Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jérémie 29.9
Bible en Swahili de l’est


Lettre aux Juifs exilés à Babylone

1 Maneno haya ndiyo maneno ya waraka, ambao nabii Yeremia aliupeleka toka Yerusalemu, kwa hao waliobaki wa wakuu waliochukuliwa mateka, na kwa makuhani, na kwa manabii, na kwa watu wote, ambao Nebukadreza aliwachukua mateka toka Yerusalemu hata Babeli;
Esther 9.20 Jérémie 24.1-24.7 Jérémie 28.4 Hébreux 13.22 Galates 6.11
2 (hapo walipokwisha kutoka Yerusalemu Yekonia mfalme, na mama yake mfalme, na matowashi, na wakuu wa Yuda na Yerusalemu, na mafundi, na wahunzi;)
Jérémie 22.24-22.28 2 Rois 24.12-24.16 2 Chroniques 36.9-36.10 Jérémie 27.20 Jérémie 28.4
3 kwa mkono wa Elasa, mwana wa Shafani, na Gemaria, mwana wa Hilkia, (ambao Sedekia, mfalme wa Yuda, aliwatuma hata Babeli, kwa Nebukadreza, mfalme wa Babeli), kusema,
Jérémie 36.25 1 Chroniques 6.13 Jérémie 39.14 Ezéchiel 8.11 Jérémie 26.24
4 Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, awaambia hivi watu wote waliochukuliwa mateka, niliowafanya wachukuliwe toka Yerusalemu mpaka Babeli;
Jérémie 24.5 Esaïe 45.7 Esaïe 5.5 Amos 3.6 Esaïe 10.5-10.6
5 Jengeni nyumba, mkakae ndani yake, kapandeni bustani, mkale matunda yake;
Jérémie 29.28 Ezéchiel 28.26 Jérémie 29.10
6 oeni wake, mkazae wana na binti; kawaozeni wake wana wenu, mkawaoze waume binti zenu, wazae wana na binti; mkaongezeke huko wala msipungue.
Jérémie 16.2-16.4 Genèse 21.21 Genèse 1.27-1.28 1 Corinthiens 7.36-7.38 Genèse 24.60
7 Kautakieni amani mji ule, ambao nimewafanya mchukuliwe mateka, mkauombee kwa Bwana; kwa maana katika amani yake mji huo ninyi mtapata amani.
1 Timothée 2.1-2.2 Esdras 6.10 Esdras 7.23 Daniel 4.19 Daniel 6.4-6.5
8 Maana Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Manabii walio kati yenu, na wabashiri wenu, wasiwadanganye ninyi, wala msisikilize ndoto zenu, mnazootesha.
Ephésiens 5.6 Jérémie 27.14-27.15 Jérémie 28.15 Jérémie 5.31 Jérémie 23.21
9 Kwa maana kwa jina langu hutabiri maneno ya uongo kwenu; mimi sikuwatuma, asema Bwana.
Jérémie 27.15 Jérémie 29.31 Jérémie 29.23
10 Maana Bwana asema hivi, Babeli utakapotimiziwa miaka sabini, nitawajilia ninyi, na kulitimiza neno langu jema kwenu, kwa kuwarudisha mahali hapa.
Jérémie 27.22 Jérémie 25.12 Jérémie 24.6-24.7 Daniel 9.2 Zacharie 7.5
11 Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema Bwana, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho.
Esaïe 55.8-55.12 Psaumes 33.11 Psaumes 40.5 Michée 4.12 Job 23.13
12 Nanyi mtaniita, mtakwenda na kuniomba, nami nitawasikiliza.
Jérémie 33.3 Psaumes 50.15 Matthieu 7.7-7.8 Psaumes 10.17 Psaumes 145.19
13 Nanyi mtanitafuta na kuniona, mtakaponitafuta kwa moyo wenu wote.
Psaumes 119.2 Jérémie 24.7 Joël 2.12 Deutéronome 4.29-4.31 Psaumes 119.10
14 Nami nitaonekana kwenu, asema Bwana, nami nitawarudisha watu wenu waliofungwa, nami nitawakusanya ninyi, nikiwatoa katika mataifa yote, na katika mahali pote, nilikowafukuza, asema Bwana; nami nitawaleta tena, hata mahali ambapo kutoka hapo naliwafanya mchukuliwe mateka.
Jérémie 30.3 Psaumes 126.4 Esaïe 55.6 Psaumes 32.6 Jérémie 32.37-32.44
15 Maana mmesema, Bwana ametuinulia manabii huko Babeli.
Ezéchiel 1.3 Jérémie 28.1-28.17 Jérémie 29.8-29.9 Ezéchiel 1.1
16 Maana Bwana asema hivi, katika habari za mfalme aketiye katika kiti cha enzi cha Daudi, na katika habari za watu wote wakaao ndani ya mji huu, ndugu zenu wasiokwenda pamoja nanyi kufungwa;
Jérémie 38.2-38.3 Jérémie 38.17-38.23 Ezéchiel 6.1-6.9 Jérémie 29.3 Ezéchiel 24.1-24.14
17 Bwana wa majeshi asema hivi, Tazama, nitaleta juu yao upanga, na njaa, na tauni, nami nitawafanya kuwa kama tini mbovu, zisizoweza kuliwa, kwa kuwa ni mbovu sana.
Jérémie 24.8-24.10 Jérémie 29.18 Jérémie 15.2-15.3 Jérémie 43.11 Luc 21.11
18 Nami nitawafuatia kwa upanga, na njaa, na tauni, nami nitawatoa watupwe huko na huko katika falme zote za dunia, wawe kitu cha kulaaniwa, na cha kushangaza, na cha kuzomewa, na cha kulaumiwa, katika mataifa yote nilikowafukuza.
Jérémie 42.18 Jérémie 15.4 2 Chroniques 29.8 Deutéronome 28.25 Jérémie 24.9
19 Kwa sababu hawakusikiliza maneno yangu, asema Bwana, ambayo naliwatuma watumishi wangu, hao manabii, nikiamka mapema, na kuwatuma; lakini hamkutaka kusikiliza, asema Bwana.
Jérémie 6.19 Jérémie 26.5 Jérémie 7.24-7.26 Zacharie 1.4-1.6 Jérémie 25.3-25.7
20 Basi, lisikieni neno la Bwana, ninyi nyote mliochukuliwa mateka, niliowapeleka toka Yerusalemu mpaka Babeli.
Jérémie 24.5 Michée 4.10 Ezéchiel 3.15 Ezéchiel 3.11
21 Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, katika habari za Ahabu, mwana wa Kolaya, na katika habari za Sedekia, mwana wa Maaseya, wawatabiriao ninyi maneno ya uongo kwa jina langu; Tazama, nitawatia katika mikono ya Nebukadreza, mfalme wa Babeli, naye atawaua mbele ya macho yenu.
Jérémie 14.14-14.15 Jérémie 29.8-29.9 Lamentations 2.14
22 Tena katika habari zao laana itatumiwa na wafungwa wote wa Yuda, walioko Babeli, kusema, Bwana akufanye uwe kama Sedekia, na kama Ahabu, ambao mfalme wa Babeli aliwaoka motoni;
Daniel 3.6 Esaïe 65.15 Daniel 3.21 1 Corinthiens 16.22 Genèse 48.20
23 kwa sababu wametenda upumbavu katika Israeli, nao wamezini na wake za jirani zao, nao wamenena maneno ya uongo kwa jina langu, nisiyowaamuru; nami ndimi nijuaye, nami ni shahidi, asema Bwana.
Jérémie 23.14 Hébreux 4.13 Malachie 3.5 Jérémie 16.17 Jérémie 29.21
24 Na katika habari za Shemaya, Mnehelami, utanena, ukisema,
Jérémie 29.31-29.32
25 Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, ya kwamba, Kwa kuwa kwa jina lako mwenyewe umewapelekea barua watu wote walioko Yerusalemu, na Sefania, mwana wa Maaseya, kuhani, na makuhani wote, kusema,
Jérémie 37.3 Jérémie 52.24 Jérémie 29.29 Jérémie 21.1-21.2 Néhémie 6.17
26 Bwana amekufanya kuhani badala ya Yehoyada, kuhani, ili mpate kuwa watumishi katika nyumba ya Bwana, kwa kila mtu aliye na wazimu, na kwa kila mtu ajifanyaye kuwa nabii, umtie katika mkatale na pingu.
Jérémie 20.1-20.2 2 Rois 9.11 Jean 10.20 Osée 9.7 Actes 26.24
27 Mbona, basi, hukumkemea Yeremia wa Anathothi, ajifanyaye kuwa nabii kwenu,
Actes 5.40 2 Chroniques 25.16 Actes 4.17-4.21 Actes 5.28 Nombres 16.3
28 ambaye ametuma watu kwetu katika Babeli, kusema, Uhamisho huu ni wa siku nyingi; jengeni nyumba, mkakae ndani yake; pandeni bustani, mkale matunda yake.
Jérémie 29.5 Jérémie 29.1 Jérémie 29.10
29 Na Sefania, kuhani, akasoma barua hii masikioni mwa Yeremia nabii.
Jérémie 29.25
30 Ndipo neno la Bwana likamjia Yeremia, kusema,
31 Uwapelekee habari watu wote waliohamishwa, kusema, Bwana asema hivi, katika habari za Shemaya, Mnehelami; Kwa sababu Shemaya amewatabiria ninyi, lakini sikumtuma mimi, naye amewatumainisha neno la uongo;
Jérémie 29.9 Jérémie 14.14-14.15 Jérémie 29.23-29.24 Ezéchiel 13.22-13.23 Ezéchiel 13.8-13.16
32 basi, Bwana asema hivi, Tazama, nitamwadhibu Shemaya, Mnehelami, na wazao wake; hatakuwa na mtu atakayekaa katika watu hawa, wala hatayaona mema nitakayowatendea watu wangu, asema Bwana; kwa sababu amenena maneno ya uasi juu ya Bwana.
Jérémie 28.16 Jérémie 17.6 Jérémie 22.30 2 Rois 7.19-7.20 2 Rois 7.2

Cette Bible est dans le domaine public.