Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Lévitique 1.14
Bible en Swahili de l’est


Les sacrifices

L’holocauste

1 Bwana akamwita Musa, na kusema naye kutoka katika hema ya kukutania, akamwambia,
Exode 19.3 Exode 25.22 Exode 40.34-40.35 Exode 29.42 Exode 39.32
2 Nena na wana wa Israeli, uwaambie, Mtu wa kwenu atakapomtolea Bwana matoleo, mtatoa matoleo yenu katika wanyama wa mifugo, katika ng’ombe na katika kondoo.
Lévitique 22.18-22.19 Ephésiens 5.2 Genèse 4.3 Genèse 4.5 1 Chroniques 16.29
3 Matoleo yake kwamba ni sadaka ya kuteketezwa ya ng’ombe, atatoa ng’ombe mume mkamilifu; ataleta mlangoni pa hema ya kukutania, ili akubaliwe mbele ya Bwana.
Hébreux 9.14 Deutéronome 15.21 Exode 12.5 Lévitique 22.19-22.24 Nombres 29.13
4 Kisha ataweka mkono wake juu ya kichwa cha hiyo sadaka ya kuteketezwa; nayo itakubaliwa kwa ajili yake, ili kufanya upatanisho kwa ajili yake.
Lévitique 3.2 Exode 29.15 Exode 29.10 2 Chroniques 29.23-29.24 Exode 29.19
5 Naye atamchinja huyo ng’ombe mbele ya Bwana; kisha wana wa Haruni, hao makuhani, wataileta karibu hiyo damu, na kuinyunyiza damu yake kando-kando katika madhabahu iliyo hapo mlangoni pa hema ya kukutania
Lévitique 1.11 Lévitique 3.8 Lévitique 3.2 Hébreux 12.24 1 Pierre 1.2
6 Kisha atachuna sadaka ya kuteketeza na kuikata vipande vyake.
Lévitique 7.8 Genèse 3.21
7 Kisha wana wa Haruni, watatia moto juu ya madhabahu, na kuzipanga kuni juu ya moto,
Lévitique 6.12-6.13 Genèse 22.9 2 Chroniques 7.1 1 Chroniques 21.26 Néhémie 13.31
8 kisha wana wa Haruni, makuhani, watazipanga kuni zilizo juu ya moto uliopo juu ya madhabahu;
Lévitique 8.18-8.21 1 Rois 18.33 Lévitique 9.13-9.14 Exode 29.17-29.18 Lévitique 1.12
9 lakini matumbo yake, na miguu yake, ataiosha kwa maji; na huyo kuhani ataviteketeza vyote juu ya madhabahu, ili iwe sadaka ya kuteketezwa, dhabihu ya kusongezwa kwa njia ya moto, ya harufu ya kupendeza kwa Bwana.
Genèse 8.21 Lévitique 1.13 Ephésiens 5.2 Exode 29.18 Lévitique 3.11
10 Na matoleo yake kwamba ni katika kundi, katika kondoo, au katika mbuzi, kuwa sadaka ya kuteketezwa; atatoa mume mkamilifu.
Lévitique 4.23 Malachie 1.14 Esaïe 53.6-53.7 Genèse 4.4 Genèse 8.20
11 Naye atamchinja hapo upande wa madhabahu ulioelekea kaskazini mbele za Bwana; na wana wa Haruni, hao makuhani, watainyunyiza damu yake juu ya madhabahu pande zote.
Lévitique 1.5 Lévitique 1.7-1.9 Lévitique 9.12-9.14 Exode 40.22 Ezéchiel 8.5
12 Kisha atamkata vipande vyake, pamoja na kichwa chake, na mafuta yake; kisha atavipanga vile vipande juu ya kuni zilizo juu ya madhabahu;
13 lakini matumbo yake, na miguu yake, ataosha kwa maji; na huyo kuhani atavisongeza vyote na kuviteketeza juu ya madhabahu; ni sadaka ya kuteketezwa, dhabihu ya kusongezwa kwa njia ya moto, ya harufu ya kupendeza kwa Bwana.
Lévitique 1.9
14 Na matoleo yake atakayomtolea Bwana kuwa sadaka ya kuteketezwa, kwamba ni katika ndege, ndipo atakapoleta matoleo yake katika hua au katika makinda ya njiwa.
Lévitique 5.7 Luc 2.24 Lévitique 12.8 2 Corinthiens 8.12 Hébreux 7.26
15 Kisha kuhani atamleta karibu na madhabahu, naye atamkongonyoa kichwa, na kumteketeza kwa moto juu ya madhabahu; na damu yake itachuruzishwa kando ya madhabahu;
Esaïe 53.4-53.5 1 Jean 2.27 Lévitique 5.8-5.9 Psaumes 22.21 Psaumes 69.1-69.21
16 kisha atakiondoa kile kibofu chake, pamoja na taka zake, na kukitupa kando ya madhabahu upande wa mashariki, mahali pa majivu;
Lévitique 4.12 Hébreux 13.11-13.14 1 Pierre 1.2 Lévitique 16.27 Luc 1.35
17 kisha atampasua na mabawa yake, lakini asimkate vipande viwili; kisha kuhani atamteketeza juu ya madhabahu, juu ya kuni zilizo juu ya moto; ni sadaka ya kuteketezwa, dhabihu ya kusongezwa kwa njia ya moto, ya harufu ya kupendeza kwa Bwana.
Genèse 15.10 Lévitique 5.8 Matthieu 27.50 Jean 19.30 Genèse 8.21

Cette Bible est dans le domaine public.