Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Amos 6.6
Bible en Swahili de l’est


Corruption et inconscience des grands

1 Ole wao wanaostarehe katika Sayuni, na hao wanaokaa salama katika mlima wa Samaria, watu mashuhuri wa taifa lililo la kwanza, ambao nyumba ya Israeli huwaendea.
Amos 4.1 Esaïe 32.9-32.11 Jacques 5.5 Exode 19.5-19.6 Sophonie 1.12
2 Piteni hata Kalne, mkaone; tena tokea huko enendeni hata Hamathi iliyo kuu; kisha shukeni hata Gathi ya Wafilisti; je! Ninyi ni bora kuliko falme hizi? Au mpaka wao ni mkubwa kuliko mpaka wenu?
Nahum 3.8 Genèse 10.10 2 Rois 18.34 2 Chroniques 26.6 1 Samuel 17.4
3 Ninyi mnaoiweka mbali siku hiyo mbaya, na kulileta karibu kao la udhalimu;
Amos 9.10 Esaïe 56.12 Ezéchiel 12.27 Esaïe 47.7 2 Pierre 3.4
4 ninyi mnaolala juu ya vitanda vya pembe, na kujinyosha juu ya masemadari yenu; ninyi mnaokula wana-kondoo wa kundi, na ndama waliomo zizini;
Jacques 5.5 Amos 3.12 Ezéchiel 34.2-34.3 Esaïe 22.13 1 Samuel 25.36-25.38
5 ninyi mnaoimba nyimbo za upuzi pamoja na sauti ya vinanda, na kujifanyizia vinanda vya namna nyingi, kama vile Daudi;
Esaïe 5.12 Amos 5.23 1 Chroniques 23.5 Ecclésiaste 2.8 Genèse 31.27
6 ninyi mnaokunywa divai katika mabakuli, na kujipaka marhamu iliyo nzuri; lakini hawahuzuniki kwa sababu ya mateso ya Yusufu.
Genèse 49.22 Esther 3.15 Romains 12.15 2 Rois 15.29 Jean 12.3
7 Basi kwa ajili ya hayo sasa watakwenda utumwani pamoja na wa kwanza watakaokwenda utumwani, na kelele za machezo za hao waliojinyosha zitakoma.
Amos 7.11 1 Rois 20.16-20.20 Amos 5.5 Daniel 5.4-5.6 Esther 7.8-7.10
8 Bwana MUNGU ameapa kwa nafsi yake, asema Bwana, Mungu wa majeshi; Naizira fahari ya Yakobo, nachukizwa na majumba yake; kwa sababu hiyo nitautoa huo mji, pamoja na wote waliomo ndani yake.
Jérémie 51.14 Amos 4.2 Psaumes 47.4 Amos 3.11 Jérémie 22.5
9 Hata itakuwa, wakisalia wanaume kumi katika nyumba moja, watakufa.
Amos 5.3 Esther 5.11 Esaïe 14.21 Psaumes 109.13 Esther 9.10
10 Na mjomba wa mtu atakapomwinua, yaani, yeye amchomaye moto, ili atoe mifupa yake nyumbani, naye atakapomwambia yeye aliye katika pande za ndani za nyumba, Je! Yuko mtu ye yote pamoja nawe? Naye atakaposema, La, hapana; ndipo atasema, Nyamaza kimya; maana hatuna ruhusa kulitaja jina la Bwana.
Amos 8.3 1 Samuel 31.12 Amos 5.13 Jérémie 44.26 Ezéchiel 20.39
11 Kwa maana, angalia, Bwana atoa amri, na nyumba kubwa itapigwa na kuwa na mahali palipobomolewa, na nyumba ndogo nayo itapigwa iwe na nyufa.
Amos 3.15 Esaïe 55.11 2 Rois 25.9 Esaïe 10.5-10.6 Amos 6.8
12 Je! Farasi watapiga mbio juu ya mwamba? Je! Mtu atalima na ng’ombe huko? Hata mmegeuza hukumu kuwa uchungu, na matunda ya haki kuwa pakanga;
Amos 5.7 Osée 10.4 Amos 5.11-5.12 1 Rois 21.7-21.13 Esaïe 59.13-59.14
13 ninyi mnaolifurahia jambo lisilo na maana, msemao, Je! Hatukujipatia pembe kwa nguvu zetu wenyewe?
Esaïe 28.14-28.15 Luc 12.19-12.20 2 Rois 14.25 Jacques 4.16 Jonas 4.6
14 Maana, angalia, nitaondokesha taifa juu yenu, enyi nyumba ya Israeli, asema Bwana, Mungu wa majeshi, nao watawatesa ninyi toka mahali pa kuingilia katika Hamathi hata kijito cha Araba.
2 Rois 14.25 1 Rois 8.65 Jérémie 5.15-5.17 Ezéchiel 47.15-47.17 Esaïe 7.20

Cette Bible est dans le domaine public.