Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ezéchiel 9.10
Bible en Swahili de l’est


Jugements des idolâtres

1 Kisha akalia kwa sauti kuu masikioni mwangu, akisema, Waamuru wale wanaousimamia mji wakaribie, kila mmoja na awe na kitu chake cha kuangamiza mkononi mwake.
Esaïe 6.8 1 Chroniques 21.15 Apocalypse 1.10-1.11 2 Rois 10.24 Ezéchiel 43.6-43.7
2 Na tazama, watu sita wakaja, wakitokea kwa njia ya lango la juu, lielekealo upande wa kaskazini, kila mmoja ana kitu chake cha kufisha mkononi mwake; na mtu mmoja kati yao amevaa bafta, naye ana kidau cha wino cha mwandishi kiunoni. Wakaingia, wakasimama karibu na madhabahu ya shaba.
Ezéchiel 10.2 Lévitique 16.4 Apocalypse 15.6 Ezéchiel 10.6-10.7 2 Rois 15.35
3 Na huo utukufu wa Bwana wa Israeli ulikuwa umepanda juu kutoka kwa kerubi, ambaye ulikuwa juu yake, mpaka kizingiti cha nyumba; akamwita mtu yule aliyekuwa amevaa bafta, mwenye kidau cha wino cha mwandishi kiunoni.
Ezéchiel 10.4 Ezéchiel 11.22-11.23 Ezéchiel 43.2-43.4 Ezéchiel 8.4 Ezéchiel 3.23
4 Bwana akamwambia, Pita kati ya mji, kati ya Yerusalemu, ukatie alama katika vipaji vya nyuso vya watu wanaougua na kulia kwa sababu ya machukizo yote yanayofanyika kati yake.
Apocalypse 9.4 Apocalypse 14.1 2 Corinthiens 1.22 Apocalypse 7.2-7.3 Psaumes 119.53
5 Na hao wengine aliwaambia, nami nalisikia, Piteni kati ya mji nyuma yake, mkapige; jicho lenu lisiachilie, wala msione huruma;
Ezéchiel 5.11 Exode 32.27 Deutéronome 32.39-32.42 Ezéchiel 7.9 Ezéchiel 8.18
6 Waueni kabisa, mzee, na kijana, na msichana, na watoto wachanga, na wanawake; lakini msimkaribie mtu ye yote mwenye hiyo alama; tena anzeni katika patakatifu pangu. Basi, wakaanza kwa wazee waliokuwa mbele ya nyumba.
2 Chroniques 36.17 Jérémie 25.29 Apocalypse 9.4 Luc 12.47 1 Samuel 15.3
7 Akawaambia, itieni nyumba unajisi, mkazijaze nyua mizoga ya hao waliouawa; haya, enendeni. Wakaenenda, wakapiga-piga katika mji.
Ezéchiel 7.20-7.22 2 Chroniques 36.17 Luc 13.1 Lamentations 2.4-2.7 Psaumes 79.1-79.3
8 Tena ikawa, walipokuwa wakipiga, nami nikiachwa, nalianguka kifudifudi, nikalia, nikasema, Ee Bwana MUNGU! Utaangamiza mabaki yote ya Israeli, wakati wa kumwaga ghadhabu yako juu ya Yerusalemu?
Ezéchiel 11.13 Ezéchiel 4.14 Nombres 14.5 1 Chroniques 21.16 Josué 7.6
9 Ndipo akaniambia, Uovu wa nyumba ya Israeli na Yuda ni mwingi sana, nayo nchi imejaa damu, nao mji umejaa kupotosha hukumu; maana husema, Bwana ameiacha nchi hii, naye Bwana haoni.
Ezéchiel 8.12 Job 22.13 Ezéchiel 7.23 2 Chroniques 36.14-36.16 Michée 3.1-3.3
10 Nami, jicho langu halitaachilia, wala sitaona huruma; lakini nitaleta njia yao juu ya vichwa vyao.
Ezéchiel 7.4 Esaïe 65.6 Ezéchiel 8.18 Ezéchiel 11.21 Ezéchiel 5.11
11 Na tazama, mtu yule aliyevaa bafta, mwenye kidau cha wino kiunoni, akaleta habari, akisema, Nimefanya kama ulivyoniamuru.
Zacharie 6.7-6.8 Apocalypse 16.17 Apocalypse 16.2 Esaïe 46.10-46.11 Psaumes 103.20

Cette Bible est dans le domaine public.