Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Michée 7.1
Bible en Swahili de l’est


1 Ole wangu! Maana mimi ni kama hapo walipokwisha kuyachuma matunda ya wakati wa hari, kama zabibu zichumwazo baada ya mavuno; hapana shada la kuliwa; roho yangu inatamani tini iivayo kwanza.
Esaïe 28.4 Osée 9.10 Esaïe 24.13 Esaïe 17.6 Jérémie 45.3
2 Mtu amchaye Mungu ametoweka, asionekane katika nchi, wala hapana mtu mwenye adili katika wanadamu; wote huotea ili kumwaga damu; kila mtu humwinda ndugu yake kwa wavu.
Psaumes 12.1 Jérémie 5.26 Esaïe 57.1 Proverbes 1.11 Esaïe 59.7
3 Mikono yao inayashika mabaya wayatende kwa bidii; mtu mkuu aomba rushwa, kadhi yu tayari kuipokea; mtu mkubwa hunena madhara yaliyomo rohoni mwake; hivyo ndivyo wayafumavyo hayo pamoja.
Michée 3.11 Proverbes 4.16-4.17 Amos 5.12 Jérémie 8.10 Osée 4.18
4 Mtu aliye mwema miongoni mwao ni kama mbigili; mtu aliye mwenye adili miongoni mwao ni mbaya kuliko boma la michongoma; hiyo siku ya walinzi wako, yaani, siku ya kujiliwa kwako, imefika; sasa kutatokea kufadhaika kwao.
Esaïe 22.5 Ezéchiel 2.6 2 Samuel 23.6-23.7 Esaïe 10.3 Hébreux 6.8
5 Msimwamini rafiki, msimwekee kiongozi tumaini; ilinde milango ya midomo ya kinywa chako ili mkeo alalaye kifuani mwako asijue habari.
Jérémie 9.4 Psaumes 118.8-118.9 Job 6.14-6.15 Matthieu 10.16 Juges 16.5-16.20
6 Kwa maana mwana humwaibisha babaye, na binti huondoka ashindane na mamaye; na mwanamke aliyeolewa hushindana na mavyaaye; adui za mtu ni watu wa nyumbani mwake mwenyewe.
Matthieu 10.35-10.36 Matthieu 10.21 Luc 12.53 Ezéchiel 22.7 Proverbes 30.17

Espérance et promesses pour Israël

7 Lakini mimi, nitamtazamia Bwana; nitamngojea Mungu wa wokovu wangu; Mungu wangu atanisikia.
Psaumes 25.5 Esaïe 25.9 Psaumes 37.7 Psaumes 62.1-62.8 Esaïe 45.22
8 Usifurahi juu yangu, Ee adui yangu; niangukapo, nitasimama tena; nikaapo gizani, Bwana atakuwa nuru kwangu.
Esaïe 9.2 Psaumes 112.4 Psaumes 107.10-107.15 2 Corinthiens 4.6 Jean 8.12
9 Nitaivumilia ghadhabu ya Bwana, kwa kuwa nimemwasi; hata atakaponitetea teto langu, na kunifanyia hukumu; atanileta nje kwenye nuru, nami nitaiona haki yake.
Psaumes 37.6 1 Samuel 24.15 2 Thessaloniciens 1.5-1.10 1 Corinthiens 4.5 Apocalypse 6.10-6.11
10 Ndipo adui yangu ataliona jambo hilo, na aibu itamfunika, yeye aliyeniambia, Yuko wapi Bwana, Mungu wako? Macho yangu yatamtazama; sasa atakanyagwa kama matope ya njia kuu.
Zacharie 10.5 Joël 2.17 Michée 4.11 Psaumes 42.10 Psaumes 18.42
11 Ni siku ya kujengwa kuta zako! Siku hiyo mpaka utasongezwa mbali.
Néhémie 2.8 Néhémie 4.3 Néhémie 2.17 Esaïe 54.11 Néhémie 4.6
12 Siku hiyo watakujia kutoka Ashuru na miji ya Misri, na kutoka Misri mpaka huo Mto, na kutoka bahari hii mpaka bahari hii, na kutoka mlima huu mpaka mlima huu.
Esaïe 19.23-19.25 Esaïe 11.16 Osée 11.11 Jérémie 3.18 Esaïe 43.6
13 Hata hivyo nchi itakuwa ukiwa kwa sababu ya hao wakaao ndani yake, kwa sababu ya matunda ya matendo yao.
Esaïe 3.10-3.11 Jérémie 25.11 Job 4.8 Jérémie 17.10 Michée 3.12
14 Walishe watu wako kwa fimbo yako, kundi la urithi wako, wakaao peke yao, mwituni katikati ya Karmeli; na walishe katika Bashani na Gileadi, kama siku za kale.
Michée 5.4 Psaumes 28.9 Amos 9.11 Esaïe 49.10 Psaumes 95.7
15 Kama katika siku zile za kutoka kwako katika nchi ya Misri nitamwonyesha mambo ya ajabu.
Esaïe 11.16 Exode 3.20 Jérémie 23.7-23.8 Esaïe 63.11-63.15 Psaumes 78.12-78.72
16 Mataifa wataona, na kuzitahayarikia nguvu zao zote; wataweka mikono yao juu ya vinywa vyao, masikio yao yatakuwa na uziwi.
Esaïe 26.11 Job 40.4 Job 29.9-29.10 Esaïe 52.15 Zacharie 8.20-8.23
17 Watayaramba mavumbi kama nyoka, kama vitu vitambaavyo juu ya nchi watatoka katika mahali walimojificha, wakitetemeka; watakuja kwa Bwana, Mungu wetu, kwa hofu, nao wataogopa kwa sababu yako.
Esaïe 49.23 Psaumes 72.9 Psaumes 18.45 Apocalypse 3.9 Lamentations 3.29
18 Ni nani aliye Mungu kama wewe, mwenye kusamehe uovu, na kuliachilia kosa la watu wa urithi wake waliosalia? Hashiki hasira yake milele, kwa maana yeye hufurahia rehema.
Esaïe 43.25 Jérémie 50.20 Jérémie 32.41 Michée 2.12 Exode 15.11
19 Atarejea na kutuhurumia; atayakanyaga maovu yetu; nawe utazitupa dhambi zao zote katika vilindi vya bahari.
Esaïe 38.17 Jérémie 50.20 Romains 6.14 Esaïe 43.25 Esaïe 63.15-63.17
20 Wewe utamtimilizia Yakobo kweli yako, na Ibrahimu rehema zako, ulizowaapia baba zetu tangu siku za kale.
Luc 1.72-1.74 Genèse 28.13-28.14 Genèse 17.7-17.8 Genèse 26.3-26.4 Luc 1.54-1.55

Cette Bible est dans le domaine public.