Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jérémie 37.21
Bible en Swahili de l’est


Annonce du retour et de la victoire des Babyloniens

1 Na Sedekia, mwana wa Yosia, akamiliki badala ya Konia, mwana wa Yehoyakimu, ambaye Nebukadreza amemmilikisha katika nchi ya Yuda.
Jérémie 22.24 2 Rois 24.17 2 Rois 24.12 2 Chroniques 36.9-36.10 Ezéchiel 17.12-17.21
2 Lakini yeye, wala watumishi wake, wala watu wa nchi, hawakuyasikiliza maneno ya Bwana aliyonena kwa kinywa cha nabii Yeremia.
2 Chroniques 36.12-36.16 2 Rois 24.19-24.20 Proverbes 29.12 1 Rois 14.18 Ezéchiel 21.25
3 Sedekia, mfalme, akamtuma Yehukali, mwana wa Shelemia, na Sefania, mwana wa Maaseya, kuhani, kwa Yeremia, nabii, kusema, Utuombee sasa kwa Bwana, Mungu wetu.
Jérémie 21.1-21.2 1 Rois 13.6 Jérémie 29.25 Jérémie 52.24 Jérémie 42.2-42.4
4 Basi Yeremia alikuwa akiingia na kutoka kati ya watu; kwa maana walikuwa hawakumfunga gerezani.
Jérémie 37.15 Jérémie 32.2-32.3
5 Na jeshi la Farao lilikuwa limetoka nchi ya Misri; na Wakaldayo waliohusuru Yerusalemu, waliposikia habari zao, wakavunja kambi yao mbele ya Yerusalemu.
Ezéchiel 17.15 Jérémie 34.21 Jérémie 37.11 2 Rois 24.7 Jérémie 37.7
6 Ndipo neno la Bwana likamjia nabii Yeremia, kusema,
7 Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi; Mtamwambia hivi mfalme wa Yuda, aliyewatuma kwangu kuniuliza; Angalieni, jeshi la Farao, ambalo linakuja kuwasaidia, litarudi Misri, nchi yao wenyewe.
Lamentations 4.17 2 Rois 22.18 Jérémie 21.2 Ezéchiel 17.17 Jérémie 37.3
8 Na Wakaldayo watakuja tena, na kupigana na mji huu; nao watautwaa, na kuuteketeza.
Jérémie 39.2-39.8 Jérémie 38.23 Jérémie 34.21-34.22 Jérémie 32.29
9 Bwana asema hivi, Msijidanganye mkisema, Bila shaka Wakaldayo watatuacha na kwenda zao; maana hawatawaacha.
Abdias 1.3 Matthieu 24.4-24.5 Ephésiens 5.6 Jacques 1.22 Galates 6.3
10 Maana mngelipiga jeshi lote la Wakaldayo wanaopigana nanyi, wakabaki kati yao watu waliojeruhiwa tu, hata hivyo wangeondoka kila mtu katika hema yake, na kuuteketeza mji huu.
Lévitique 26.36-26.38 Esaïe 30.17 Jérémie 37.8 Esaïe 10.4 Esaïe 13.15

Jérémie en prison

11 Hata ikawa, jeshi la Wakaldayo lilipokuwa limevunja kambi yao mbele ya Yerusalemu, kwa kuliogopa jeshi la Farao,
Jérémie 37.5
12 ndipo Yeremia akatoka Yerusalemu, ili aende mpaka nchi ya Benyamini, alipokee huko fungu lake kati ya watu.
Jérémie 1.1 Josué 21.17-21.18 1 Rois 19.3 Matthieu 10.23 1 Chroniques 6.60
13 Naye alipokuwa katika lango la Benyamini, akida wa walinzi alikuwapo, jina lake Iriya, mwana wa Shelemia, mwana wa Hanania; akamkamata Yeremia, nabii, akisema, Unakwenda kujiunga na Wakaldayo.
Jérémie 38.7 Zacharie 14.10 Jérémie 38.1 Actes 6.11 Luc 23.2
14 Ndipo Yeremia akasema, Ni uongo, siendi kujiunga na Wakaldayo; lakini yeye asimsadiki; basi Iriya akamkamata Yeremia, akamleta kwa wakuu.
Psaumes 52.1-52.2 Psaumes 27.12 Matthieu 5.11-5.12 Jérémie 40.4-40.6 1 Pierre 3.16
15 Nao wakuu wakamkasirikia Yeremia, wakampiga, wakamtia gerezani katika nyumba ya Yonathani, mwandishi; kwa maana ndiyo waliyoifanya kuwa gereza.
Jérémie 38.26 Actes 5.18 Genèse 39.20 Jérémie 26.16 Jérémie 20.1-20.3
16 Basi, Yeremia alipokuwa ameingia katika nyumba ya shimo, na katika vyumba vya ndani; na Yeremia alipokuwa amekaa humo siku nyingi;
Jérémie 38.6 Jérémie 38.10-38.13 Genèse 40.15 Lamentations 3.55 Lamentations 3.53
17 ndipo Sedekia, mfalme, akatuma watu wamlete; naye mfalme akamwuliza kwa siri ndani ya nyumba yake, akasema, Je! Liko neno lililotoka kwa Bwana? Yeremia akasema, Liko. Akasema pia, Utatiwa katika mikono ya mfalme wa Babeli.
Jérémie 21.7 Jérémie 38.14-38.16 1 Rois 22.16 Jérémie 38.5 Jérémie 21.1-21.2
18 Pamoja na haya Yeremia akamwambia mfalme Sedekia, Nimefanya kosa gani juu yako, au juu ya watumishi wako, au juu ya watu hawa, hata mkanitia gerezani?
Jean 10.32 Actes 25.8 Actes 25.25 Actes 25.11 Daniel 6.22
19 Wako wapi sasa manabii wenu waliowatabiria, wakisema, Mfalme wa Babeli hatakuja juu yenu, wala juu ya nchi hii?
Jérémie 2.28 Jérémie 28.10-28.17 2 Rois 3.13 Deutéronome 32.36-32.37 Lamentations 2.14
20 Na sasa unisikilize, Ee bwana wangu mfalme; maombi yangu yakapate kibali mbele yako; usinirudishe nyumbani mwa Yonathani, mwandishi, nisije nikafa humo.
Jérémie 36.7 Actes 23.16-23.22 Actes 28.18-28.19 Jérémie 38.26 Jérémie 38.6-38.9
21 Ndipo Sedekia mfalme akatoa amri, wakamtia Yeremia katika uwanda wa walinzi; wakampa kila siku mkate mmoja uliotoka katika njia ya waokaji, hata mkate wote wa mji ulipokwisha. Basi Yeremia akakaa katika uwanda wa walinzi.
Jérémie 38.28 Jérémie 38.13 Jérémie 52.6 Jérémie 32.2 Jérémie 38.9

Cette Bible est dans le domaine public.