Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Romains 13.12
Bible en Swahili de l’est


Devoirs envers les autorités

1 Kila mtu na aitii mamlaka iliyo kuu; kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu; na ile iliyopo umeamriwa na Mungu.
Tite 3.1 Jean 19.11 1 Pierre 2.13-2.17 Daniel 2.21 Proverbes 8.15-8.16
2 Hivyo amwasiye mwenye mamlaka hushindana na agizo la Mungu; nao washindanao watajipatia hukumu.
Tite 3.1 1 Pierre 2.13 Jérémie 44.14-44.17 Romains 13.5 Marc 12.40
3 Kwa maana watawalao hawatishi watu kwa sababu ya matendo mema, bali kwa sababu ya matendo mabaya. Basi, wataka usimwogope mwenye mamlaka? Fanya mema, nawe utapata sifa kwake;
1 Pierre 3.13-3.14 Ecclésiaste 10.4-10.6 Romains 13.4 Proverbes 14.35 Jérémie 22.15-22.18
4 kwa kuwa yeye ni mtumishi wa Mungu kwako kwa ajili ya mema. Lakini ufanyapo mabaya, ogopa; kwa maana hauchukui upanga bure; kwa kuwa ni mtumishi wa Mungu, amlipizaye kisasi mtenda mabaya kwa ajili ya ghadhabu.
Romains 12.19 2 Chroniques 19.6 1 Thessaloniciens 4.6 Proverbes 24.23-24.24 Michée 3.9
5 Kwa hiyo ni lazima kutii, si kwa sababu ya ile ghadhabu tu, ila na kwa sababu ya dhamiri.
1 Pierre 2.19 Ecclésiaste 8.2 1 Pierre 3.16 Actes 24.16 Hébreux 13.18
6 Kwa sababu hiyo tena mwalipa kodi; kwa kuwa wao ni wahudumu wa Mungu, wakidumu katika kazi iyo hiyo.
Luc 20.21-20.26 Matthieu 22.17-22.21 Matthieu 17.24-17.27 Marc 12.14-12.17 Romains 12.8
7 Wapeni wote haki zao; mtu wa kodi, kodi; mtu wa ushuru, ushuru; astahiliye hofu, hofu; astahiliye heshima, heshima.
Matthieu 17.25 Luc 20.25 Matthieu 22.21 1 Timothée 5.17 Exode 20.12

Devoirs envers les autres

8 Msiwiwe na mtu cho chote, isipokuwa kupendana; kwa maana ampendaye mwenzake ameitimiza sheria.
Romains 13.10 Matthieu 7.12 Galates 5.14 Jacques 2.8 Matthieu 22.39-22.40
9 Maana kule kusema, Usizini, Usiue, Usiibe, Usitamani; na ikiwapo amri nyingine yo yote, inajumlishwa katika neno hili, ya kwamba, Mpende jirani yako kama nafsi yako.
Lévitique 19.18 Matthieu 19.18-19.19 Exode 20.12-20.17 Luc 10.27 Marc 12.31
10 Pendo halimfanyii jirani neno baya; basi pendo ndilo utimilifu wa sheria.
Romains 13.8 Matthieu 22.39-22.40 1 Corinthiens 13.4-13.7
11 Naam, tukiujua wakati, kwamba saa ya kuamka katika usingizi imekwisha kuwadia; kwa maana sasa wokovu wetu u karibu nasi kuliko tulipoanza kuamini
Ephésiens 5.14 1 Corinthiens 15.34 Luc 21.28 1 Pierre 4.7 1 Thessaloniciens 5.1-5.3
12 Usiku umeendelea sana, mchana umekaribia, basi na tuyavue matendo ya giza, na kuzivaa silaha za nuru.
Ephésiens 5.11 2 Corinthiens 6.7 Esaïe 2.20 Ezéchiel 18.31-18.32 1 Thessaloniciens 5.5-5.8
13 Kama ilivyohusika na mchana na tuenende kwa adabu; si kwa ulafi na ulevi, si kwa ufisadi na uasherati, si kwa ugomvi na wivu.
Galates 5.21 1 Thessaloniciens 4.12 Luc 21.34 1 Thessaloniciens 4.3-4.5 Ephésiens 5.18
14 Bali mvaeni Bwana Yesu Kristo, wala msiuangalie mwili, hata kuwasha tamaa zake.
Galates 3.27 Ephésiens 4.24 Galates 5.24 1 Pierre 2.11 Romains 8.12-8.13

Cette Bible est dans le domaine public.