mwenye mamlaka hushindana na agizo la Mungu; nao washindanao watajipatia hukumu.
1 Pierre 2.13 Tite 3.1 Jérémie 23.8-23.17 Luc 20.47 Esaïe 58.2
3 Kwa maana watawalao hawatishi watu kwa sababu ya matendo mema, bali kwa sababu ya matendo mabaya. Basi, wataka usimwogope mwenye mamlaka? Fanya mema, nawe utapata sifa kwake;
Proverbes 20.2 Deutéronome 25.1 1 Pierre 3.13-3.14 Ecclésiaste 10.4-10.6 Romains 13.4
4 kwa kuwa yeye ni mtumishi wa Mungu kwako kwa ajili ya mema. Lakini ufanyapo mabaya, ogopa; kwa maana hauchukui upanga bure; kwa kuwa ni mtumishi wa Mungu, amlipizaye kisasi mtenda mabaya kwa ajili ya ghadhabu.
2 Chroniques 19.6 Romains 12.19 Proverbes 24.23-24.24 1 Thessaloniciens 4.6 Esaïe 1.17
5 Kwa hiyo ni lazima kutii, si kwa sababu ya ile ghadhabu tu, ila na kwa sababu ya dhamiri.
Ecclésiaste 8.2 1 Pierre 2.19 1 Samuel 24.5-24.6 1 Pierre 2.13-2.15 1 Pierre 3.16
6 Kwa sababu hiyo tena mwalipa kodi; kwa kuwa wao ni wahudumu wa Mungu, wakidumu katika kazi iyo hiyo.
Matthieu 22.17-22.21 Matthieu 17.24-17.27 Marc 12.14-12.17 Luc 20.21-20.26 Luc 23.2
7 Wapeni wote haki zao; mtu wa kodi, kodi; mtu wa ushuru, ushuru; astahiliye hofu, hofu; astahiliye heshima, heshima.
Matthieu 17.25 Luc 20.25 1 Timothée 5.17 Matthieu 22.21 1 Timothée 6.1

Devoirs envers les autres

8 Msiwiwe na mtu cho chote, isipokuwa kupendana; kwa maana ampendaye mwenzake ameitimiza sheria.
Romains 13.10 Matthieu 7.12 Galates 5.14 Matthieu 22.39-22.40 Jacques 2.8
9 Maana kule kusema, Usizini, Usiue, Usiibe, Usitamani; na ikiwapo amri nyingine yo yote, inajumlishwa katika neno hili, ya kwamba, Mpende jirani yako kama nafsi yako.
Lévitique 19.18 Matthieu 19.18-19.19 Exode 20.12-20.17 Marc 12.31 Romains 7.7-7.8
10 Pendo halimfanyii jirani neno baya; basi pendo ndilo utimilifu wa sheria.
Romains 13.8 Matthieu 22.39-22.40 1 Corinthiens 13.4-13.7
11 Naam, tukiujua wakati, kwamba saa ya kuamka katika usingizi imekwisha kuwadia; kwa maana sasa wokovu wetu u karibu nasi kuliko tulipoanza kuamini
Ephésiens 5.14 1 Corinthiens 15.34 Luc 21.28 1 Pierre 4.7 1 Corinthiens 7.29-7.31
12 Usiku umeendelea sana, mchana umekaribia, basi na tuyavue matendo ya giza, na kuzivaa silaha za nuru.
Ephésiens 5.11 2 Corinthiens 6.7 Ezéchiel 18.31-18.32 1 Thessaloniciens 5.5-5.8 Esaïe 30.22
13 Kama ilivyohusika na mchana na tuenende kwa adabu; si kwa ulafi na ulevi, si kwa ufisadi na uasherati, si kwa ugomvi na wivu.
Galates 5.21 Luc 21.34 1 Thessaloniciens 4.3-4.5 1 Thessaloniciens 4.12 Ephésiens 5.18
14 Bali mvaeni Bwana Yesu Kristo, wala msiuangalie mwili, hata kuwasha tamaa zake.
Galates 3.27 Ephésiens 4.24 Galates 5.24 1 Pierre 2.11 Colossiens 3.5-3.8

Cette Bible est dans le domaine public.