Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Cantique 7.8
Bible en Swahili de l’est


Les filles de Jérusalem

1 Siti msharifu, jinsi zilivyo nzuri Hatua zako katika mitalawanda. Mapaja yako ya mviringo ni kama johari, Kazi ya mikono ya fundi mstadi;
Psaumes 45.13 Philippiens 1.27 Ephésiens 6.15 Ephésiens 4.15-4.16 Exode 28.15

Le jeune homme

2 Kitovu chako ni kama bilauri iliyoviringana, Na isikose divai iliyochanganyika; Tumbo lako ni mfano wa chungu ya ngano, Iliyozungukwa na ugo wa nyinyoro;
Romains 7.4 Psaumes 45.16 Esaïe 46.3 Proverbes 3.8 Cantique 5.14
3 Maziwa yako mawili ni kama wana-paa wawili, Ambao ni mapacha ya paa;
Cantique 4.5 Cantique 6.6
4 Shingo yako ni kama huo mnara wa pembe; Macho yako kama viziwa vya Heshboni, Karibu na mlango wa Beth-rabi; Pua yako ni kama mnara wa Lebanoni, Unaoelekea Dameski;
Cantique 4.4 Psaumes 144.12 Ephésiens 1.17-1.18 Hébreux 5.14 Nombres 21.25-21.26
5 Kichwa chako juu yako ni kama Karmeli, Na nywele za kichwa chako kama urujuani, Mfalme amenaswa na mashungu yake.
Esaïe 35.2 Cantique 4.1 Cantique 1.17 Psaumes 68.24 Matthieu 18.20
6 Jinsi yalivyo mazuri, yalivyo matamu, Mapenzi katikati ya anasa!
Cantique 4.10 Cantique 1.15-1.16 Psaumes 45.11 Cantique 7.10 Cantique 4.7
7 Kimo chako kimefanana na mtende, Na maziwa yako na vichala.
Cantique 4.5 Cantique 1.13 Esaïe 66.10 Jérémie 10.5 Cantique 7.3
8 Nilisema, Nitapanda huo mtende, Na kuyashika makuti yake. Maziwa yako na yawe kama vichala vya mzabibu, Na harufu ya pumzi yako kama mapera;
Cantique 2.3 Jean 14.21-14.23 2 Corinthiens 2.14 Cantique 1.3 Jérémie 32.41
9 Na kinywa chako kama divai iliyo bora, Kwa mpendwa wangu inashuka taratibu, Ikitiririka midomoni mwao walalao.
Cantique 5.16 Actes 16.30-16.34 1 Thessaloniciens 4.13-4.14 Romains 13.11 Proverbes 16.24
10 Mimi ni wake mpendwa wangu, Na shauku yake ni juu yangu.
Cantique 6.3 Cantique 2.16 Psaumes 45.11 Galates 2.20 Cantique 7.5-7.6
11 Njoo, mpendwa wangu, twende mashambani, Tufanye maskani katika vijiji.
Cantique 4.8 Cantique 2.10-2.13 Cantique 1.4
12 Twende mapema hata mashamba ya mizabibu, Tuone kama mzabihu umechanua, Na maua yake yamefunuka; Kama mikomamanga imetoa maua; Huko nitakupa pambaja zangu.
Cantique 6.11 Ephésiens 6.24 Hébreux 2.13 1 Thessaloniciens 3.5-3.6 Proverbes 24.30-24.31
13 Mitunguja hutoa harufu yake; Juu ya milango yetu yako matunda mazuri, Mapya na ya kale, ya kila namna, Niliyokuwekea, mpendwa wangu.
Genèse 30.14 Matthieu 13.52 Matthieu 25.40 1 Corinthiens 8.8-8.9 Galates 5.22-5.23

Cette Bible est dans le domaine public.