Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jérémie 21.5
Bible en Swahili de l’est


Imminence de la prise de Jérusalem

1 Neno hili ndilo lililomjia Yeremia, kutoka kwa Bwana, hapo mfalme Sedekia alipompelekea Pashuri, mwana wa Malkiya, na Sefania, mwana wa Maaseya, kuhani, kusema,
Jérémie 29.25 Jérémie 37.3 Jérémie 38.1 Jérémie 52.24 2 Rois 24.17-24.18
2 Tafadhali utuulizie habari kwa Bwana; kwa maana Nebukadreza, mfalme wa Babeli, analeta vita juu yetu; labda Bwana atatutendea sawasawa na kazi zake zote za ajabu, ili aende zake akatuache.
Jérémie 37.3 Ezéchiel 20.1-20.3 Jérémie 37.7 1 Rois 14.2-14.3 Juges 20.27
3 Basi Yeremia akawaambia, Mwambieni Sedekia neno hili,
4 Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi, Angalieni, nitazigeuza nyuma silaha za vita zilizo mikononi mwenu, ambazo kwa hizo ninyi mnapigana na mfalme wa Babeli, na Wakaldayo, wanaowahusuru nje ya kuta zenu, nami nitazikusanya pamoja katikati ya mji huu.
Jérémie 37.8-37.10 Jérémie 32.5 Jérémie 33.5 Esaïe 13.4 Jérémie 38.17-38.18
5 Na mimi mwenyewe nitapigana nanyi, kwa mkono ulionyoshwa na kwa mkono hodari, naam, kwa hasira, na kwa ukali, na kwa ghadhabu nyingi.
Exode 6.6 Esaïe 5.25 Esaïe 63.10 Jérémie 32.17 Exode 9.15
6 Nami nitawapiga wenyeji wa mji huu, wanadamu na wanyama pia; watakufa kwa tauni kubwa.
Jérémie 12.3-12.4 Jérémie 32.24 Ezéchiel 14.13 Jérémie 33.12 Ezéchiel 14.17
7 Na baada ya hayo, asema Bwana, nitamtia Sedekia, mfalme wa Yuda, na watumishi wake, na watu wote waliosalia ndani ya mji huu, baada ya tauni ile, na upanga, na njaa, katika mkono wa Nebukadreza, mfalme wa Babeli, na katika mikono ya adui zao, na katika mikono ya watu wale wanaowatafuta roho zao; naye atawaua kwa ukali wa upanga; hatawaachilia, wala hatawahurumia, wala hatawarehemu.
Jérémie 37.17 2 Rois 25.5-25.7 Habakuk 1.6-1.10 Ezéchiel 7.9 Ezéchiel 17.20-17.21
8 Nawe waambie watu hawa, Bwana asema hivi, Tazama naweka mbele yenu njia ya uzima, na njia ya mauti.
Deutéronome 30.19 Deutéronome 30.15 Deutéronome 11.26 Esaïe 1.19-1.20
9 Yeye atakayekaa katika mji huu atakufa kwa upanga, na kwa njaa, na kwa tauni; bali yeye atakayetoka, na kujitia pamoja na Wakaldayo wanaowahusuru, yeye ataishi, na maisha yake yatakuwa nyara kwake.
Jérémie 38.2 Jérémie 45.5 Jérémie 39.18 Jérémie 38.17-38.23 Jérémie 27.13
10 Maana nimeweka uso wangu juu ya mji huu niuletee mabaya, wala nisiuletee mema, asema Bwana; utatiwa katika mkono wa mfalme wa Babeli, naye atauteketeza.
Jérémie 44.11 Jérémie 44.27 Amos 9.4 Jérémie 52.13 2 Chroniques 36.19
11 Na katika habari za nyumba ya mfalme wa Yuda, lisikieni neno la Bwana,
Jérémie 17.20 Jérémie 13.18 Michée 3.1
12 Ee nyumba ya Daudi, Bwana asema hivi, Hukumuni hukumu ya haki asubuhi, mkawaponye waliotekwa nyara na mkono wake aliyewadhulumu, ghadhabu yangu isije ikatoka kama moto, ikaunguza, asiweze mtu ye yote kuuzima, kwa sababu ya uovu wa matendo yenu.
Esaïe 1.17 Jérémie 4.4 Proverbes 31.8-31.9 Sophonie 3.5 Jérémie 36.7
13 Tazama, mimi ni juu yako, Ewe ukaaye bondeni, na kwenye jabali la uwandani, asema Bwana ninyi mnaosema, Ni nani atakayeshuka apigane nasi? Au, Ni nani atakayeingia katika makao yetu?
Lamentations 4.12 Ezéchiel 13.8 Abdias 1.3-1.4 Psaumes 125.2 Jérémie 23.30-23.32
14 Nami nitawaadhibu kwa kadiri ya matunda ya matendo yenu, asema Bwana; nami nitawasha moto katika msitu wake, nao utateketeza vitu vyote viuzungukavyo.
Esaïe 3.10-3.11 2 Chroniques 36.19 Proverbes 1.31 Jérémie 32.19 Jérémie 52.13

Cette Bible est dans le domaine public.