Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Abdias 1.19
Bible en Swahili de l’est


Le jugement d’Édom et ses causes

1 Maono yake Obadia. Ndivyo asemavyo Bwana MUNGU juu ya Edomu; Tumepata habari kwa Bwana, Na mjumbe ametumwa kati ya mataifa, Akisema,Haya,inukeni ninyi;Na tuinuke tupigane naye.
Amos 1.11-1.12 Ezéchiel 25.12-25.14 Esaïe 63.1-63.6 Malachie 1.3-1.4 Esaïe 30.4
2 Tazama, nimekufanya mdogo kati ya mataifa; Umedharauliwa sana.
Nombres 24.18 Esaïe 23.9 Luc 1.51-1.52 1 Samuel 2.7-2.8 Michée 7.10
3 Kiburi cha moyo wako kimekudanganya, Wewe ukaaye katika pango za majabali, Mwenye makao yako juu sana; Asemaye moyoni, Ni nani atakayenishusha mimi?
Esaïe 14.13-14.15 Esaïe 16.6 Proverbes 29.23 Jérémie 49.16 2 Rois 14.7
4 Ujapopanda juu kama tai, Ijapokuwa kioto chako kimewekwa kati ya nyota, Nitakushusha kutoka huko; asema Bwana.
Esaïe 14.12-14.15 Habakuk 2.9 Job 20.6-20.7 Jérémie 51.53 Jérémie 49.16
5 Kama wevi wangekujilia, kama wanyang’anyi wangekujilia usiku, (jinsi ulivyokatiliwa mbali!) Je! Wasingeiba kiasi cha kuwatosha? Kama wachumao zabibu wangekujilia, je! Wasingeacha baadhi ya zabibu, ziokotwe?
Jérémie 49.9 Deutéronome 24.21 Esaïe 17.6 Sophonie 2.15 Michée 7.1
6 Jinsi watu wa Esau wanavyotafutwa-tafutwa! Jinsi hazina zake zilizofichwa zinavyoulizwa-ulizwa!
Jérémie 49.10 Esaïe 10.13-10.14 Jérémie 50.37 Esaïe 45.3 Daniel 2.22
7 Watu wote wa mapatano yako Wamekufukuza, hata mipakani; Wale waliofanya amani nawe Wamekudanganya, na kukushinda; Walao mkate wako wameweka mtego chini yako; Wala hana ufahamu wa hayo ndani yake.
Psaumes 41.9 Jérémie 49.7 Jérémie 30.14 Psaumes 55.12-55.13 Ezéchiel 23.22-23.25
8 Siku hiyo, je! Sitawaangamiza watu wenye akili katika Edomu, na wenye ufahamu katika kilima cha Esau? Asema Bwana.
Esaïe 29.14 Job 5.12-5.14 1 Corinthiens 3.19-3.20 Esaïe 19.3 Psaumes 33.10
9 Na mashujaa wako, Ee Temani, watafadhaika, hata iwe kila mtu akatiliwe mbali kwa kuuawa katika kilima cha Esau.
Amos 1.12 Genèse 36.11 Esaïe 63.1-63.3 Ezéchiel 25.13 Esaïe 34.5-34.8
10 Kwa sababu ya udhalimu aliotendwa ndugu yako Yakobo, aibu itakufunika, nawe utakatiliwa mbali hata milele.
Amos 1.11 Psaumes 89.45 Nombres 20.14-20.21 Genèse 27.41 Psaumes 137.7
11 Siku ile uliposimama upande, siku ile wageni walipochukua mali zake, na watu wa kabila nyingine walipoingia katika malango yake, na kumpa kura juu ya Yerusalemu, wewe nawe ulikuwa kama mmoja wao.
Psaumes 137.7 Joël 3.3 Nahum 3.10 2 Rois 25.11 2 Rois 24.10-24.16
12 Lakini usiitazame siku ya ndugu yako, siku ya mashaka yake, wala usisimange juu ya wana wa Yuda siku ya kuangamizwa kwao; wala usinene maneno ya kiburi katika siku ya shida yao.
Proverbes 17.5 Michée 4.11 Ezéchiel 35.15 1 Samuel 2.3 Psaumes 22.17
13 Usiingie katika lango la watu wangu, siku ya msiba wao; naam, usiyatazame mateso yao, siku ya msiba wao; wala usitie mikono yako juu ya mali zao, siku ya msiba wao.
Ezéchiel 35.10 Psaumes 22.17 Ezéchiel 35.5 Zacharie 1.15 2 Samuel 16.12
14 Wala usisimame penye njia panda, ili kuwakatilia mbali watu wake wakimbiao; wala usiwatoe watu wake waliosalia, katika siku ya dhiki.
Genèse 35.3 Jérémie 30.7 Amos 1.6 Abdias 1.12 Psaumes 31.8

Le jour de l’Éternel

15 Kwa maana hiyo siku ya Bwana i karibu juu ya mataifa yote; kama ulivyotenda, ndivyo utakavyotendwa; malipo yako yatakurudia juu ya kichwa chako mwenyewe.
Habakuk 2.8 Ezéchiel 30.3 Ezéchiel 35.15 Jérémie 50.29 Psaumes 137.8
16 Kwa maana kama vile mlivyokunywa juu ya mlima wangu mtakatifu, ndivyo mataifa yote watakavyokunywa daima; naam, watakunywa na kubabaika, nao watakuwa kana kwamba hawakuwa kamwe.
Jérémie 49.12 Joël 3.17 Jérémie 25.15-25.16 Esaïe 51.22-51.23 Esaïe 49.25-49.26
17 Bali katika mlima Sayuni watakuwako wenye kuokoka, nao utakuwa mtakatifu; na nyumba ya Yakobo watamiliki milki zao.
Amos 9.11-9.15 Joël 2.32 Esaïe 14.1-14.2 Amos 9.8 Jérémie 44.28
18 Na nyumba ya Yakobo itakuwa moto, na nyumba ya Yusufu itakuwa mwali wa moto, na nyumba ya Esau itakuwa mabua makavu, nao watawaka kati yao, na kuwateketeza; wala hatasalia mtu awaye yote katika nyumba ya Esau; kwa kuwa Bwana amesema hayo.
Zacharie 12.6 Esaïe 10.17 Joël 2.5 Esaïe 5.24 Nahum 1.10
19 Na watu wa Negebu wataumiliki mlima wa Esau; na watu wa Shefela watawamiliki Wafilisti; nao watalimiliki konde la Efraimu, na konde la Samaria, na Benyamini atamiliki Gileadi.
Amos 9.12 Jérémie 32.44 Sophonie 2.4-2.7 Nombres 24.18-24.19 Ezéchiel 37.21-37.25
20 Na watu wa jeshi hili la wana wa Israeli waliotekwa, walio kati ya Wakanaani, watamiliki mpaka Sarepta; na hao watu wa Yerusalemu waliotekwa, waliomo Sefaradi, wataimiliki miji ya Negebu.
Luc 4.26 1 Rois 17.9-17.10 Jérémie 33.13 Jérémie 32.44 Ezéchiel 34.12-34.13
21 Tena waokozi watakwea juu ya mlima Sayuni ili kuuhukumu mlima wa Esau; na huo ufalme utakuwa ni mali ya Bwana.
Apocalypse 11.15 Daniel 7.27 Psaumes 22.28 Zacharie 14.9 Daniel 2.44

Cette Bible est dans le domaine public.