Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jérémie 37.2
Bible en Swahili de l’est


Annonce du retour et de la victoire des Babyloniens

1 Na Sedekia, mwana wa Yosia, akamiliki badala ya Konia, mwana wa Yehoyakimu, ambaye Nebukadreza amemmilikisha katika nchi ya Yuda.
Jérémie 22.24 2 Rois 24.17 2 Rois 24.12 Jérémie 52.31 2 Chroniques 36.9-36.10
2 Lakini yeye, wala watumishi wake, wala watu wa nchi, hawakuyasikiliza maneno ya Bwana aliyonena kwa kinywa cha nabii Yeremia.
2 Rois 24.19-24.20 Proverbes 29.12 2 Chroniques 36.12-36.16 1 Rois 16.7 2 Samuel 12.25
3 Sedekia, mfalme, akamtuma Yehukali, mwana wa Shelemia, na Sefania, mwana wa Maaseya, kuhani, kwa Yeremia, nabii, kusema, Utuombee sasa kwa Bwana, Mungu wetu.
Jérémie 21.1-21.2 Jérémie 29.25 Jérémie 52.24 1 Rois 13.6 Actes 8.24
4 Basi Yeremia alikuwa akiingia na kutoka kati ya watu; kwa maana walikuwa hawakumfunga gerezani.
Jérémie 37.15 Jérémie 32.2-32.3
5 Na jeshi la Farao lilikuwa limetoka nchi ya Misri; na Wakaldayo waliohusuru Yerusalemu, waliposikia habari zao, wakavunja kambi yao mbele ya Yerusalemu.
Ezéchiel 17.15 Jérémie 37.11 2 Rois 24.7 Jérémie 34.21 Jérémie 37.7
6 Ndipo neno la Bwana likamjia nabii Yeremia, kusema,
7 Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi; Mtamwambia hivi mfalme wa Yuda, aliyewatuma kwangu kuniuliza; Angalieni, jeshi la Farao, ambalo linakuja kuwasaidia, litarudi Misri, nchi yao wenyewe.
Lamentations 4.17 2 Rois 22.18 Jérémie 21.2 Jérémie 37.3 Esaïe 31.1-31.3
8 Na Wakaldayo watakuja tena, na kupigana na mji huu; nao watautwaa, na kuuteketeza.
Jérémie 38.23 Jérémie 39.2-39.8 Jérémie 34.21-34.22 Jérémie 32.29
9 Bwana asema hivi, Msijidanganye mkisema, Bila shaka Wakaldayo watatuacha na kwenda zao; maana hawatawaacha.
Matthieu 24.4-24.5 Ephésiens 5.6 Abdias 1.3 Galates 6.7 Jacques 1.22
10 Maana mngelipiga jeshi lote la Wakaldayo wanaopigana nanyi, wakabaki kati yao watu waliojeruhiwa tu, hata hivyo wangeondoka kila mtu katika hema yake, na kuuteketeza mji huu.
Esaïe 30.17 Lévitique 26.36-26.38 Jérémie 49.20 Jérémie 21.4-21.7 Jérémie 51.4

Jérémie en prison

11 Hata ikawa, jeshi la Wakaldayo lilipokuwa limevunja kambi yao mbele ya Yerusalemu, kwa kuliogopa jeshi la Farao,
Jérémie 37.5
12 ndipo Yeremia akatoka Yerusalemu, ili aende mpaka nchi ya Benyamini, alipokee huko fungu lake kati ya watu.
Jérémie 1.1 Jérémie 32.8-32.9 1 Rois 19.9 1 Thessaloniciens 5.22 Josué 21.17-21.18
13 Naye alipokuwa katika lango la Benyamini, akida wa walinzi alikuwapo, jina lake Iriya, mwana wa Shelemia, mwana wa Hanania; akamkamata Yeremia, nabii, akisema, Unakwenda kujiunga na Wakaldayo.
Zacharie 14.10 Jérémie 38.7 Jérémie 18.18 Jérémie 21.9 Actes 24.13
14 Ndipo Yeremia akasema, Ni uongo, siendi kujiunga na Wakaldayo; lakini yeye asimsadiki; basi Iriya akamkamata Yeremia, akamleta kwa wakuu.
Matthieu 5.11-5.12 Jérémie 40.4-40.6 Psaumes 52.1-52.2 Psaumes 27.12 Luc 6.26
15 Nao wakuu wakamkasirikia Yeremia, wakampiga, wakamtia gerezani katika nyumba ya Yonathani, mwandishi; kwa maana ndiyo waliyoifanya kuwa gereza.
Jérémie 38.26 Genèse 39.20 Jérémie 26.16 Jérémie 20.1-20.3 2 Chroniques 16.10
16 Basi, Yeremia alipokuwa ameingia katika nyumba ya shimo, na katika vyumba vya ndani; na Yeremia alipokuwa amekaa humo siku nyingi;
Jérémie 38.6 Jérémie 38.10-38.13 Lamentations 3.55 Lamentations 3.53 Genèse 40.15
17 ndipo Sedekia, mfalme, akatuma watu wamlete; naye mfalme akamwuliza kwa siri ndani ya nyumba yake, akasema, Je! Liko neno lililotoka kwa Bwana? Yeremia akasema, Liko. Akasema pia, Utatiwa katika mikono ya mfalme wa Babeli.
Jérémie 21.7 1 Rois 22.16 Jérémie 38.5 Jérémie 21.1-21.2 1 Rois 14.1-14.4
18 Pamoja na haya Yeremia akamwambia mfalme Sedekia, Nimefanya kosa gani juu yako, au juu ya watumishi wako, au juu ya watu hawa, hata mkanitia gerezani?
Actes 25.8 Jean 10.32 Daniel 6.22 Actes 25.25 Actes 25.11
19 Wako wapi sasa manabii wenu waliowatabiria, wakisema, Mfalme wa Babeli hatakuja juu yenu, wala juu ya nchi hii?
2 Rois 3.13 Jérémie 2.28 Jérémie 28.10-28.17 Jérémie 28.1-28.5 Jérémie 29.31
20 Na sasa unisikilize, Ee bwana wangu mfalme; maombi yangu yakapate kibali mbele yako; usinirudishe nyumbani mwa Yonathani, mwandishi, nisije nikafa humo.
Jérémie 36.7 Actes 25.10-25.11 Jérémie 26.15 Actes 23.16-23.22 Actes 28.18-28.19
21 Ndipo Sedekia mfalme akatoa amri, wakamtia Yeremia katika uwanda wa walinzi; wakampa kila siku mkate mmoja uliotoka katika njia ya waokaji, hata mkate wote wa mji ulipokwisha. Basi Yeremia akakaa katika uwanda wa walinzi.
Jérémie 38.13 Jérémie 38.28 Jérémie 38.9 Jérémie 52.6 Jérémie 32.2

Cette Bible est dans le domaine public.