Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jérémie 43.4
Bible en Swahili de l’est


1 Ikawa Yeremia alipokwisha kuwaambia watu wote maneno yote ya Bwana, Mungu wao, ambayo Bwana, Mungu wao, amemtuma kwao, yaani, maneno hayo yote,
Jérémie 26.8 Jérémie 42.22 Jérémie 51.63 Actes 20.27 Jérémie 1.17
2 ndipo Azaria, mwana wa Hoshaya, na Yohana mwana wa Karea, na watu wote wenye kiburi wakanena, wakimwambia Yeremia, Unasema uongo; Bwana, Mungu wetu, hakukutuma useme, Msiende Misri kukaa huko;
Esaïe 7.9 Jérémie 40.8 2 Chroniques 36.13 Jérémie 5.12-5.13 Jérémie 42.1
3 bali Baruku, mwana wa Neria, akushawishi kinyume chetu, ili kututia katika mikono ya Wakaldayo, ili watuue, na kutuchukua mateka mpaka Babeli.
Jérémie 36.4 Jérémie 36.26 Jérémie 36.10 Jérémie 38.4 Jérémie 43.6
4 Basi Yohana, mwana wa Karea, na wakuu wote wa majeshi, na watu wote hawakuitii sauti ya Bwana, kwamba wakae katika nchi ya Yuda.
Jérémie 42.5-42.6 Jérémie 44.5 2 Chroniques 25.16 Psaumes 37.3 Ecclésiaste 9.16
5 Lakini Yohana, mwana wa Karea, na wakuu wote wa majeshi, wakawatwaa wote waliosalia wa Yuda, waliokuwa wamerudi kutoka taifa zote walikofukuzwa, wakae katika Yuda;
Jérémie 40.11-40.12 Jérémie 41.15-41.16 1 Samuel 26.19
6 wanaume, na wanawake, na watoto, na binti za mfalme, na kila mtu ambaye Nebuzaradani, amiri wa askari walinzi, amemwacha pamoja na Gedalia, mwana wa Ahikamu, mwana wa Shafani, pia na Yeremia, nabii, na Baruku, mwana wa Neria;
Jérémie 40.7 Jérémie 39.10 Lamentations 3.1 Jérémie 41.10 Ecclésiaste 9.1-9.2
7 wakaingia nchi ya Misri; maana hawakuitii sauti ya Bwana; wakafika hata Tahpanesi.
Jérémie 44.1 Jérémie 2.16 Esaïe 30.4 Jérémie 46.14 Ezéchiel 30.18

Annonce de la conquête de l’Égypte par Nebucadnetsar

8 Ndipo neno la Bwana likamjia Yeremia huko Tahpenesi, kusema,
Psaumes 139.7 2 Timothée 2.9 Jérémie 2.16
9 Twaa mawe makubwa mikononi mwako, ukayafiche ndani ya chokaa ya kazi ya matofali, penye maingilio ya nyumba ya Farao huko Tahpanesi, machoni pa watu wa Yuda;
Jérémie 18.2-18.12 Jérémie 19.1-19.15 Actes 21.11 2 Samuel 12.31 Exode 1.14
10 ukawaambie, Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Tazama, nitatuma na kumtwaa Nebukadreza, mfalme wa Babeli, mtumishi wangu, nami nitaweka kiti chake cha enzi juu ya mawe haya niliyoyaficha; naye atatandaza hema yake ya fahari juu yake.
Jérémie 1.15 Esaïe 44.28-45.1 Psaumes 18.11 Psaumes 27.5 Psaumes 31.20
11 Naye atakuja, na kuipiga nchi ya Misri; watu walioandikiwa kufa watakufa, nao walioandikiwa kuwa mateka watakuwa mateka, nao walioandikiwa kupigwa kwa upanga watapigwa kwa upanga.
Jérémie 15.2 Jérémie 44.13 Ezéchiel 29.19-29.20 Esaïe 19.1-19.25 Zacharie 11.9
12 Nami nitawasha moto katika nyumba za miungu ya Misri, na kuziteketeza, na kuwachukua mateka; naye atajipamba kwa nchi ya Misri, kama vile mchungaji avaavyo nguo zake; naye atatoka huko na amani.
Jérémie 46.25 Ezéchiel 30.13 Exode 12.12 Psaumes 109.18-109.19 Esaïe 49.18
13 Naye atazivunja nguzo za Bethshemeshi, iliyoko huko katika nchi ya Misri, na nyumba za miungu ya Misri ataziteketeza.
Esaïe 19.18

Cette Bible est dans le domaine public.