Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jérémie 24.2
Bible en Swahili de l’est


1 Bwana akanionyesha, na tazama, vikapu viwili vya tini, vimewekwa mbele ya hekalu la Bwana, baada ya Nebukadreza, mfalme wa Babeli, kumchukua mateka Yekonia, mwana wa Yehoyakimu, mfalme wa Yuda, na wakuu wa Yuda, pamoja na mafundi na wafua chuma, kutoka Yerusalemu, kuwaleta Babeli.
Jérémie 29.2 2 Chroniques 36.10 2 Rois 24.12-24.16 Amos 8.1-8.2 Amos 7.7
2 Kikapu kimoja kilikuwa na tini nzuri sana, kama tini zilizotangulia kuiva; na kikapu cha pili kilikuwa na tini mbovu sana zisizoweza kuliwa, kwa kuwa zilikuwa mbovu sana.
Esaïe 5.4 Michée 7.1 Esaïe 5.7 Malachie 1.12-1.14 Ezéchiel 15.2-15.5
3 Ndipo Bwana akaniambia, Unaona nini Yeremia? Nikasema, Naona tini; tini nzuri zilizo nzuri sana; na tini mbovu zilizo mbovu sana, zisizoweza kuliwa, kwa kuwa ni mbovu sana.
Amos 8.2 Zacharie 4.2 Jérémie 1.11-1.14 Matthieu 25.32-25.33 Amos 7.8
4 Kisha neno la Bwana likanijia, kusema,
5 Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi, Kama zilivyo tini hizi nzuri, ndivyo nitakavyowaangalia mateka wa Yuda, niliowatoa katika mahali hapa, waende mpaka nchi ya Wakaldayo, wapate mema.
Nahum 1.7 Zacharie 13.9 Matthieu 25.12 Romains 8.28 2 Timothée 2.19
6 Kwa maana nitawatulizia macho yangu, wapate mema, nami nitawaingiza katika nchi hii tena; nami nitawajenga, wala sitawabomoa; nitawapanda wala sitawang’oa.
Jérémie 42.10 Jérémie 29.10 Jérémie 33.7 Jérémie 12.15 Jérémie 32.41
7 Nami nitawapa moyo, wanijue ya kuwa mimi ni Bwana; nao watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao; kwa maana watanirudia kwa moyo wao wote.
Jérémie 30.22 Hébreux 8.10 Ezéchiel 37.23 1 Samuel 7.3 Zacharie 8.8
8 Na habari za tini zile mbovu, zisizoweza kuliwa, kwa kuwa ni mbovu sana; hakika, asema, Bwana, ndivyo nitakavyomtoa Sedekia, mfalme wa Yuda, na wakuu wake, na mabaki ya Yerusalemu, waliosalia katika nchi hii, na hao wanaokaa katika nchi ya Misri.
Jérémie 43.1-44.1 Jérémie 24.2 Jérémie 21.10 Jérémie 32.28-32.29 Jérémie 44.26-44.30
9 Naam, nitawatoa watupwe huko na huko katika falme zote za dunia, wapate mabaya; wawe kitu cha kulaumiwa, na mithali, na dhihaka, na laana, katika mahali pote nitakapowafukuza.
Jérémie 15.4 Jérémie 29.18 Deutéronome 28.37 1 Rois 9.7 Jérémie 34.17
10 Nami nitatuma upanga, na njaa, na tauni, kati yao, hata watakapopotelea mbali katika nchi niliyowapa, wao na baba zao.
Esaïe 51.19 Ezéchiel 5.12-5.17 Jérémie 5.12 Jérémie 34.17 Ezéchiel 33.27

Cette Bible est dans le domaine public.