Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 14
Bible en Swahili de l’est


1 Maana Bwana atamhurumia Yakobo, atamchagua Israeli tena, naye atawaweka katika nchi yao wenyewe; na mgeni atajiunga nao, nao wataambatana na nyumba ya Yakobo.
Zacharie 1.17 Psaumes 102.13 Esaïe 54.7-54.8 Ephésiens 2.12-2.19 Zacharie 8.22-8.23
2 Na hao mataifa watawatwaa na kuwaleta mpaka mahali pao wenyewe, na nyumba ya Israeli watawamiliki, na kuwafanya watumishi na wajakazi katika nchi ya Bwana; nao watawachukua hali ya kufungwa watu wale waliowafunga wao, nao watawamiliki watu wale waliowaonea.
Esaïe 60.14 Esaïe 61.5 Daniel 7.18 Apocalypse 11.11-11.18 Daniel 7.25-7.27
3 Tena itakuwa katika siku ile, ambayo Bwana atakupa raha baada ya huzuni yako, na baada ya taabu yako, na baada ya utumishi ule mgumu uliotumikishwa;
Esdras 9.8-9.9 Jérémie 30.10 Deutéronome 28.65-28.68 Zacharie 8.8 Esaïe 12.1
4 utatunga mithali hii juu ya mfalme wa Babeli, na kusema, Jinsi alivyokoma mwenye kuonea; Jinsi ulivyokoma mji ule wenye jeuri!
Apocalypse 18.16 Esaïe 49.26 Esaïe 13.19 Apocalypse 17.6 Esaïe 45.2-45.3
5 Bwana amelivunja gongo la wabaya, Fimbo ya enzi yao wenye kutawala.
Esaïe 9.4 Psaumes 125.3 Esaïe 10.5 Jérémie 48.15-48.17 Esaïe 14.29
6 Yeye aliyewapiga mataifa kwa ghadhabu, Kwa mapigo yasiyokoma; Aliyewatawala mataifa kwa hasira, Ameadhibiwa asizuie mtu.
Esaïe 46.10-46.11 Jérémie 25.26 Esaïe 21.1-21.10 Jacques 2.13 Daniel 4.35
7 Dunia yote inastarehe na kutulia; Hata huanzilisha kuimba.
Psaumes 126.1-126.3 Esaïe 49.13 Psaumes 98.7-98.9 Apocalypse 18.20 Psaumes 98.1
8 Naam, misunobari inakufurahia, Na mierezi ya Lebanoni, ikisema, Tokea wakati ulipolazwa chini wewe, Hapana mkata miti aliyetujia.
Ezéchiel 31.16 Esaïe 55.12-55.13 Zacharie 11.2
9 Kuzimu chini kumetaharuki kwa ajili yako, Ili kukulaki utakapokuja; Huwaamsha waliokufa kwa ajili yako, Naam, walio wakuu wote wa dunia; Huwainua wafalme wote wa mataifa, Watoke katika viti vyao vya enzi.
Ezéchiel 32.21-32.32 Jérémie 50.8 Proverbes 15.24
10 Hao wote watajibu na kukuambia, Je! Wewe nawe umekuwa dhaifu kama sisi! Wewe nawe umekuwa kama sisi!
Psaumes 82.6-82.7 Psaumes 49.20 Psaumes 49.6-49.14 Luc 16.20-16.23 Ecclésiaste 2.16
11 Fahari yako imeshushwa hata kuzimu, Na sauti ya vinanda vyako; Funza wametandazwa chini yako, Na vidudu vinakufunika.
Esaïe 66.24 Esaïe 22.2 Job 24.19-24.20 Job 17.13-17.14 Esaïe 21.4-21.5
12 Jinsi ulivyoanguka kutoka mbinguni, Ewe nyota ya alfajiri, mwana wa asubuhi! Jinsi ulivyokatwa kabisa, Ewe uliyewaangusha mataifa!
Luc 10.18 Apocalypse 22.16 Apocalypse 2.28 2 Pierre 1.19 Esaïe 34.4
13 Nawe ulisema moyoni mwako, Nitapanda mpaka mbinguni, Nitakiinua kiti changu juu kuliko nyota za Mungu; Nami nitaketi juu ya mlima wa mkutano, Katika pande za mwisho za kaskazini.
Ezéchiel 28.2 Ezéchiel 28.12-28.16 Esaïe 2.2 Ezéchiel 27.3 2 Thessaloniciens 2.4
14 Nitapaa kupita vimo vya mawingu, Nitafanana na yeye Aliye juu.
Esaïe 47.8 2 Thessaloniciens 2.4 Esaïe 37.23-37.24 Genèse 3.5
15 Lakini utashushwa mpaka kuzimu; Mpaka pande za mwisho za shimo.
Matthieu 11.23 Luc 10.15 Ezéchiel 32.23 Actes 12.22-12.23 Ezéchiel 28.8-28.9
16 Wao wakuonao watakukazia macho, Watakuangalia sana, wakisema, Je! Huyu ndiye aliyeitetemesha dunia, Huyu ndiye aliyetikisa falme;
Jérémie 50.23 Psaumes 52.7 Esaïe 14.4-14.5 Psaumes 64.9 Jérémie 51.20-51.23
17 Aliyeufanya ulimwengu ukiwa, akaipindua miji yake; Asiyewafungua wafungwa wake waende kwao?
Esaïe 45.13 Joël 2.3 Ezéchiel 6.14 Sophonie 2.13-2.14 Esaïe 58.6
18 Wafalme wote wa mataifa wamezikwa wote kwa heshima, Kila mmoja ndani ya nyumba yake mwenyewe;
Job 30.23 2 Chroniques 24.16 Ecclésiaste 12.5 2 Chroniques 24.25 Ezéchiel 32.18-32.32
19 Bali wewe umetupwa mbali na kaburi lako, Kama chipukizi lililochukiza kabisa; Kama vazi la wale waliouawa, Wale waliochomwa kwa upanga, Wale washukao mpaka misingi ya shimo; Kama mzoga uliokanyagwa chini ya miguu.
Jérémie 41.7 Jérémie 41.9 Esaïe 22.16-22.18 2 Rois 9.25 1 Rois 21.24
20 Hutaungamanishwa pamoja nao katika mazishi, Kwa maana umeiharibu nchi yako, Umewaua watu wako; Kizazi chao watendao uovu hakitatajwa milele.
Job 18.19 Psaumes 21.10 Job 18.16 Psaumes 109.13 Psaumes 37.28
21 Fanyeni tayari machinjo kwa watoto wake. Kwa sababu ya uovu wa baba zao; Wasije wakainuka na kuitamalaki nchi, Na kuujaza miji uso wa ulimwengu.
Exode 20.5 Matthieu 23.35 Lévitique 26.39 Habakuk 2.8-2.12 Esaïe 27.6
22 Nami nitainuka, nishindane nao; asema Bwana wa majeshi; na katika Babeli nitang’oa jina na mabaki, mwana na mjukuu; asema Bwana.
1 Rois 14.10 Proverbes 10.7 Jérémie 51.3-51.4 Jérémie 50.26-50.27 Jérémie 50.29-50.35
23 Tena nitaifanya hiyo nchi kuwa makao ya nungu, na maziwa ya maji; nami nitaifagilia mbali kwa ufagio wa uharibifu; asema Bwana wa majeshi.
Sophonie 2.14 Esaïe 34.11-34.15 1 Rois 14.10 Apocalypse 18.21-18.23 Jérémie 51.25-51.26

Prophétie sur l’Assyrie

24 Bwana wa majeshi ameapa, akisema, Hakika yangu kama vile vilivyoazimia, ndivyo itakavyokuwa; na kama nilivyokusudia, ndivyo itakavyotokea;
Actes 4.28 Job 23.13 Proverbes 19.21 Ephésiens 1.9 Jérémie 29.11
25 kwamba nitamvunja huyo Mwashuri vipande vipande katika nchi yangu, na juu ya mlima wangu nitamkanyaga chini ya miguu yangu; ndipo nira yake iliyo juu yao itakapoondoka, na mzigo wake utatoka mabegani mwao.
Esaïe 9.4 Nahum 1.13 Esaïe 31.8-31.9 Esaïe 10.12 Esaïe 17.12-17.14
26 Hilo ndilo kusudi lililokusudiwa duniani mwote, na huo ndio mkono ulionyoshwa juu ya mataifa yote.
Esaïe 23.9 Sophonie 3.6-3.8 Exode 15.12 Esaïe 5.25
27 Maana Bwana wa majeshi amekusudia, naye ni nani atakayelibatili? Na mkono wake ulionyoshwa, ni nani atakayeugeuza nyuma?
2 Chroniques 20.6 Esaïe 43.13 Job 9.12 Psaumes 33.11 Proverbes 21.30

Prophétie contre les Philistins

28 Ufunuo huu ulikuja mwaka ule alipokufa mfalme Ahazi.
2 Rois 16.20 Esaïe 13.1 2 Chroniques 28.27 Esaïe 6.1
29 Usifurahi, Ee Ufilisti, pia wote, Kwa sababu fimbo ile iliyokupiga imevunjika; Maana katika shina la nyoka atatoka fira, Na uzao wake ni joka la moto arukaye
Esaïe 30.6 Esaïe 11.8 2 Chroniques 26.6 2 Chroniques 28.18 2 Rois 18.8
30 Nao walio maskini kabisa watakula, Na wahitaji watajilaza salama; Nami nitatia shina lako kwa njaa, Na mabaki yako watauawa.
Esaïe 7.21-7.22 Esaïe 51.19 Joël 3.4-3.8 Esaïe 3.15 Amos 1.6-1.8
31 Piga yowe, Ee lango; lia, Ee mji; Ee Ufilisti, pia wote, umeyeyuka kabisa; Maana moshi unakuja toka kaskazini, Wala hakuna atakayechelewa katika majeshi yake.
Jérémie 1.14 Esaïe 14.29 Esaïe 13.6 Esaïe 20.1 Esaïe 3.26
32 Wajumbe wa taifa hilo waletewe jibu gani? Ya kuwa Bwana ameiweka misingi ya Sayuni, na ndani yake wale walioonewa katika watu wake wataona kimbilio.
Psaumes 87.5 Psaumes 87.1 Jacques 2.5 Psaumes 102.16 Sophonie 3.12

Cette Bible est dans le domaine public.