Les filles de Jérusalem
 1 Siti msharifu, jinsi zilivyo nzuri Hatua zako katika mitalawanda. Mapaja yako ya mviringo ni kama johari, Kazi ya mikono ya fundi mstadi;
Psaumes 45.13  Philippiens 1.27  Ephésiens 6.15  Ephésiens 4.15-4.16  Exode 28.15  
Le jeune homme
 2 Kitovu chako ni kama bilauri iliyoviringana, Na isikose divai iliyochanganyika; Tumbo lako ni mfano wa chungu ya ngano, Iliyozungukwa na ugo wa nyinyoro;
Romains 7.4  Psaumes 45.16  Esaïe 46.3  Proverbes 3.8  Cantique 5.14  
 3 Maziwa yako mawili ni kama wana-paa wawili, Ambao ni mapacha ya paa;
Cantique 4.5  Cantique 6.6  
 4 Shingo yako ni kama huo mnara wa pembe; Macho yako kama viziwa vya Heshboni, Karibu na mlango wa Beth-rabi; Pua yako ni kama mnara wa Lebanoni, Unaoelekea Dameski;
Cantique 4.4  Psaumes 144.12  Ephésiens 1.17-1.18  Hébreux 5.14  Nombres 21.25-21.26  
 5 Kichwa chako juu yako ni kama Karmeli, Na nywele za kichwa chako kama urujuani, Mfalme amenaswa na mashungu yake.
Esaïe 35.2  Cantique 4.1  Cantique 1.17  Psaumes 68.24  Matthieu 18.20  
 6 Jinsi yalivyo mazuri, yalivyo matamu, Mapenzi katikati ya anasa!
Cantique 4.10  Cantique 1.15-1.16  Psaumes 45.11  Cantique 7.10  Cantique 4.7  
 7 Kimo chako kimefanana na mtende, Na maziwa yako na vichala.
Cantique 4.5  Cantique 1.13  Esaïe 66.10  Jérémie 10.5  Cantique 7.3  
 8 Nilisema, Nitapanda huo mtende, Na kuyashika makuti yake. Maziwa yako na yawe kama vichala vya mzabibu, Na harufu ya pumzi yako kama mapera;
Cantique 2.3  Jean 14.21-14.23  2 Corinthiens 2.14  Cantique 1.3  Jérémie 32.41  
 9 Na kinywa chako kama divai iliyo bora, Kwa mpendwa wangu inashuka taratibu, Ikitiririka midomoni mwao walalao.
Cantique 5.16  Actes 16.30-16.34  1 Thessaloniciens 4.13-4.14  Romains 13.11  Proverbes 16.24  
 10 Mimi ni wake mpendwa wangu, Na shauku yake ni juu yangu.
Cantique 6.3  Cantique 2.16  Psaumes 45.11  Galates 2.20  Cantique 7.5-7.6  
 11 Njoo, mpendwa wangu, twende mashambani, Tufanye maskani katika vijiji.
Cantique 4.8  Cantique 2.10-2.13  Cantique 1.4  
 12 Twende mapema hata mashamba ya mizabibu, Tuone kama mzabihu umechanua, Na maua yake yamefunuka; Kama mikomamanga imetoa maua; Huko nitakupa pambaja zangu.
Cantique 6.11  Ephésiens 6.24  Hébreux 2.13  1 Thessaloniciens 3.5-3.6  Proverbes 24.30-24.31  
 13 Mitunguja hutoa harufu yake; Juu ya milango yetu yako matunda mazuri, Mapya na ya kale, ya kila namna, Niliyokuwekea, mpendwa wangu.Genèse 30.14  Matthieu 13.52  Matthieu 25.40  1 Corinthiens 8.8-8.9  Galates 5.22-5.23