Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ezéchiel 18.16
Bible en Swahili de l’est


On récolte ce qu’on sème

1 Neno la Bwana likanijia tena, kusema,
2 Je! Maana yake ni nini hata mkatumia mithali hii katika Israeli, mkisema, Baba wamekula zabibu mbichi, nao watoto wakatiwa ganzi la meno?
Lamentations 5.7 Esaïe 3.15 Jérémie 31.29-31.30 Romains 9.20 Jérémie 15.4
3 Kama mimi niishivyo, asema Bwana MUNGU, hamtakuwa na sababu ya kuitumia tena mithali hii katika Israeli.
Ezéchiel 18.19-18.20 Ezéchiel 18.30 Ezéchiel 33.11-33.20 Ezéchiel 36.31-36.32 Romains 3.19
4 Tazama, roho zote ni mali yangu; kama vile roho ya baba ni mali yangu, ndivyo ilivyo roho ya mwana mali yangu; roho ile itendayo dhambi itakufa.
Ezéchiel 18.20 Romains 6.23 Nombres 16.22 Hébreux 12.9 Zacharie 12.1
5 Bali kama mtu ni mwenye haki, na kuyatenda yaliyo halali na haki;
Romains 2.7-2.10 Matthieu 7.21-7.27 1 Jean 3.7 Psaumes 24.4-24.6 Ezéchiel 33.14
6 hakula juu ya milima, wala hakuviinulia macho vinyago vya nyumba ya Israeli, wala hakumtia unajisi mke wa jirani yake, wala hakumkaribia mwanamke wakati wa kutengwa kwake;
Ezéchiel 18.15 Ezéchiel 20.24 Deutéronome 4.19 Ezéchiel 6.13 Ezéchiel 18.11-18.12
7 wala hakumdhulumu mtu, bali amemrudishia mdeni wake rehani yake, wala hakumnyang’anya mtu mali yake kwa nguvu, naye amewapa wenye njaa chakula chake, na kuwavika nguo walio uchi;
Ezéchiel 18.16 Ezéchiel 18.12 Exode 22.26 Deutéronome 24.12-24.13 Ezéchiel 33.15
8 ambaye hakumkopesha mtu ili apate faida, wala hakupokea ziada ya namna yo yote; naye ameuepusha mkono wake na uovu, na kufanya hukumu ya haki kati ya mtu na mwenzake;
Exode 22.25 Zacharie 8.16 Deutéronome 23.19-23.20 Ezéchiel 22.12 Psaumes 15.5
9 tena ikiwa amezifuata sheria zangu, na kuzishika hukumu zangu; mtu huyu ni mwenye haki; hakika ataishi, asema Bwana MUNGU.
Ezéchiel 20.11 Amos 5.4 Habakuk 2.4 Ezéchiel 18.17 Romains 1.17
10 Walakini akizaa mwana aliye mnyang’anyi, mmwaga damu, atendaye mambo hayo mojawapo;
Exode 21.12 1 Jean 3.12 Jean 18.40 Lévitique 19.13 Genèse 9.5-9.6
11 wala hakutenda mojawapo la mambo hayo yampasayo, bali amekula juu ya milima, na kumtia unajisi mke wa jirani yake,
Jacques 2.17 Jean 15.14 1 Rois 13.22 1 Rois 13.8 Apocalypse 22.14
12 na kuwadhulumu maskini na wahitaji, na kuwanyang’anya watu mali yao kwa nguvu, wala hakurudisha rehani, naye ameviinulia macho vinyago, na kufanya machukizo,
Ezéchiel 8.17 Ezéchiel 8.6 Amos 4.1 2 Rois 21.11 Ezéchiel 18.16
13 naye amekopesha watu ili apate faida, na kupokea ziada; je! Ataishi baada ya hayo? La, hataishi; amefanya machukizo hayo yote; hakika atakufa; damu yake itakuwa juu yake.
Lévitique 20.9 Ezéchiel 3.18 Exode 22.25 Ezéchiel 18.8 Ezéchiel 18.17
14 Na kama yeye huyo akizaa mwana, naye ameona dhambi zote za baba yake alizozitenda, akaogopa, asifanye neno lo lote kama hayo;
2 Chroniques 34.21 Proverbes 23.24 Ezéchiel 18.10 Psaumes 119.59-119.60 Aggée 1.5
15 hakula juu ya milima, wala hakuviinulia macho vinyago vya nyumba ya Israeli, wala hakumtia unajisi mke wa jirani yake,
Ezéchiel 18.11-18.13 Ezéchiel 18.6-18.7
16 wala hakumdhulumu mtu, wala hakutwaa kitu kiwekwe rehani, wala hakumnyang’anya mtu mali yake kwa nguvu, bali amewapa wenye njaa chakula chake, na kuwafunika nguo walio uchi;
Ezéchiel 18.7 Esaïe 58.7-58.10 Proverbes 22.9 Luc 11.41 Psaumes 41.1
17 tena ikiwa ameuzuia mkono wake asimwonee maskini, wala hakupokea faida na ziada, naye amezifanya hukumu zangu, na kuzifuata sheria zangu; hatakufa huyu kwa sababu ya uovu wa baba yake, hakika ataishi.
Ezéchiel 18.8-18.9 Proverbes 14.31 Lévitique 18.4 Ezéchiel 20.30 Ezéchiel 33.15-33.16
18 Kwa habari za yule baba yake, kwa sababu aliwaonea watu kwa ukali mwingi, na kumnyang’anya ndugu yake mali yake kwa nguvu; na kuyatenda yasiyo mema kati ya watu wake, tazama, atakufa katika uovu wake.
Ezéchiel 3.18 Esaïe 3.11 Jean 8.24 Jean 8.21 Ezéchiel 18.4
19 Lakini ninyi mwasema, Kwani yule mwana asiuchukue uovu wa baba yake? Yule mwana atakapofanya yaliyo halali na haki, na kuzishika amri zangu na kuzitenda, hakika ataishi.
Exode 20.5 Zacharie 1.3-1.6 Jérémie 15.4 Deutéronome 5.9 Ezéchiel 20.18-20.20
20 Roho itendayo dhambi, ndiyo itakayokufa; mwana hatauchukua uovu wa baba yake, wala baba hatauchukua uovu wa mwanawe, haki yake mwenye haki itakuwa juu yake, na uovu wake mwenye uovu utakuwa juu yake.
Deutéronome 24.16 2 Rois 14.6 Ezéchiel 18.4 Romains 2.6-2.9 1 Rois 8.32
21 Lakini mtu mbaya akighairi, na kuacha dhambi zake zote alizozitenda, na kuzishika amri zangu zote, na kutenda yaliyo halali na haki, hakika ataishi, hatakufa.
Ezéchiel 18.27-18.28 Ezéchiel 33.19 Ezéchiel 18.30 Proverbes 28.13 Ezéchiel 18.5
22 Dhambi zake zote alizozitenda hazitakumbukwa juu yake hata mojawapo; katika haki yake aliyoitenda ataishi.
Ezéchiel 33.16 Esaïe 43.25 Psaumes 18.20-18.24 Michée 7.19 Ezéchiel 18.24
23 Je! Mimi ninafurahia kufa kwake mtu mwovu? Asema Bwana MUNGU; si afadhali kwamba aghairi, na kuiacha njia yake, akaishi?
Ezéchiel 18.32 Ezéchiel 33.11 1 Timothée 2.4 2 Pierre 3.9 Psaumes 147.11
24 Bali mwenye haki atakapoghairi, na kuiacha haki yake, na kutenda uovu, na kufanya machukizo yote kama yale afanyayo mtu mwovu, je, ataishi? Katika matendo yake yote ya haki aliyoyatenda halitakumbukwa hata mojawapo. Katika kosa lile alilolikosa, naam, katika dhambi yake aliyoitenda, atakufa.
Ezéchiel 33.18 1 Samuel 15.11 Proverbes 21.16 2 Chroniques 24.2 Jean 8.24
25 Lakini ninyi mwasema, Njia ya Bwana si sawa. Sikilizeni sasa, Enyi nyumba ya Israeli; Je! Njia yangu siyo iliyo sawa? Njia zenu sizo zisizo sawa?
Ezéchiel 33.17 Sophonie 3.5 Ezéchiel 33.20 Genèse 18.25 Malachie 2.17
26 Mwenye haki atakapoghairi, na kuiacha haki yake, na kutenda uovu, akafa katika uovu huo; katika uovu wake alioutenda atakufa.
27 Tena, mtu mwovu atakapoghairi, na kuuacha uovu wake alioutenda, na kutenda yaliyo halali na haki, ataponya roho yake, nayo itakuwa hai.
Esaïe 1.18 Esaïe 55.7 Ezéchiel 18.21 Actes 20.21 Ezéchiel 33.5
28 Kwa sababu atafakari, na kughairi, na kuyaacha makosa yake yote aliyoyatenda, hakika ataishi, hatakufa.
Ezéchiel 12.3 Psaumes 119.6 Psaumes 119.1 Ezéchiel 33.12 Colossiens 3.5-3.9
29 Lakini nyumba ya Israeli husema, Njia ya Bwana si sawa. Ee nyumba ya Israeli, je! Njia zangu sizo zilizo sawa? Njia zenu sizo zisizo sawa?
Ezéchiel 18.2 Proverbes 19.3 Ezéchiel 18.25
30 Basi, nitawahukumu ninyi, nyumba ya Israeli, kila mmoja kwa kadiri ya njia zake, asema Bwana MUNGU. Rudini, mkaghairi, na kuyaacha makosa yenu yote; basi hivyo uovu wenu hautakuwa uharibifu wenu.
Ezéchiel 18.21 Osée 12.6 Joël 2.12-2.13 Ezéchiel 33.20 Luc 13.3
31 Tupilieni mbali nanyi makosa yenu yote mliyoyakosa; jifanyieni moyo mpya na roho mpya; mbona mnataka kufa, enyi nyumba ya Israeli?
Psaumes 51.10 Ezéchiel 11.19 Esaïe 1.16-1.17 Romains 8.13 Ezéchiel 33.11
32 Maana mimi sikufurahii kufa kwake afaye, asema Bwana MUNGU; basi ghairini, mkaishi.
Ezéchiel 18.23 2 Pierre 3.9 Ezéchiel 33.11 Lamentations 3.33

Cette Bible est dans le domaine public.