Le malheur de Jérusalem
1 Jinsi mji huu ukaavyo ukiwa, Huo uliokuwa umejaa watu! Jinsi alivyokuwa kama mjane, Yeye aliyekuwa mkuu kati ya mataifa! Binti mfalme kati ya majimbo, Jinsi alivyoshikwa shokoa!
1 Rois 4.21 Esdras 4.20 Esaïe 3.26 Esaïe 54.4 Apocalypse 18.16-18.17
2 Hulia sana wakati wa usiku, Na machozi yake yapo mashavuni; Miongoni mwa wote waliompenda Hakuna hata mmoja amfarijiye; Rafiki zake wote wamemtenda hila, Wamekuwa adui zake.
Psaumes 6.6 Michée 7.5 Psaumes 31.11 Lamentations 1.9 Jérémie 4.30
3 Yuda amehamishwa kwa sababu ya kuonewa, Na kwa sababu ya utumwa mkuu; Anakaa kati ya makafiri, Haoni raha iwayo yote; Wote waliomfuata wamempata Katika dhiki yake.
Deutéronome 28.64-28.67 Lamentations 2.9 Jérémie 13.19 Jérémie 24.9 Jérémie 52.15
4 Njia za Sayuni zaomboleza, Kwa kuwa hakuna ajaye kwa sikukuu; Malango yake yote yamekuwa ukiwa, Makuhani wake hupiga kite; Wanawali wake wanahuzunika; Na yeye mwenyewe huona uchungu.
Joël 1.8-1.13 Jérémie 9.11 Lamentations 2.6-2.7 Esaïe 24.4-24.6 Jérémie 10.22
5 Watesi wake wamekuwa kichwa, Adui zake hufanikiwa; Kwa kuwa Bwana amemtesa Kwa sababu ya wingi wa makosa yake; Watoto wake wadogo wamechukuliwa mateka Mbele yake huyo mtesi.
Ezéchiel 8.17-8.18 Ezéchiel 9.9 Jérémie 30.14-30.15 Psaumes 90.7-90.8 Jérémie 39.9
6 Naye huyo binti Sayuni Enzi yake yote imemwacha; Wakuu wake wamekuwa kama ayala Wasioona malisho; Nao wamekwenda zao hawana nguvu Mbele yake anayewafuatia.
Ezéchiel 24.25 Jérémie 48.41 Deutéronome 32.30 Psaumes 44.9-44.11 Jérémie 47.3
7 Siku za mateso na misiba yake, Yerusalemu huyakumbuka matamaniko yake yote Yaliyokuwa tangu siku za kale; Hapo watu wake walipoanguka mikononi mwa mtesi, Wala hakuna hata mmoja wa kumsaidia; Hao watesi wake walimwona, Wakafanya sabato zake kuwa mzaha.
Psaumes 77.5-77.9 Psaumes 79.4 Psaumes 42.4 Esaïe 5.1-5.4 Luc 15.17
8 Yerusalemu amefanya dhambi sana; Kwa hiyo amekuwa kama kitu kichafu; Wote waliomheshimu wanamdharau, Kwa sababu wameuona uchi wake; Naam, yeye anaugua, Na kujigeuza aende nyuma.
Lamentations 1.20-1.22 Esaïe 59.2-59.13 Jérémie 13.22 Jérémie 13.26 Lamentations 1.11
9 Uchafu wake ulikuwa katika marinda yake; Hakukumbuka mwisho wake; Kwa hiyo ameshuka kwa ajabu; Yeye hana mtu wa kumfariji; Tazama, Bwana, teso langu; Maana huyo adui amejitukuza.
Esaïe 47.7 Deutéronome 32.29 Lamentations 1.17 Psaumes 25.18 Ecclésiaste 4.1
10 Huyo mtesi amenyosha mkono wake Juu ya matamaniko yake yote; Maana ameona ya kuwa makafiri wameingia Ndani ya patakatifu pake; Ambao kwa habari zao wewe uliamuru Wasiingie katika kusanyiko lako.
Jérémie 51.51 Deutéronome 23.3 Psaumes 74.4-74.8 Lamentations 1.7 Esaïe 64.10-64.11
11 Watu wake wote hupiga kite, Wanatafuta chakula; Wameyatoa matamaniko yao wapate chakula Cha kuihuisha nafsi; Ee Bwana, tazama, uangalie; Kwa maana mimi nimekuwa mnyonge.
Jérémie 52.6 Jérémie 38.9 Lamentations 2.12 Job 40.4 Psaumes 25.15-25.19
12 Je! Si kitu kwenu, enyi nyote mpitao njia, Angalieni, mtazame Kama kuna majonzi yo yote mfano wa majonzi yangu, Niliyotendwa mimi, Ambayo Bwana amenihuzunisha kwa hayo Siku ya hasira yake iwakayo.Luc 23.28-23.31 Daniel 9.12 Jérémie 30.24 Jérémie 18.16 Luc 21.22-21.23
13 Toka juu amepeleka moto mifupani mwangu, Nao umeishinda; Ametandika wavu aninase miguu, Amenirudisha nyuma; Amenifanya kuwa mtu wa pekee, Na mgonjwa mchana kutwa.
Habakuk 3.16 Job 30.30 Psaumes 22.14 Ezéchiel 17.20 Job 19.6
14 Kongwa la makosa yangu limefungwa na mkono wake; Hayo yameshikamana; Yamepanda juu shingoni mwangu; Amezikomesha nguvu zangu;
Esaïe 47.6 Deutéronome 28.48 Ezéchiel 25.7 Ezéchiel 25.4 Proverbes 5.22
15 Bwana amenitia mikononi mwao, Ambao siwezi kupingamana nao. Bwana amewafanya mashujaa wangu wote Kuwa si kitu kati yangu; Ameita mkutano mkuu kinyume changu Ili kuwaponda vijana wangu; Bwana amemkanyaga kama shinikizoni Huyo bikira binti Yuda.
Esaïe 63.3 Malachie 4.3 Esaïe 28.18 Michée 7.10 2 Rois 25.4-25.7
16 Mimi ninayalilia mambo hayo; Jicho langu, jicho langu linachuruzika maji; Kwa kuwa mfariji yu mbali nami, Ambaye ilimpasa kunihuisha nafsi; Watoto wangu wameachwa peke yao, Kwa sababu huyo adui ameshinda.
Lamentations 1.2 Lamentations 2.18 Jérémie 13.17 Lamentations 3.48-3.49 Jérémie 14.17
17 Sayuni huinyosha mikono yake; Hakuna hata mmoja wa kumfariji; Bwana ametoa amri juu ya Yakobo, Kwamba wamzungukao wawe watesi wake; Yerusalemu amekuwa kati yao Kama kitu kichafu.
Jérémie 4.31 Esaïe 1.15 Lamentations 1.9 Lamentations 1.16 2 Rois 24.2-24.4
18 Bwana ndiye mwenye haki; Maana nimeiasi amri yake; Sikieni, nawasihi, enyi watu wote, Mkayatazame majonzi yangu; Wasichana wangu na wavulana wangu Wamechukuliwa mateka.
Lamentations 1.12 Jérémie 12.1 1 Samuel 12.14-12.15 Psaumes 119.75 Lamentations 1.5-1.6
19 Naliwaita hao walionipenda Lakini walinidanganya; Makuhani wangu na wazee wangu Walifariki mjini; Hapo walipokuwa wakitafuta chakula ili kuzihuisha nafsi zao.
Lamentations 1.2 Lamentations 2.20 Lamentations 1.11 Job 19.13-19.19 Jérémie 27.13-27.15
20 Angalia, Ee Bwana; maana mimi ni katika dhiki; Mtima wangu umetaabika; Moyo wangu umegeuka ndani yangu; Maana nimeasi vibaya sana; Huko nje upanga hufisha watu; Nyumbani mna kama mauti.
Lamentations 2.11 Esaïe 16.11 Ezéchiel 7.15 Deutéronome 32.25 Job 30.27
21 Wamesikia kwamba napiga kite; Hakuna hata mmoja wa kunifariji; Adui zangu wote wamesikia habari ya mashaka yaliyonipata; Hufurahi kwa kuwa umeyafanya hayo; Utaileta siku ile uliyoitangaza, Nao watakuwa kama mimi.
Lamentations 1.8 Lamentations 1.16 Jérémie 50.11 Lamentations 2.15 Lamentations 1.22
22 Huo uovu wao wote Na uje mbele zako wewe; Ukawatende wao kama ulivyonitenda mimi Kwa dhambi zangu zote; Kwa maana mauguzi yangu ni mengi sana, Na moyo wangu umezimia.
Psaumes 109.14-109.15 Néhémie 4.4-4.5 Jérémie 8.18 Apocalypse 6.10 Esaïe 13.7